Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 3 uku. 4-5
  • Tafuta Ukweli wa Mambo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tafuta Ukweli wa Mambo
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tatizo
  • Kanuni ya Biblia
  • Faida ya Kujua Ukweli wa Mambo
  • Mambo Yenye Unaweza Kufanya
  • Umeambukizwa na Tabia ya Ubaguzi?
    Amuka!—2020
  • Chuki Ni Tatizo Linaloenea Katika Dunia Yote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Dunia Isiyokuwa na Chuki Itakuwa Wakati Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Onyesha Upendo
    Amuka!—2020
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 3 uku. 4-5
Wanaume wawili wako wanauliza maulizo mwanamuke mumoja mbele wamupatie kazi ku izine ya kutengeneza gari. Anaonekana iko na wasiwasi.

Tafuta Ukweli Wa Mambo

Tatizo

Mara mingi watu wanakuwaka na ubaguzi juu hawana habari za kweli. Tufikirie mifano yenye kufuata:

  • Wakubwa fulani wa kazi wako na mawazo yenye haiko ya kweli kuhusu wanamuke. Wanawaza kama wanamuke hawawezi kufanya kazi yenye kuomba nguvu mingi ao akili mingi.

  • Katika Ulaya ya enzi za kati (ni kusema, kipindi cha kuanzia mwaka wa 476 K.K.Y. mupaka mwaka 1500 hivi K.K.Y.) Wayahudi walisemewa uongo na kushitakiwa kama walikuwa wanatia sumu ndani ya visima na kama walieneza magonjwa. Wayahudi walisemewa tena uongo wakati wa utawala wa Wanazi. Ile wakati walishitakiwa kama ni wao njo walikuwa wanafanya inchi ya Ujerumani ikuwe na matatizo ya feza. Ile mashitaka ilifanya Wayahudi wabaguliwe sana na mpaka leo ile ubaguzi ingali inaonekana kwa kiasi fulani.

  • Watu wengi wanakosea kwa kufikiri kama watu wote wenye kuwa na ulemavu fulani hawakuwake na furaha, ao wanakuwaka tu na huzuni.

Watu wenye wanaamini mambo ya kuwazia, kama vile mambo yenye tumetoka kuzungumuzia, wanaweza kutaja mifano fulani ao mambo yenye kuonekana kuwa ya kweli ili kuunga mukono mawazo yao. Na mutu yeyote mwenye anapinga mawazo yao, wanasema kama ule mutu hajue kitu.

Kanuni ya Biblia

“Mutu mwenye hana ujuzi haiko mutu muzuri.”​—MEZALI 19:2.

Ile inamaanisha nini? Ile inamaanisha kama ikiwa hatujue ukweli wa mambo, tutakamata maamuzi ya mubaya. Ikiwa tunaamini mambo ya kuwaziawazia kuliko kuamini mambo ya kweli, tutahukumu watu mubaya.

Biblia Inafundisha Watu Wakuwe na Ubaguzi?

Watu fulani wanasema kama Biblia inachochea watu wakuwe na ubaguzi. Lakini Biblia inasema nini?

  • Watu wote wanatoka kwa mutu mumoja: ‘Kutoka kwa mutu mumoja, Mungu alifanya kila taifa la watu.’​—Matendo 17:26.

  • Mungu hana ubaguzi: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.”​—Matendo 10:34, 35.

  • Mungu anakazia uangalifu zaidi namna tunaonekana kwa ndani, hapana namna tunaonekana kwa inje: “Mwanadamu bure anaona kile chenye kinaonekana kwa macho, lakini Yehova anaona ndani ya moyo.”​—1 Samweli 16:7.a

a Yehova ni jina la Mungu kama vile inaonyeshwa mu Biblia.

Faida ya Kujua Ukweli wa Mambo

Kama tuko na habari za kweli juu ya watu, hatutaamini mambo ya uongo yenye watu wanasema juu yao. Na wakati tunafikia kujua kwamba hawakutuambia kweli juu ya kikundi fulani cha watu, itakuwa nguvu tuamini mbiombio mambo yenye watu wanatuambia juu ya watu wengine.

Mufano wa Kweli: Jovica (wa Inchi ya Balkani)

Jovica, mwenye tulishazungumuzia, alikomalia fasi kwenye watu wa inchi yao, habari, na programu za tevizyo zilikuwa zinazungumuzia ripoti za mubaya kuhusu kikundi kidogo cha watu. Anasema hivi: “Nilifikia kubagua wale watu na hata kuwachukia. Niliwaza kabisa kama niko na sheria ya kujisikia vile.

“Lakini wakati nilikuwa katika jeshi nililazimika kuishi na kutumika pamoja na wanajeshi wenzangu kutoka katika kile kikundi kidogo cha watu. Kisha wakati fulani, nilijua mambo mingi juu yao. Nilianza hata kujifunza luga yao na kusikiliza nyimbo zao za asili. Nilianza kufurahia kupitisha wakati pamoja nao, na mawazo yangu juu yao ilianza kubadilika. Lakini, inawezekana nikuwe tena na ubaguzi. Kwa hiyo, niliepuka kusikiliza habari zenye zinasema mubaya watu wa kile kikundi. Pia, siangaliake filme ao teatre zenye zinapendwa na watu wengi zenye zinatumia maneno ya kuwazarau. Najua kama ubaguzi unaweza kufanya tukasirikie na kuchukia wale wenye tunabagua.”

Mambo Yenye Unaweza Kufanya

  • Tukumbuke kuwa wakati watu wanasema kama watu wa kikundi fulani wako na tabia ya mubaya, ile haimaanishe kama watu wote wa kile kikundi wako na ile tabia.

  • Tukumbuke kama inawezekana hatujue mambo mingi kuhusu kikundi fulani cha watu.

  • Tafuta habari za kweli fasi yenye inastahili.

Hawachukianake tena

Picha: 1. Wanaume wawili wako wanatembea na kuzungumuza pamoja.

Ni nini ilisaidia Waarabu na Wayahudi waachane na ubaguzi?

Angalia video Ni Wakati Gani Upendo Mushikamanifu Utamaliza Chuki? Tafuta ile video ku jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine