Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g19 na. 2 uku. 10-11
  • Namna ya Kuwa Mwenye Kutumainika

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kuwa Mwenye Kutumainika
  • Amuka!—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUWA MWENYE KUTUMAINIKA KUNATIA NDANI NINI?
  • JUU YA NINI NI JAMBO LA MAANA KUWA MWENYE KUTUMAINIKA ?
  • UWAFUNDISHE NAMNA YA KUWA WENYE KUTUMAINIKA
  • Faida ya Kazi za Nyumbani
    Amuka!—2017
  • 8 Onyesha Mufano
    Amuka!—2018
  • Namna ya Kusaidia Watoto Wakati Wanashindwa Kufanya Jambo Fulani
    Musaada kwa Familia
  • Namna ya Kumufundisha Mutoto Wako
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2019
g19 na. 2 uku. 10-11
Baba mumoja anasaidia mutoto wake kumwangia mumea maji

SOMO LA 4

Namna ya Kuwa Mwenye Kutumainika

KUWA MWENYE KUTUMAINIKA KUNATIA NDANI NINI?

Watu wenye kutumainika ni wenye kutegemeka. Wanafanya kazi zenye walipewa na wanamaliza kuzifanya bila kuchelewa.

Mutoto anaweza kuanza kujifunza kuwa mutu mwenye kutumainika hata wakati angali mudogo sana. Kitabu Parenting Without Borders kinasema hivi: “Wakati watoto wako na miezi 15 wanaweza kufanya kile muzazi anawaambia wafanye, na wakati wanakuwa na miezi 18 hivi wanapenda kufanya chochote chenye wazazi wao wako wanafanya. Katika maeneo mingi, wakati watoto wako kati ya miaka 5 na 7, wazazi wanaweza kuwaonyesha namna wanaweza kusaidia kufanya kazi za mu nyumba. Hata kama ni wadogo, watoto wanaweza kufanya kazi mingi muzuri.”

JUU YA NINI NI JAMBO LA MAANA KUWA MWENYE KUTUMAINIKA ?

Katika maeneo fulani, vijana wengi wenye kukomaa wanajaribu kuishi peke yao lakini wanashindwa kufanya vile na kisha wanarudia kuishi pamoja na wazazi wao. Wakati fulani, ile inatokea juu wazazi wao hawakuwafundisha hata kidogo namna ya kutumia muzuri feza zao, namna ya kutunza nyumba, na namna ya kuwa mutu mwenye kutumainika mu maisha yao ya kila siku.

Kwa hiyo, ni muzuri kufundisha watoto wako namna ya kuwa mwenye kutumainika leo ili wajue kile watafanya wakati watakuwa wakubwa. Kitabu How to Raise an Adult kinasema hivi: “Usiache watoto wako waendelee kukutegemea mupaka wafikie miaka 18 njo sasa uwaache waanze kujitegemea.”

UWAFUNDISHE NAMNA YA KUWA WENYE KUTUMAINIKA

Uwapatie kazi za kufanya ku nyumba.

KANUNI YA BIBLIA: “Kila namna ya kazi ya nguvu iko na faida.”​—Mezali 14:23.

Sikuzote watoto wadogo wanapenda kusaidia kufanya kazi yoyote yenye wazazi wao wako wanafanya. Unaweza kutumia ile tamaa yenye ni ya kawaida kwa watoto ili kuwapatia kazi za kufanya ku nyumba.

Wazazi fulani wanajizuia kufanya vile. Wanawaza kama, kwa sababu watoto wangali wanaenda ku masomo, wako na kazi mingi zenye wanapewa kule, na kwa hiyo, hawapendi kuwaongezea muzigo.

Lakini, watoto wenye wanafanya kazi za ku nyumba, wanaweza kuweza masomo juu kazi zenye wanapewa ku nyumba zinawafundisha kukubali kazi zenye wanapewa ku masomo na kuzimaliza. Zaidi ya ile, kitabu Parenting Without Borders, kinasema hivi: “Ikiwa hatuache watoto wetu watusaidie wakati wako wadogo na wakati wanapenda kufanya vile, wataanza kuwaza kama kusaidia wengine haiko jambo la maana. . . . Wataanza pia kuwaza kama wengine njo wanapaswa kuwatumikia.”

Kama vile ile maneno inaonyesha, kufanya kazi za ku nyumba kunazoeza watoto wakuwe wanachangia kuliko kutumia tu, wakuwe wanatoa kuliko kupokea tu. Kufanya kazi ku nyumba kunafanya watoto watambue kama wako na sehemu ya maana mu familia na waelewe kama kusaidia ku kazi ni jambo lenye wanapaswa kufanya.

Saidia watoto wako wakubali matokeo ya makosa yao.

KANUNI YA BIBLIA: “Sikiliza shauri na ukubali nizamu, ili ukuwe na hekima katika wakati wako wenye kuja.” ​—Mezali 19:20.

Wakati watoto wako wanafanya makosa​—kwa mufano, kama mutoto wako mwanaume ao mwanamuke anaharibisha kitu cha mutu mwingine bila kujua​—usifiche ile jambo. Watoto wanaweza kukubali matokeo; mu ile hali, watafanya vile kwa kuomba musamaha ao kwa kulipa kitu chenye waliharibisha.

Kama watoto wanaelewa kama makosa yenye wanafanya iko na matokeo, watajifunza

  • kuwa waaminifu na kukubali makosa yao

  • kuepuka kutupia wengine makosa yao

  • kuepuka kujitetea

  • kuomba musamaha, wakati inafaa

Baba mumoja anasaidia mutoto wake kumwangia mumea maji

UMUZOEZE KUANZIA LEO

Watoto wenye wanafundishwa kuwa wenye kutumainika wataweza kuongoza muzuri zaidi maisha yao wakati watakuwa wakubwa

Ufundishe Kupitia Mufano

  • Niko mufanyakazi mwenye bidii, mutu mwenye kupanga mambo muzuri, na ninaheshimia wakati?

  • Watoto wangu wananiona vile niko ninafanya kazi za ku nyumba?

  • Ninakubali makosa yangu, na ninaomba hata musamaha wakati inafaa?

Mambo Yenye Tulifanya . . .

“Wakati wa kupiga chakula, watoto wangu walinisaidia tangu wakati walikuwa wadogo sana. Wakati nilikuwa ninapanga nguo zenye kuwa safi, wao pia walipanga nguo fulani. Wakati nilikuwa ninasafisha, wao pia walisafisha. Waliona kufanya kazi kuwa jambo lenye kufurahisha. Walifurahia kuwa tu pamoja na mimi na kufanya kile nilikuwa ninafanya. Ni vile walijifunza kukamata mambo kwa uzito.” ​—Laura.

“Siku moja, nilimuambia mutoto wetu mudogo mwanaume aite rafiki wa familia yetu na amuombe musamaha kwa kumukosea adabu. Kwa miaka mingi alipaswa kuomba musamaha mara mingi kwa sababu ya kusema mambo ya kweli lakini yenye haiko muzuri kusema; sasa amejifunza kuomba musamaha yeye mwenyewe wakati anafanya kosa.”​—Debra.

FAIDA ZA KUKUBALI MATOKEO

Mwalimu Jessica Lahey anaandika hivi mu gazeti Atlantic: “Watoto wanafanyaka makosa, na wakati wanafanya makosa, ni jambo la maana wazazi wakumbuke kama watoto wanaweza kujifunza mambo ya maana kupitia makosa yao. Kila mwaka nilikuwa na wanafunzi wenye walifanya makosa na wenye wazazi wao hawakuwaepusha na matokeo ya makosa yao. Lakini waliwasaidia warekebishe makosa yao. Wale wanafunzi walikuwa wenye furaha zaidi na waliweza kufanya mambo muzuri zaidi.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine