Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwfq habari 19
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Pasaka?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Pasaka?
  • Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mawazo ya watu wengi
  • Juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Pasaka?
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ista?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Pasaka Ni Sikukuu ya Kikristo Kabisa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mambo Watu Wanaamini na Desturi Zisizomupendeza Mungu
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Je, Ni Vibaya Kufanya Sikukuu?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
ijwfq habari 19

Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana / Mazoea / Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Pasaka?

Mawazo ya watu wengi

Uongo: Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Pasaka juu hawako Wakristo.

Ukweli: Tunaamini kama Yesu Kristo ni Mukombozi wetu, na tunafanya yetu yote ili ‘kufuata hatua zake kwa ukaribu.’​—1 Petro 2:21; Luka 2:11.

Uongo: Hamuamini kama Yesu alifufuliwa.

Ukweli: Tunaamini kama Yesu alifufuliwa; tunajua kama ile njo musingi wa imani ya Kikristo na tunaikaziaka sana wakati tuko nahubiri.​—1 Wakorinto 15:3, 4, 12-15.

Uongo: Hamuhangaikie kuona watoto wenu wanakosa ile furaha ya sherehe ya Pasaka.

Ukweli: Tunapenda watoto wetu, na tunatumia wakati mingi juu ya kuwazoeza na kuwasaidia wakuwe na furaha.​—Tito 2:4.

Juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Pasaka?

  • Sherehe ya Pasaka haitegemee Biblia.

  • Yesu alitupatia amri ya kukumbuka kifo yake, hapana ufufuo wake. Tunafanyaka ile ukumbusho kila mwaka mu tarehe ya kifo yake kulingana na kalendari ya miezi ya Biblia .​—Luka 22:19, 20.

  • Tunaamini kama mambo yenye watu wanafanyaka wakati wa kusherehekea Pasaka, inatokana na desturi zenye watu walikuwa wanafuata zamani juu wapate nguvu ya uzazi; kwa hiyo Mungu hapende watu wake wakuwe wanasherehekea Pasaka. Anapenda watu “washikamane na yeye tu,” na anachukia ibada yenye iko amo matendo yenye haimupendeze.​—Kutoka 20:5; 1 Wafalme 18:21.

Tunaamini kama uamuzi wetu wa kukatala kusherehekea Pasaka unategemea kabisa Biblia, yenye inatutia moyo tukuwe na “hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri” kuliko tu kufuata desturi za wanadamu. (Mezali 3:21; Matayo 15:3) Hata kama tunaambiaka watu wengine kuhusu imani yetu juu ya Pasaka, kama wanatuuliza, tunaheshimiaka haki ya kila mutu ya kujiamulia ikiwa ataisherehekea ao hapana.​—1 Petro 3:15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine