MAISHA YA MUKRISTO
Uko Tayari?
Kama kunatokea musiba wa asili mu eneo lenu, uko tayari? Pengine matetemeko ya inchi, upepo mukubwa, moto wa misitu, na maji ya mingi yenye kubeba nyumba na vitu inaweza kutokea bila kutazamia na kuharibu kabisa. Zaidi ya ile, muvurugo, magonjwa yenye kuenea haraka, na mashambulizi ya wateroriste vinaweza kutokea nafasi yoyote na bila kutazamia. (Muh 9:11) Tusiwaze kama ile misiba haiwezi kutokea hata kidogo fasi kwenye tunaishi.
Kila mutu anapaswa kukamata hatua fulani ili kuwa tayari kama musiba unatokea. (Mez 22:3) Hata kama tengenezo la Yehova linafanyaka mambo fulani ili kusaidia wakati misiba inatokea, kila mutu anapaswa kujitayarisha.—Gal 6:5, maelezo ya chini.
MUANGALIE VIDEO UKO TAYARI KWA AJILI YA MUSIBA WA ASILI? NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Namna gani tunaweza kujitayarisha kiroho mbele musiba utokee?
Juu ya nini ni jambo la lazima . . .
• kuendelea kupashana habari na wazee mbele musiba utokee, wakati wa musiba, na kisha musiba?
• kutayarisha vitu vya musaada wa kwanza?—g17.5 6
• kuzungumuzia aina fulani ya misiba yenye inaweza kutokea na namna ya kufanya?
Ni mu njia gani tatu tunaweza kusaidia wale wenye wanafikiwa na musiba wa asili?