Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 1/15 uku. 16
  • Habari Fulani za Ulimwengu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Habari Fulani za Ulimwengu
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ULIMWENGU
  • Uingereza
  • Australia
  • Namna Gani Naweza Kupata Dini ya Kweli?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Dini Zimeanza Kukosa Watu?
    Amuka!—2015
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Mwisho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!
    Misho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2015
g 1/15 uku. 16
Paa ya kanisa

HABARI FULANI ZA ULIMWENGU

Matendo Fulani ya Dini

Dini inatazamiwa kuwa nguvu ya kuunganisha watu. Lakini mara nyingi, inaletea watu ugomvi na kukosa kuaminiana.

ULIMWENGU

Muchoro wa dunia, sehemu tatu juu ya ine zinaonyeshwa

Wakaaji wa dunia zaidi ya 75 juu ya 100 wanaishi katika inchi zenye kuwa na vizuizi vikubwa juu ya dini fulani, iwe ni kwa sababu ya sheria za serikali ao uadui katika jamii. Katika miaka tano iliyopita, hesabu ya inchi ambamo dini ndogo-ndogo zilitendewa vibaya iliongezeka mara mbili.

JAMBO LA KUFIKIRIA: Ni sababu gani tofauti-tofauti zinazofanya watu fulani wachukie dini?—Mathayo 23:27, 28; Yohana 15:19.

Uingereza

Tony Blair, Waziri Mukubwa wa zamani, anaandika katika gazeti moja (Observer) kama “kutumia dini vibaya” ndiyo sababu kubwa iliyotokeza matendo ya ugaidi (terrorisme) hivi karibuni. Anaongeza hivi: “Vita vya hii miaka 100 inawezekana havitokane na mawazo makali ya kisiasa, kama vita vilivyotokea kati ya mwaka wa 1901 na 2000, lakini inawezekana sana kuwa vita hivyo vimepiganwa kwa sababu ya mambo yanayohusu tofauti ya kidesturi na ya kidini.”

JAMBO LA KUFIKIRIA: Sababu gani dini ndiyo inatokeza mara nyingi mugawanyiko?—Marko 7:6-8.

Australia

Mutu mumoja aliyefutwa na watu wengine ine wanaopandisha mikono yao juu

Shirika la Uchunguzi wa Hesabu (Statistiques) la Australia linaripoti kuwa Muaustralia 1 juu ya 5 anasema kuwa hana dini yoyote. Ripoti hiyo inasema hata kama “kuwa tu katika dini fulani haiko sawa na kushiriki kwa bidii katika mambo mbalimbali ya kidini.” Wanaume 15 tu juu ya 100 na wanawake 22 tu juu ya 100 walio na dini fulani ndio wanakubali kuwa wanashiriki kwa bidii katika kikundi cha kidini ao cha kiroho.

JAMBO LA KUFIKIRIA: Ni matendo gani mabaya yanayoonekana waziwazi katika dini nyingi za leo?—Mathayo 7:15-20.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine