WIMBO 44
Sala ya Mutu wa Hali ya Chini
Maandishi
1. Yehova nakuomba:
‘Sikia sala yangu.’
Magumu yenye niko nayo
iko ya mingi.
Ninavunjika moyo na
ninahangaika.
Mungu wa faraja,
ninaomba musaada.
(REFREE)
Niongoze, nifariji;
Nipe nguvu nisimame.
Eh! Yehova, nakuomba
Nipatie nguvu mupya.
2. Nikichoka, Neno yako
inanipa nguvu.
Muko maneno yenye
ningependa kusema.
Nipe imani na nijue
kama upendo
Wako ni mukubwa kuupita
moyo wangu.
(REFREE)
Niongoze, nifariji;
Nipe nguvu nisimame.
Eh! Yehova, nakuomba
Nipatie nguvu mupya.
(Ona pia Zb. 42:6; 119:28; Ro. 8:26; 2 Ko. 4:16; 1 Yo. 3:20.)