Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 52 uku. 126-uku. 127 fu. 1
  • Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto​—Je, Wewe Pia Unayaona?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zenye Kuwa Katika 2 Wafalme
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • Wale Wenye Kuwa Pamoja na Sisi Ni Wengi Kuliko Wale Wenye Kuwa Pamoja Nao
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 52 uku. 126-uku. 127 fu. 1
Elisha na mutumishi wake wamezungukwa na maaskari wa Wasiria

52

Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto

Ben-hadadi, Mufalme wa Siria, alikuwa anashambulia Israeli mara mingi. Lakini kila mara nabii Elisha alikuwa anajulisha mufalme wa Israeli, kwa hiyo alikuwa anakimbia. Basi, Ben-hadadi aliamua kukamata Elisha kinguvu. Walimujulisha kama Elisha iko mu muji wa Dotani, basi alituma maaskari wa Siria kule ili wamukamate.

Wasiria walifika Dotani usiku. Asubui, mutumishi wa Elisha alienda inje na akaona kama maaskari mingi walikuwa wamezunguka muji. Akaogopa sana. Kisha, akasema hivi kwa sauti kubwa: ‘Elisha, tutafanya nini?’ Elisha akamuambia: ‘Wale wenye kuwa pamoja na sisi ni wengi kuliko wale wenye kuwa pamoja nao.’ Mara moja Yehova akafanya mutumishi wa Elisha aone namna milima yote ya pembeni-pembeni ilikuwa imejaa farasi na magari ya vita ya moto.

Elisha na mutumishi wake wanaona jeshi la malaika limewazunguka

Wakati maaskari Wasiria walitafuta kukamata Elisha, akasali hivi: ‘Tafazali Yehova, uwafanye wakuwe vipofu.’ Mara moja, wale maaskari, hata kama walikuwa wanaona, hawakujua kama walikuwa wapi. Kisha, Elisha akawaambia: ‘Mulishapotea. Munifuate, nitawapeleka kwa ule mwenye muko munatafuta.’ Wakafuata Elisha mupaka Samaria, kwenye mufalme wa Israeli alikuwa anaishi.

Wakati Wasiria walivumbua kwenye walikuwa, hakukuwa kitu chenye wangeweza kufanya. Mufalme wa Israeli akauliza Elisha: ‘Niwaue?’ Unawaza, Elisha alitumia ile nafasi ili kulipiza kisasi watu wenye walijaribu kumufanya mubaya? Hapana. Elisha aliambia Mufalme wa Israeli: ‘Usiwaue. Uwapatie chakula na uwaache waende.’ Kwa hiyo, mufalme akawafanyia karamu kubwa na akawaacha warudie kwao.

Maaskari Wasiria wako wanakula chakula mu muji wa Samaria

“Huu ndio uhakika wenye tuko nao kwake, kwamba hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.”​—1 Yohana 5:14

Maulizo: Yehova alifanya nini ili kulinda Elisha na mutumishi wake? Unawaza kama na wewe Yehova anaweza kukulinda?

2 Wafalme 6:8-24

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine