Utangulizi wa Sehemu ya 5
Miezi mbili kisha kuvuka Bahari Nyekundu, Waisraeli walifika ku Mulima Sinai. Ku ile mulima, Yehova alifanya agano na Waisraeli juu wakuwe taifa lake la pekee. Aliwachunga na kuwapatia kila kitu chenye walikuwa nacho lazima. Aliwapatia mana ili wakule, fasi ya kuishi yenye usalama, na nguo zao hazikuharibika. Kama uko muzazi, usaidie mutoto wako aelewe juu ya nini Yehova alipatia Waisraeli Sheria, tabenakulo, na makuhani. Umuonyeshe sababu gani tunapaswa kutimiza mambo yenye tulisema tutafanya, kuendelea kuwa wanyenyekevu, na kuwa washikamanifu kwa Yehova sikuzote.