Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 11 uku. 22-23
  • Mambo Watu Wanaamini na Desturi Zisizomupendeza Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Watu Wanaamini na Desturi Zisizomupendeza Mungu
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Chagua Kumuabudu Mungu mu Njia Yenye Anapenda
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Pasaka?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Je, Sikukuu Zote Zinamufurahisha Mungu?
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Sikukuu Zinazomuchukiza Mungu
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
Ona Habari Zaidi
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 11 uku. 22-23

Somo 11

Mambo Watu Wanaamini na Desturi Zisizomupendeza Mungu

Ni aina gani ya mambo watu wanaamini na desturi zilizo mbaya? (1)

Je! Wakristo wanapaswa kuamini kwamba Mungu ni Utatu? (2)

Kwa nini Wakristo wa kweli hawasherehekei Krismasi (Noeli), Ista (Pasaka), au siku za kuzaliwa? (3, 4)

Je! wafu wanaweza kuzuru wale wanaoishi? (5)

Je! Yesu alikufa juu ya musalaba? (6)

Kumupendeza Mungu ni kwa maana kadiri gani? (7)

1. Mambo yote ambayo watu wanaamini au desturi zote si mbaya. Mungu hazikubali ikiwa zinatokana na dini isiyo ya kweli au ikiwa zinapingana na mafundisho ya Biblia.​—⁠Matayo 15:⁠6.

2. Utatu: Je! Yehova ni Utatu​—⁠watu watatu katika Mungu moja? Hapana! Yehova, yeye Baba, ni “Mungu pekee wa kweli.” (Yoane 17:3; Marko 12:29) Yesu ni Mwana Wake muzaliwa wa kwanza, naye anajitia chini ya Mungu. (1 Wakorinto 11:⁠3) Baba ni mukubwa kupita yule Mwana. (Yoane 14:28) Ile roho takatifu si mutu; ni kani (nguvu) ya utendaji ya Mungu.​—⁠Mwanzo 1:2; Matendo 2:⁠18.

3. Krismasi na Ista: Yesu hakuzaliwa kwenye Desemba 25. Yeye alizaliwa karibu na Oktoba 1, kipindi cha mwaka katika hicho wachungaji wanalinda makundi yao inje wakati wa usiku. (Luka 2:​8-12) Yesu hakuwaamuru kamwe Wakristo kusherehekea kuzaliwa kwake. Badala yake, aliwaelezea wanafunzi wake kufanya ukumbusho wa kifo chake. (Luka 22:​19, 20) Krismasi na desturi zayo vimekuja kutokana na dini zisizo za kweli za wakati wa zamani. Ni hivyo hivyo kuhusu desturi za Ista, kama vile matumizi ya mayai au sungura. Wakristo wa kwanza hawakusherehekea Krismasi au Ista, nao Wakristo wa kweli hawafanyi hivyo leo.

4. Siku za Kuzaliwa: Misherehekeo miwili tu inayosemwa katika Biblia imefanywa na watu ambao hawakuwa waabudu wa Yehova. (Mwanzo 40:​20-22; Marko 6:​21, 22, 24-27) Wakristo wa kwanza kwanza hawakusherehekea siku za kuzaliwa. Ile desturi ya kusherehekea siku za kuzaliwa inatokana na dini zisizo za kweli za wakati wa zamani. Wakristo wa kweli wanatoa zawadi na kuwa na wakati wa kujifurahisha pamoja wakati wowote mwingine katika mwaka.

5. Kuwaogopa Wafu: Wafu hawawezi kufanya jambo lolote wala kujisikia jambo lolote. Hatuwezi kuwasaidia, nao hawawezi kutuumiza sisi. (Zaburi 146:4; Muhubiri 9:​5, 10) Nafsi inakufa; haiendelei kuishi kisha kufa kwa mutu. (Ezekieli 18:⁠4) Lakini wakati mwingine malaika wabaya, wanaoitwa madaimoni, wanajifanya kuwa roho za watu waliokufa. Desturi yoyote inayohusiana na kuogopa au kuabudu wafu ni mbaya.​—⁠Isaya 8:19.

6. Musalaba: Yesu hakufa juu ya musalaba. Yeye alikufa juu ya muhimili, au muti. Lile neno la Kigiriki lililotafsiriwa “musalaba” katika Biblia nyingi lilimaanisha tu kipande kimoja cha muti. Alama ya musalaba imekuja kutokana na dini zisizo za kweli za wakati wa zamani. Musalaba haukutumiwa au kuabudiwa na wakristo wa kwanza kwanza. Kwa hiyo, unafikiri kwamba ingekuwa sawa kutumia musalaba katika kuabudu?​—⁠Kumbukumbu la Torati 7:26; 1 Wakorinto 10:⁠14.

7. Inaweza kuwa vigumu sana kuachana na mengine ya mambo hayo ambayo watu wanaamini pia na desturi fulani. Watu wa jamaa na marafiki wanaweza kujaribu kukusadikisha usifanye mabadiliko katika mambo unayoamini. Lakini kumupendeza Mungu ndilo jambo la lazima kuliko kuwapendeza watu.​—⁠Mezali 29:25; Matayo 10:​36, 37.

[Picha katika ukurasa wa 22]

Mungu si Utatu

[Picha katika ukurasa wa 23]

Krismasi na Ista zinatokana na dini zisizo za kweli za wakati wa zamani

[Picha katika ukurasa wa 23]

Hakuna sababu yoyote ya kuwaabudu wafu au kuwaogopa

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine