3 | Mifano ya Biblia Inaweza Kukusaidia
BIBLIA INAZUNGUMUZIA . . . Wanaume na wanamuke waaminifu wenye walikuwa na “hisia kama zetu.”—YAKOBO 5:17.
Ile Iko na Maana Gani?
Mu Biblia muko habari ya wanaume na wanamuke wenye walikuwa na hisia mbalimbali. Wakati tuko nasoma habari zao, tunaweza kupata habari ya mutu fulani mwenye alijisikiaka sawa siye.
Namna ile Inaweza Kusaidia
Siye wote tunapendaka wengine watuelewe na inakuwaka vile zaidi sana wakati mutu iko na matatizo ya akili. Wakati tunasoma habari za kweli za watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia, tunaweza kuona kama hali yao inapatana na yetu, na kama walikuwa nawaza sawa siye na kujisikia vile tunajisikiaka. Wakati tuko na mahangaiko na tunajisikia mubaya, hatutajiona kuwa peke yetu juu kuko wengine wenye walishakajisikia sawa siye.
Mu Biblia muko mawazo ya watu wengi wenye walijisikiaka kuwa wanakosa mutu wa kuwasaidia na wanakosa tumaini. Kuko siku ulishakajiambia, ‘Nachoka na hii maisha’? Musa, Eliya, na Daudi walijisikiaka vile.—Hesabu 11:14; 1 Wafalme 19:4; Zaburi 55:4.
Biblia inazungumuzia mwanamuke mwenye kuitwa Hana mwenye alikuwaka na “uchungu mwingi sana” juu hakukuwaka na mutoto na mbanda yake alikuwaka namuchokoza sana.—1 Samweli 1:6, 10.
Biblia inazungumuzia mwanaume mwenye kuitwa Yobu, mwenye hali yake inaweza kufanana na yetu. Hata kama alikuwa mwanaume wa imani, aliteseka juu alikuwa na huzuni sana, na siku moya alisema hivi: “Ninachukia maisha yangu; sitaki kuendelea kuishi.”—Yobu 7:16.
Kujifunza namna wale watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia waliweza kupiganisha ile mawazo yao yenye kuhangaisha, kunaweza kutusaidia na siye tupiganishe mahangaiko yetu.