WIMBO 76
Sema Vile Unajisikiaka
1. Sema vile weye
unajisikiaka,
Kama tu unapata
Wenye kupendezwa.
Kisha kujikaza
Kufundisha wengine,
Umuache Yehova
Awakomalishe.
(REFREE)
Nafurahi kupatia
Mungu nguvu yangu yote,
Na sauti yangu ili
Kumusifu sana.
2. Sema vile weye
unajisikiaka,
Watu wakiitika
Kweli ya Ufalme.
Hata wakatale,
Ao watufukuze,
Siye hatutaacha
Kuwahubiria.
(REFREE)
Nafurahi kupatia
Mungu nguvu yangu yote,
Na sauti yangu ili
Kumusifu sana.
3. Sema vile weye
unajisikiaka,
Kuona vile Mungu
Anakupa nguvu.
Tuko nafundisha
Wenye wanapendezwa;
Sababu ule mwisho
Unakaribia.
(REFREE)
Nafurahi kupatia
Mungu nguvu yangu yote,
Na sauti yangu ili
Kumusifu sana.
(Ona pia Mdo. 13:48; 1 Te. 2:4; 1 Ti. 1:11.)