Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 2 uku. 3
  • Watu Wanapendezwa na Mambo ya Mashetani!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watu Wanapendezwa na Mambo ya Mashetani!
  • Amuka!—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utangulizi
    Amuka!—2017
  • Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2017
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuzungumuza na Mashetani?
    Amuka!—2017
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2017
g17 na. 2 uku. 3
Kijana mumoja anashangaa kwa sababu ya mambo yenye anaona kwenye chombo chake cha kielektroni

HABARI KUBWA | HATARI YA KUJIFURAHISHA NA MAMBO YA MASHETANI

Watu Wanapendezwa na Mambo ya Mashetani!

“Ondoka, wanyonya-damu, watu-mbweha na maiti yenye kutembea—kusumbuliwa na mashetani na mambo ya kuondoa pepo yanatendeka pale.”—The Wall Street Journal.

VITABU, filme, na michezo ya video vinaonyesha watu kama vile vijana na wakubwa wenye kuwa wachawi, wafumu wenye kuvutia, na watu-mbweha wenye sura ya kuvutia. Sababu gani watu wanapendezwa na mambo hayo?

Claude Fischer, profesa wa sosholojia anaandika hivi: “Katika miaka ya hivi karibuni, hesabu ya watu wenye kuamini mizimu imeongezeka, ni kusema, kutoka mutu mumoja kati ya Waamerika kumi mupaka kufikia mutu mumoja kati ya Waamerika tatu. Hesabu ya vijana Waamerika wenye wanasema kama wameenda kwa wachawi, wanaamini mizimu, na wenye wanaamini pia kwamba kuna nyumba za mashetani, inapita karibu mara mbili hesabu ya watu wakubwa wenye wamesema hivyo.”

Haiko jambo la kushangaza kwamba, habari za watu wenye kuwa na pepo zinaogopesha tena. Katika gazeti The Wall Street Journal, Michael Calia anaandika hivi: “Kujulikana tena kwa watu wenye kusumbuliwa na mashetani katika desturi nyingi kunatokana na kuonyeshwa sana, katika miaka kumi yenye imepita, kwa wanyonya-damu, watu-mbweha na maiti yenye kutembea.”

Ripoti moja inaonyesha kwamba “kati ya 25% na 50% ya watu katika dunia yote wanaamini mizimu, na habari juu ya mizimu inazungumuziwa sana katika vitabu vya desturi nyingi.” Na uchunguzi moja wenye ulifanywa na Christopher Bader na Carson Mencken, maprofesa wa sosholojia katika inchi ya États-Unis, “ulionyesha kwamba kati ya 70% na 80% ya Waamerika wanaamini sana hata aina moja ya mambo ya mashetani.”

Kuna hatari gani kama mutu anajifurahisha na mambo ya mashetani?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine