Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 5 uku. 3-7
  • Wakati Musiba Unatokea—Hatua Zenye Zinaweza Kuokoa Uzima

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Musiba Unatokea—Hatua Zenye Zinaweza Kuokoa Uzima
  • Amuka!—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MBELE YA MUSIBA​—UJITAYARISHE!
  • WAKATI WA MUSIBA​—UTENDE HARAKA
  • KISHA MUSIBA​—UKUWE MUANGALIFU!
  • Je, Unajitayarisha kwa Ajili ya Misiba?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Uko Tayari?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Ukuwe Tayari mu hii Sehemu ya Mwisho ya “Siku za Mwisho”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Kukabiliana na Misiba ya Asili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2017
g17 na. 5 uku. 3-7
Wazima-moto wanajikaza kuzima moto

HABARI KUBWA

Wakati Musiba Unatokea Hatua Zenye Zinaweza Kuokoa Uzima

“Mulipuko mukubwa wenye ulitokea karibu, ulinitupa chini. Moshi ulitokea katika matundu ya kuingizia hewa, na biro yetu yenye kuwa juu ilianza kuwaka moto.”​—Joshua.

Tetemeko la dunia . . . upepo mukubwa . . . shambulizi la wateroriste . . . kupiga watu masasi kwenye masomo. Mara nyingi, maneno hayo yanatajwa katika vichwa vya habari mbalimbali. Kwa kweli, ni mwepesi kusoma habari kuhusu musiba, lakini kupatwa na musiba ni jambo lingine. Unaweza kufanya nini mbele ya musiba, wakati wa musiba, na kisha musiba kutokea ili kuwa na uwezekano mukubwa wa kuokoka?

MBELE YA MUSIBA​—UJITAYARISHE!

MUSIBA unaweza kupata kila mutu. Kujitayarisha ni jambo la maana sana ili kuokoka. Lakini, kujitayarisha kunatia ndani nini?

  • Ujitayarishe kiakili. Utambue kwamba misiba inatokea kila mara na kwamba wewe na watu wenye unapenda munaweza kupatwa na musiba. Haifae kujitayarisha kisha musiba kutokea.

  • Ujifunze kuhusu misiba yenye inaweza kutokea katika eneo lenu. Ujue ni wapi unaweza kukimbilia ili kujilinda. Uchunguze kama nyumba yako na kwenye inapatikana ni salama kabisa. Ondoa vitu vyenye vinaweza kutokeza moto. Utie vifaa vyenye kutambua moshi, na ubadilishe betri ya vifaa hivyo mara moja ao zaidi katika mwaka.

  • Utayarishe vitu vya lazima. Umeme, maji, telefone, na kazi za kusafirisha watu vinaweza kukosekana. Kama uko na motokari, ujikaze kuwa na mafuta (carburant) ya kutosha, na sikuzote ukuwe na chakula, maji, na vitu vya musaada wa kwanza katika nyumba yako.​—Ona kisanduku “Uko na Kila Kitu Chenye Unahitaji?”

    Familia moja inatayarisha vifaa kwa ajili ya musaada wa kwanza

    Kujitayarisha ni jambo la maana sana ili kuokoka

  • Ukuwe na namba za telefone za marafiki wa karibu na wa mbali.

  • Upange na ufanye mazoezi kuhusu namna ya kujiokoa. Ujue nafasi za karibu za kutoka katika nyumba yako, na mipango ya usalama ya masomo ya watoto wako. Mupange nafasi za kukutania​—kama vile kwenye masomo ao maktaba​—nafasi moja yenye kuwa karibu, na ingine yenye kuwa inje na ujirani wenu. Watu wenye mamlaka wanashauria kuwa na tabia ya kutembelea nafasi hizo za kukutania mukiwa familia.

  • Upange kusaidia wengine, kutia ndani watu wenye kuzeeka na walemavu.

WAKATI WA MUSIBA​—UTENDE HARAKA

Joshua mwenye tulitaja kwenye mwanzo wa habari hii anasema hivi: “Wakati moto ulitokea, watu wengi hawakushituka, hawakutenda haraka. Wamoja walifunga ordinatere ao kujaza chupa za maji. Mwanaume mumoja alisema, ‘Pengine tunapaswa kungoja kidogo.’” Hata kama wengine walisitasita, Joshua alisema kwa sauti kubwa: “Tunapaswa kutoka hapa sasa!” Kisha kusikia hivyo, wafanyakazi wenzake waliacha kubisha na wakashuka chini wakimufuata. Joshua aliendelea kusema kwa sauti kubwa, “Kama mutu anaanguka, mumusimamishe, na muendelee mbele. Sisi wote tutaokoka!”

  • Katika moto. Ulale chini na utambae haraka mupaka kwenye nafasi ya kutokea yenye kuwa karibu sana. Moshi inafanya ikuwe nguvu kuona, na watu wengi wenye wanakufa na moto, wanakufa kwa sababu ya kuvuta moshi. Uache vitu vyako. Mutu anaweza kupoteza uzima wake kwa muda mufupi tu.

  • Katika tetemeko la dunia. Ujifiche chini ya kitu chenye hakiwezi kuvunjika ao kwenye kona ya ukuta wa ndani. Ujue kwamba matetemeko mengine madogo-madogo yanaweza kufuata, na uende haraka inje, mbali na majengo. Waokoaji wenye kuwa na mazoezi wanaweza kukawia, kwa hiyo, jaribu kuokoa watu wengine kama unaweza.

  • Katika tsunami. Kama maji inavuka mara moja mipaka yake, uende haraka kwenye eneo lenye kuinuka. Ujue kwamba mawimbi mengi na makubwa yanaweza kutokea.

  • Katika kimbunga ao upepo mukubwa. Uende mahali pa kujilinda na upepo mukubwa.

  • Katika mafuriko. Ukuwe inje ya majengo yenye kupatwa na mafuriko. Epuka kutembea ao kutembeza motokari katika maji. Maji ya mafuriko yanaweza kuchangana na maji machafu na kuwa na hatari, kama vile takataka, mashimo, na singa za umeme zenye zimeanguka.

  • Ulijua? Maji yenye kuteremuka ya sentimetre 60 yanaweza kubeba gari. Watu wengi wenye wanakufa katika mafuriko, wanakufa wakati wanajaribu kutembeza katika maji yenye kuteremuka.

  • Kama wenye mamlaka wanaomba watu waondoke, ondoka haraka! Uambie marafiki wako kwenye uko, kwa kuwa wanaweza kutia maisha yao katika hatari kwa sababu ya kukutafuta.

    Familia moja inasikiliza radio

    Kama wenye mamlaka wanaomba watu waondoke, ondoka haraka!

  • Ulijua? Inaweza kuwa muzuri zaidi kuandika ujumbe kuliko kuita kwenye telefone.

  • Kama watu wenye mamlaka wanasema watu wabakie katika nyumba zao ao mahali pa kukimbilia, kubali. Kama aksidenti ao shambulizi la kikemia, kibiolojia, ao la kinyuklia linatokea inje, uzime vifaa vya kuleta hewa ndani ya nyumba, na ufunge milango na madirisha. Wakati wa tukio la kinyuklia, uende kwenye sehemu ya chini zaidi ya nyumba yenu ili kupunguza hatari ya kupumua hewa yenye kuwa na sumu. Usikilize habari za televizyo ao radio ya eneo lenu. Ubakie ndani ya nyumba mupaka watu wenye mamlaka watangaze kwamba hatari imepita.

KISHA MUSIBA​—UKUWE MUANGALIFU!

Ili kuepuka magonjwa na hatari, ufikirie mashauri yenye kufuata:

  • Ubaki na marafiki, kama inawezekana, kuliko kubaki katika kambi.

  • Uhakikishe kwamba kuna usafi mahali penye unaishi.

  • Tumia kifaa cha kujilinda wakati unaondoa vitu vyenye kuharibika. Kama inawezekana, uvae glavu (gants), viato vyenye kuwa nguvu, kofia yenye kuwa nguvu, na kifaa cha kukulinda na vumbi. Ukuwe muangalifu na singa za umeme na moto wenye kufichama.

  • Rudilia maisha yako ya kawaida kama inawezekana. Watoto wako na lazima ya kuona kwamba unatulia na uko na tumaini. Ufanye kazi za masomo, mucheze, na muabudu mukiwa familia. Musikazie habari zenye kuzungumuzia mambo ya misiba, na usimwangie mahangaiko yako ao kuvunjika moyo kwako juu ya watu wa familia. Ukubali musaada, na usaidie wengine.

    Familia moja inarudilia maisha yake ya kawaida kisha musiba

    Kisha musiba, rudilia maisha yako ya kawaida kama inawezekana

  • Utambue kwamba musiba unafanya mutu apoteze vitu vingi. Serikali na shirika zingine za kutoa musaada zinajikaza kusaidia watu waokoke, hapana kurudisha kila kitu chenye kilipotea. Ili kuokoka, tuko na lazima ya maji safi, chakula, nguo, na mahali pa kuishi.​—1 Timotheo 6:7, 8.

  • Utambue kwamba unaweza kuumia moyoni na utafute musaada. Hilo linatokea mara nyingi kisha kuteseka kwa mara ya kwanza. Alama hizo zinatia ndani mahangaiko, kushuka moyo, na kubadilika-badilika kwa hisia, na pia magumu ya kufikiri, ya kufanya kazi, na ya kulala. Uzungumuze na marafiki wenye kukuhangaikia.

Hata kama Joshua aliokoka wakati moto ulitokea katika eneo lake la kazi, wengi kati ya watu wenye alijua hawakuokoka. Alipata musaada wa wazee Wakristo na musaada wa washauri wa afya ya akili. Joshua anasema hivi: “Walinihakikishia kwamba huzuni yangu ilikuwa kawaida na ingepita. Kisha miezi sita, ndoto za mubaya zilianza kupunguka. Alama zingine zimefanya siku nyingi.”

Misiba inapotosha mawazo yetu kuhusu haki. Watu fulani wanamulaumu Mungu kimakosa. Kama vile Joshua, watu wengi wanajilaumu kwa sababu waliokoka lakini wengine walikufa. Anasema hivi: “Naendelea kujiuliza kama singeweza kuokoa watu wengi zaidi. Nafarijiwa na imani yangu kwamba karibuni Mungu ataleta haki kamilifu na atatosha mambo yote ya mubaya. Kwa kungojea wakati huo, nafurahia maisha kila siku na kufanya yangu yote ili kuendelea kuwa na furaha hiyo.”​—Ufunuo 21:4, 5.a

a Ili kupata habari zaidi kuhusu ahadi za Mungu kwa ajili ya wakati unaokuja, na sababu gani anaruhusu mateso, ona kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Unaweza kukichukua kwenye www.jw.org.

UKO NA KILA KITU CHENYE UNAHITAJI?

Vifaa kwa ajili ya musaada wa kwanza

Mashirika yenye kuangalia mambo ya misiba yanashauri familia kuweka akiba ya vitu kwa ajili ya musiba na kuangalia kila mwaka kama vingali vyenye kufaa. Bila shaka, mambo yenye unahitaji ni tofauti kulingana na hali na mahali penye unaishi, kwa hiyo, uzungumuze na mashirika yenye kuangalia mambo ya misiba ili kupata mashauri yenye kufaa kwa ajili ya eneo lenu.

Kwa ujumla, inashauriwa kuweka litre 11 hivi ya maji kwa kila mutu na chakula chenye kuwa tayari kukuliwa ambacho hakiwezi kuharibika katika siku tatu.

Pia, familia fulani ziko na sakoshe yenye kuwa na vitu kama vile:b

  • Blangeti, nguo za kuleta joto, na viatu vyenye kuwa nguvu

  • Torche, radio (ya betri ao ya manivelle), na betri za ziada

  • Vyombo vya musaada wa kwanza na filimbi ya kupiga ili kuomba musaada

  • Vyombo vya kulia chakula, chombo cha kufungua vitu mbalimbali, kisanduku kidogo chenye kuwa na vyombo mbalimbali, na viberiti vyenye haviwezi kuharibika na maji

  • Vifaa vya kujilinda na vumbi, utepe wa kushika kitu wenye hauwezi kuharibika na maji, na hema kwa ajili ya nafasi ya kukaa ao kulala

  • Muswaki (brosse à dents), sabuni, vitambaa vya kupanguzia, na karatasi ya choo

  • Vifaa kwa ajili ya kutunza watoto na vifaa vya pekee kwa ajili ya wazee na walemavu

  • Kuwa na dawa, kopi za mapendekezo ya matunzo, na karatasi zingine za lazima katika kitu chenye hakiwezi kuharibika na maji

  • Namba za telefone za kuita wakati uko na lazima ya musaada wa haraka, na mahali pa kukutana, na pia karte ya eneo

  • Karte za benki na feza

  • Funguo za ziada za nyumba na funguo za motokari

  • Karatasi, kalamu ya risasi (crayon), vitabu, na michezo kwa ajili ya watoto

  • Biblia

b Pengine vifaa fulani vyenye kuwa hapa havipatane na hali yako ao eneo lenu. Unaweza pia kuongeza vifaa vyenye havitajwe hapa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine