Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lv uku. 209-uku. 211 fu. 2
  • Kufunika Kichwa: Wakati Gani na Sababu Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kufunika Kichwa: Wakati Gani na Sababu Gani?
  • Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Ukichwa mu Kutaniko
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
lv uku. 209-uku. 211 fu. 2

NYONGEZA

Kufunika Kichwa: Wakati Gani na Sababu Gani?

Wakati gani na sababu gani mwanamuke Mukristo anapaswa kufunika kichwa kuhusiana na mambo ya ibada? Acha tuchunguze mambo ambayo mutume Paulo aliandika kwa musaada wa roho ya Mungu juu ya jambo hilo. Anatupatia muongozo unaofaa ili kufanya maamuzi mazuri yanayoonyesha kwamba tunamuheshimu Mungu. (1 Wakorintho 11:3-16) Mutume Paulo anaonyesha mambo matatu tunayopaswa kufikiria: (1) ni kuhusu mambo ao shuguli gani mwanamuke anapaswa kufunika kichwa, (2) ni hali gani zitamulazimisha kufanya hivyo, na (3) ni sababu gani zinazopaswa kumuchochea atii kanuni hiyo.

Mwanamuke Mukristo anafunika kichwa chake wakati anaongoza funzo la Biblia wakati bwana yake iko

Mambo. Mutume Paulo anataja mambo mawili: sala na pia kutoa unabii. (Mustari wa 4, na 5) Sala ni tendo la ibada linalomusaidia mutu azungumuze na Yehova. Leo, Mukristo anapofundisha mambo yaliyo katika Biblia, inaweza kusemwa kuwa anatoa unabii. Je, hiyo inamaanisha kwamba mutume Paulo alitaka kusema kuwa kila wakati mwanamuke anasali ao anafundisha mambo ya Biblia anapaswa kufunika kichwa? Hapana. Hali ndio itaamua ikiwa anapaswa kufunika kichwa ao hapana.

Hali. Maneno ya mutume Paulo yanaonyesha hali mbili: katika familia na katika kutaniko. Anasema hivi: ‘Kichwa cha mwanamuke ni mwanaume. Kila mwanamuke ambaye anasali ao anatoa unabii na kichwa chake kikiwa hakijafunikwa anakiaibisha kichwa chake [ao kukipatisha haya].’ (Mustari wa 3, na 5) Katika mupango wa familia, Yehova amemuweka bwana kuwa kichwa cha bibi yake. Ikiwa mwanamuke anakataa kutambua mamlaka ya bwana yake na kuchukua madaraka ambayo Yehova amemukabizi mwanaume, basi mwanamuke huyo anamupatisha bwana yake haya. Kwa mufano, ikiwa ni lazima aongoze funzo la Biblia na bwana yake iko hapo, anapaswa kufunika kichwa ili kuonyesha kwamba anakubali mamlaka ya bwana yake. Anapaswa kufanya hivyo, iwe bwana yake ni mwenye kubatizwa ao hapana, kwa sababu bwana yake ndiye kichwa cha familia.a Ikiwa ni lazima afundishe ao asali na mutoto wake mwanaume, mwenye kubatizwa, aliye chini ya miaka 18 iko hapo, anapaswa kufunika kichwa pia, si kwa sababu mutoto huyo ni kichwa cha familia, lakini ni kwa sababu ya mamlaka wanaume waliobatizwa wamepewa katika kutaniko la Kikristo.

Hali nyingine ambayo mutume Paulo anazungumuzia sasa ni katika kutaniko; anasema hivi: ‘Mutu yeyote akiwa na muelekeo wa kubishania desturi fulani nyingine, sisi hatuna nyingine, wala makutaniko ya Mungu.’ (Mustari wa 16) Katika kutaniko la Kikristo ni wanaume waliobatizwa ndio wamepewa daraka la kuongoza. (1 Timotheo 2:11-14; Waebrania 13:17) Ni wanaume tu ndio wanawekwa kuwa wazee ao watumishi wa huduma, na Mungu amewapa daraka la kulitunza kundi lake. (Matendo 20:28) Hata hivyo, kuna wakati hali fulani zinaweza kufanya mwanamuke Mukristo atimize jambo ambalo kwa kawaida ni mwanaume aliyebatizwa ndiye anastahili kulifanya. Kwa mufano, anaweza kuongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri kwa sababu hakuna ndugu aliyebatizwa ili kuuongoza. Ao anaweza kuongoza funzo lake la Biblia wakati anatokea katika mahubiri na ndugu mwenye kubatizwa. Kwa sababu mambo hayo ni sehemu ya mambo yanayopaswa kushugulikiwa na kutaniko, anapaswa kufunika kichwa ili kuonyesha kwamba anatimiza daraka ambalo kwa kawaida limepewa wanaume katika kutaniko.

Lakini, kuna mambo mengine mengi yanayohusu ibada ambayo dada anaweza kufanya bila kulazimishwa afunike kichwa. Kwa mufano, wakati anapotoa maelezo kwenye mikutano, anapohubiri nyumba kwa nyumba pamoja na bwana yake ao na ndugu mwengine mwenye kubatizwa, anapojifunza na watoto wake wasiobatizwa ao anaposali pamoja nao, halazimishwe kufunika kichwa. Bila shaka, labda hali zingine zinaweza kutokea, na ikiwa dada hana uhakika kuhusu jambo fulani, anaweza kutafuta majibu katika vitabu vyetu vinavyotegemea Biblia.b Na ikiwa bado hajapata jibu lenye kutosheleza na ikiwa zamiri yake inamuambia afunike kichwa, si vibaya ikiwa anafanya hivyo, kama inavyoonyeshwa kwenye picha iliyo hapa pembeni.

Sababu. Katika mustari wa 10, tunakuta sababu mbili zinazoweza kumuchochea mwanamuke Mukristo kufunika kichwa chake: ‘Mwanamuke anapaswa kuwa na ishara ya mamlaka juu ya kichwa chake kwa sababu ya malaika.’ Kwanza tunaona maneno “ishara ya mamlaka.” Mwanamuke anapofunika kichwa chake anaonyesha kwamba anakubali mamlaka ambayo Yehova amewapa wanaume waliobatizwa katika kutaniko. Kwa kufanya hivyo, dada huyo anaonyesha kwamba anamupenda Yehova Mungu na kwamba yeye ni mushikamanifu kwa Yehova. Sababu ya pili inapatikana katika maneno “kwa sababu ya malaika.” Wakati mwanamuke anafunika kichwa, jambo hilo linawahusu malaika, viumbe wa kiroho vyenye nguvu, namna gani?

Malaika wanapendezwa wanapoona kwamba watumishi wa Mungu wanatii mamlaka yake katika tengenezo lote la Yehova, iwe mbinguni ao duniani. Pia, wanafaidika na mufano muzuri ambao wanadamu wasio wakamilifu wanatoa katika jambo hilo. Wao pia wanapaswa kutii mipango ya Yehova, jambo ambalo malaika fulani walishindwa kutimiza wakati uliopita. (Yuda 6) Leo, malaika wanaweza kuona dada fulani ana uzoefu mwingi, ujuzi mwingi, na akili nyingi kuliko ndugu fulani ambaye ni mwenye kubatizwa katika kutaniko; hata hivyo, dada huyo anatii mamlaka ya ndugu huyo katika kutaniko. Labda, dada huyo hata ni Mukristo aliyetiwa-mafuta ambaye atakuwa mumoja wa wariti pamoja na Kristo. Atakuwa na cheo cha juu kuliko malaika, atatawala pamoja na Kristo mbinguni. Dada huyo ni mufano muzuri kabisa kwa malaika! Kwa kweli, dada wote wana pendeleo nzuri la kuonyesha utii na unyenyekevu kupitia mwenendo wao wa ushikamanifu; mamilioni ya malaika waaminifu wanawatazama!

a Kwa kawaida mwanamuke Mukristo hawezi kusali kwa sauti ikiwa bwana yake aliye Shahidi iko hapo; lakini inawezekana afanye hivyo katika hali zisizo za kawaida, kama vile wakati bwana yake hana uwezo wa kusema kwa sababu ya ungojwa fulani.

b Ili kupata maelezo zaidi, tafazali soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 2, 2015, ukurasa wa 30, na wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2002 ukurasa wa 26-27 na ule wa tarehe 15 Mwezi wa 2, 1977, ukurasa wa 125-128.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine