Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lmd somo 5
  • Busara

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Busara
  • Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yenye Paulo Alifanya
  • Mufano wa Paulo Unatufundisha Nini?
  • Umuige Paulo
  • “Wamutafute Mungu, . . . na kwa Kweli Wamupate”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Unyenyekevu
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Watu wa Eneo Lako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Kupendezwa na Watu
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
Ona Habari Zaidi
Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
lmd somo 5

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

Mutume Paulo iko nazungumuza na watu wa Atene.

Mdo. 17:22, 23

SOMO YA 5

Busara

Kanuni: “Maneno yenu yakuwe yenye kupendeza sikuzote.”​—Kol. 4:6.

Mambo Yenye Paulo Alifanya

Mutume Paulo iko nazungumuza na watu wa Atene.

VIDEO: Paulo Anahubiria Watu wa Atene

1. Angalia VIDEO, ao usome Matendo 17:22, 23. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1. Paulo alijisikia namna gani juu ya matendo ya watu wa madini ya uongo kule Atene?​—Ona Matendo 17:16.

  2. Kuliko kuwahukumu, namna gani Paulo alizungumuza nao kwa busara wakati alitumia mambo yenye waliamini juu ya kuwahubiria habari njema?

Mufano wa Paulo Unatufundisha Nini?

2. Kama tunachagua muzuri mambo yenye tutasema, namna tutaisema, na wakati tutaisema, watu wanaweza kufurahia kutusikiliza.

Umuige Paulo

3. Chagua maneno muzuri. Kwa mufano, wakati unaongea na mutu mwenye iko mu dini yenye haiko ya Kikristo, inaweza kuwa muzuri kubadilisha namna utatanguliza andiko ao mambo yenye utasema juu ya Yesu.

4. Usikuwe haraka kurekebisha mutu. Umuache ajieleze waziwazi bila kumukatiza. Kama anasema jambo fulani yenye haipatane na mafundisho ya Biblia, uepuke kabisa kubishana naye. (Yak. 1:19) Kama unamusikiliza njo utafikia kujua mawazo yenye kuwa ndani ya moyo wake.​—Mez. 20:5.

5. Kama inafaa, ukubali mawazo yake na umupongeze. Pengine iko hakika kama mambo yenye anaamini njo ya kweli. Ku mwanzo, uzungumuzie kwanza mambo yenye nyiye wote munaamini. Polepole njo utamusaidia kuelewa mambo yenye Biblia inafundisha.

ONA PIA

Mez. 25:15; 2 Ti. 2:23-26; 1 Pe. 3:15

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine