Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Ikiwa dada anasindikizwa na ndugu ili kuongoza funzo la Biblia kwenye mulango, dada huyo anapaswa kujifunika kichwa?
Wakati dada anaongoza funzo la Biblia kwa ukawaida, na anasindikizwa na ndugu, dada huyo anapaswa kujifunika kichwa. (1 Kor. 11:3-10) Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2002, ukurasa wa 27, unaeleza hivi: “Kwa kuwa funzo hilo huwa limepangwa kimbele, mwenye kuongoza anafundisha na kusimamia. Chini ya hali hizi, funzo hilo ni kama mkutano wa ziada. Dada akiongoza funzo hilo akiwa pamoja na ndugu aliyebatizwa, anapaswa kufunga kitambaa kichwani.” Atafanya hivyo pia wakati anaongoza funzo la Biblia nyumbani, kwenye mulango, ao mahali pengine popote.
Lakini, ikiwa funzo la Biblia halijaanza kuongozwa kwa ukawaida, dada hatahitaji kujifunika kichwa anaposindikizwa na ndugu, hata kama kusudi la kumurudilia mwenye nyumba ni kumuonyesha namna ya kujifunza Biblia ao kuchunguza naye habari fulani inayopatikana katika kichapo kimoja kati ya vichapo ambavyo tunatumia ili kujifunza na watu Biblia. Mara nyingi, funzo la Biblia kwenye mulango linaanzishwa hatua kwa hatua kadiri tunavyomurudilia mwenye nyumba. Kwa hiyo, wahubiri watahitaji kutumia akili nzuri ili kujua ni katika hali gani na wakati gani dada anapaswa kujifunika kichwa.