Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lmd somo 8
  • Uvumilivu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uvumilivu
  • Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yenye Yesu Alifanya
  • Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?
  • Umuige Yesu
  • Muendelee Kuwa na Uvumilivu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri— Kufundisha Kupitia Video
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Zabihu ya Yesu Ikuletee Faida?
    Habari Zingine
  • Kupendezwa na Watu
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
Ona Habari Zaidi
Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
lmd somo 8

KUENDELESHA MAZUNGUMUZO

Yesu anamukaribia ndugu yake Yakobo fasi ya kufanyia kazi ya useremala. Yakobo anashangaa wakati anamuona.

Yoh. 7:3-5; 1 Ko. 15:3, 4, 7

SOMO YA 8

Uvumilivu

Kanuni: “Upendo ni wenye uvumilivu.”​—1 Ko. 13:4.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

Yesu anamukaribia ndugu yake Yakobo fasi ya kufanyia kazi ya useremala. Yakobo anashangaa wakati anamuona.

VIDEO: Yesu Anamusaidia Ndugu Yake kwa Uvumilivu

1. Angalia VIDEO, ao usome Yohana 7:3-5 na 1 Wakorinto 15:3, 4, 7. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1. Ku mwanzo, namna gani ndugu za Yesu walipokea ujumbe wake?

  2. Nini njo inaonyesha kama Yesu aliendelea kumusaidia ndugu yake Yakobo?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Inaomba tukuwe wavumilivu juu watu fulani hawaitikake habari njema haraka.

Umuige Yesu

3. Tumikisha njia zingine. Kama mutu hakubali mara moya funzo ya Biblia, usimukaze. Kwa wakati wenye kufaa, tumikisha mavideo ao habari fulani zenye zitamusaidia ajue namna funzo ya Biblia inafanyikaka na namna inaweza kumusaidia.

4. Usilinganishe watu. Kila mutu iko namna yake. Kama mutu fulani wa familia ao mutu mwenye unarudilia iko nasita kukubali funzo ya Biblia ao kuamini kweli fulani ya Biblia, ujikaze kujua ni juu ya nini. Inawezekana pengine anapendaka sana fundisho fulani ya dini? Ao pengine ni juu watu fulani wa familia ao majirani wako namuchekelea na kumukaza aache kujifunza? Umuachie wakati juu afikirie mambo fulani yenye mumezungumuzia na aone faida ya kujifunza Biblia.

5. Sali juu ya mutu mwenye kupendezwa. Umuombe Yehova akusaidie usivunjike moyo. Umuombe pia akusaidie ujue ni wakati gani njo unaweza kuacha kumutembelea mutu mwenye hapendezwe sana.​—1 Ko. 9:26.

ONA PIA

Mk. 4:26-28; 1 Ko. 3:5-9; 2 Pe. 3:9

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine