Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp23 na. 1 uku. 10-11
  • 3 | Mifano ya Biblia Inaweza Kukusaidia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 3 | Mifano ya Biblia Inaweza Kukusaidia
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Namna ile Inaweza Kusaidia
  • 2 | “Faraja Kutoka Katika Maandiko”
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • 4 | Biblia Iko na Mashauri Yenye Kusaidia
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • Namna Gani Naweza Kuongoza Hisia Zangu?
    Vijana Wanauliza
  • 1 | Sala—“Mumutupie Mahangaiko Yenu Yote”
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
wp23 na. 1 uku. 10-11
Nabii Musa iko na mahangaiko, iko naangalia mbinguni na iko nasali kwa Mungu.

3 | Mifano ya Biblia Inaweza Kukusaidia

BIBLIA INAZUNGUMUZIA  . . . Wanaume na wanamuke waaminifu wenye walikuwa na “hisia kama zetu.”—YAKOBO 5:17.

Ile Iko na Maana Gani?

Mu Biblia muko habari ya wanaume na wanamuke wenye walikuwa na hisia mbalimbali. Wakati tuko nasoma habari zao, tunaweza kupata habari ya mutu fulani mwenye alijisikiaka sawa siye.

Namna ile Inaweza Kusaidia

Siye wote tunapendaka wengine watuelewe na inakuwaka vile zaidi sana wakati mutu iko na matatizo ya akili. Wakati tunasoma habari za kweli za watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia, tunaweza kuona kama hali yao inapatana na yetu, na kama walikuwa nawaza sawa siye na kujisikia vile tunajisikiaka. Wakati tuko na mahangaiko na tunajisikia mubaya, hatutajiona kuwa peke yetu juu kuko wengine wenye walishakajisikia sawa siye.

  • Mu Biblia muko mawazo ya watu wengi wenye walijisikiaka kuwa wanakosa mutu wa kuwasaidia na wanakosa tumaini. Kuko siku ulishakajiambia, ‘Nachoka na hii maisha’? Musa, Eliya, na Daudi walijisikiaka vile.—Hesabu 11:14; 1 Wafalme 19:4; Zaburi 55:4.

  • Biblia inazungumuzia mwanamuke mwenye kuitwa Hana mwenye alikuwaka na “uchungu mwingi sana” juu hakukuwaka na mutoto na mbanda yake alikuwaka namuchokoza sana.—1 Samweli 1:6, 10.

  • Biblia inazungumuzia mwanaume mwenye kuitwa Yobu, mwenye hali yake inaweza kufanana na yetu. Hata kama alikuwa mwanaume wa imani, aliteseka juu alikuwa na huzuni sana, na siku moya alisema hivi: “Ninachukia maisha yangu; sitaki kuendelea kuishi.”—Yobu 7:16.

Kujifunza namna wale watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia waliweza kupiganisha ile mawazo yao yenye kuhangaisha, kunaweza kutusaidia na siye tupiganishe mahangaiko yetu.

Namna Biblia Iko Nasaidia Kevin

Namna Tatizo Yangu ya Akili Inanihangaishaka

Kevin iko nakunywa café na marafiki wake wawili.

“Wakati nilikuwa karibu kueneza miaka makumi tano, wanganga waliniambia kama niko na ugonjwa wa akili wenye unafanyaka namna niko najisikia ikuwe inabadilika-badilika. Wakati fulani najisikiaka kuwa naweza kumaliza tatizo yoyote yenye inaweza kunifikia mu maisha. Lakini wakati ingine ninaonaka kama ni muzuri tu nikufe kuliko kuishi.”

Namna Biblia Inanisaidiaka

“Mutu moya mwenye kuzungumuziwa mu Biblia mwenye hali yangu inafanana na yake ni mutume Petro. Alifanyaka makosa yenye ilifanya ajione kuwa wa bure. Lakini kuliko kuendelea kujiona vile, alitafuta marafiki wenye walimuhangaikia. Wakati ninajisikia mubaya juu ya magonjwa yangu, makosa yangu inanihangaishaka sana na inanifanyaka nijione kuwa wa bure. Sawa Petro, ninajikazaka kuwa karibu na marafiki wenye wako tayari kunisaidia niendelee mbele.

“Mutu mwingine mwenye kuzungumuziwa mu Biblia mwenye mufano wake unakuwaka unanifariji sana ni Mufalme Daudi. Mara mingi alikuwa mwenye kushuka moyo juu ya hali yake na alihuzunika juu ya makosa yenye alifanyaka zamani. Hali yangu inaweza kufanana na yake juu wakati fulani nahuzunikaka juu ya mambo yenye nilisema ao kufanya. Maneno ya Daudi yenye iko mu Zaburi ya 51 inakuwaka nanifariji sana. Mu mustari wa 3, Daudi alisema hivi: ‘Ninajua muzuri makosa yangu, na zambi yangu iko mbele yangu sikuzote.’ Vile kabisa njo najisikiaka wakati tatizo yangu ya akili inanihangaisha, juu mu ile hali nashindwaka kukuwa na mawazo yenye kufaa juu yangu. Lakini pia najisikiaka vile Daudi alijisikiaka wakati alisema hivi mu mustari wa 10: ‘Umba moyo safi ndani yangu, Ee Mungu, na utie ndani yangu roho mupya, yenye kuwa imara.’ Na miye nakuwaka namulilia Yehova vile juu anisaidie nikuwe na mawazo yenye kufaa juu yangu. Na tena, mustari wa 17 unakuwaka nanifariji sana. Inasema: ‘Moyo wenye kuvunjika na kupondwa, Ee Mungu, hautaukataa.’ Ile andiko inanihakikishiaka kama Mungu ananipenda.

“Kufikiria sana mifano ya mu Biblia na mambo yenye Mungu amenifanyia kunanisaidia nitumainie kama mambo itakuwa muzuri mu siku zenye kuya. Ninaona kama ahadi zenye kuwa mu Biblia ni za kweli kabisa na ile inanisaidia niendelee mbele.”

Juu ya Kupata Musaada Ingine:

Soma ku jw.org habari “Kuishi na Ugonjwa wa Kihisia,” mu gazeti Amuka! ya tarehe 8, Mwezi wa 1, 2004.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine