Biblia Inasema Nini Kuhusu Ista?
Jibu la Biblia
Biblia haiseme kwamba tunapaswa kufanya siku kubwa ya Ista. Ikiwa unachunguza historia, utaona maana iliyo wazi kabisa ya Ista—ni desturi ambayo inatokana na siku kubwa ya zamani ya kutukuza uwezo wa kuzaa. Fikiria mambo yanayofuata.
Jina: Kitabu kimoja kinasema hivi: ‘Asili ya jina la Kiingereza Easter haijulikane; katika kipindi cha miaka ya 701-800, kasisi Mujerumani Venerable Bede, alichukua jina hilo kutoka kwa jina la mungu mwanamuke wa Wajerumani wa majira ya masika aliyeitwa Eostre.’ (Encyclopædia Britannica). Vitabu vingine vinaonyesha kwamba Ista inatokana na jina la Astarte, mungu mwanamuke wa uzazi wa Wafoinike ambaye kwa Wababiloni anaitwa Ishtari.
Sungura: Munyama huyo ni alama ya uwezo wa kuzaa ‘iliyokuwa ikitumiwa zamani katika sikukuu za wapagani wakati wa majira ya masika huko Ulaya na Mashariki ya Kati.’—Encyclopædia Britannica.
Mayai: Kulingana na kamusi moja (Funk & Wagnalls Standard Dictionary of Folklore, Mythology and Legend), kutafuta mayai ya Ista ambayo watu wanasema kwamba pengine yaliletwa na sungura wa Ista, ‘si muchezo wa watoto tu, lakini ni masalio ya sikukuu za zamani zilizofanywa ili kutukuza uwezo wa kuzaa.’ Watu fulani wanaamini kwamba yai la Ista lenye kupakwa rangi ‘lina nguvu za kimuujiza za kuleta furaha, baraka, afya, na ulinzi.’—Traditional Festivals.
Mavazi mapya ya Ista: “Watu waliona kwamba ni kukosa adabu na hivyo ni bahati mubaya kumusalimu mungu mwanamuke wa Skandinavia wa Majira ya Masika, ao Eastre, bila kuvaa nguo mupya.”—The Giant Book of Superstitions.
Maombi ya kukucha kwa jua: Maombi hayo yamehusianishwa na sikukuu za waabudu wa zamani wa jua ‘zilizofanywa mwanzoni mwa majira ya masika ili kukaribisha jua na uwezo wake mukubwa wa kutolea vitu vyote vilivyokuwa vikikomaa uzima.’—Celebrations—The Complete Book of American Holidays.
Kitabu kimoja kinasema hivi kuhusu mwanzo wa sikukuu ya Ista: ‘Hakuna shaka kwamba Kanisa katika siku zake za kwanza-kwanza lilichukua desturi zake za zamani za kipagani na kuziingiza katika Ukristo.’ (The American Book of Days).
Biblia inatuonya kuhusu kumwabudu Mungu kwa kufuata desturi zinazomuchukiza. (Marko 7:6-8) Barua ya pili kwa Wakorintho 6:17 inasema hivi: “‘Mujitenge,’ asema Yehova, ‘na muache kugusa kiti kilicho najisi.’” Ista ni sikukuu ya kipagani na wote wanaotaka kumupendeza Mungu wataiepuka.