MAISHA YA MUKRISTO
Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri —Kufundisha Kupitia Video
SABABU GANI NI LAZIMA KUFANYA HIVYO:
Video zinaweza kugusa mioyo ya watu kwa sababu zinachochea uwezo wao wa kuona na kusikia. Hilo linasaidia kuvuta uangalifu wa mutu na kumusaidia aendelee kukumbuka mambo yenye amejifunza. Yehova ametuachia mufano muzuri wa kutumikisha vitu vyenye kuonekana ili kufundisha.—Mdo 10:9-16; Ufu 1:1.
Video Mungu Ana Jina?, Ni Nani Aliandikisha Biblia?, na Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli? ni nyongeza za somo ya 2 na ya3 ya broshua Habari Njema. Video Sababu Gani Ujifunze Biblia?, Tunajifunzaka Biblia na Watu Namna Gani?, na Ni Mambo Gani Inafanyikaka Kwenye Jumba la Ufalme? zinatia watu moyo wajifunze na sisi Biblia ao wakuje kwenye mikutano. Video fulani kati ya video zetu za murefu zaidi zinaweza pia kutumiwa ili kufundisha wakati tunaongoza mafunzo.——km 5/13 uku. 3.
NAMNA YA KUFANYA:
Chukua kwenye Internete video yenye umepanga kuonyesha musikilizaji
Tayarisha ulizo moja ao mbili zenye video hiyo itajibia
Muangalie video hiyo pamoja
Muzungumuzie mawazo makubwa
TUMIKISHA SHAURI HILI:
Enda kwenye ukurasa wa mwisho wa trakte, na uonyeshe musikilizaji alama yenye kuongoza kwenye video Sababu Gani Ujifunze Biblia? kwenye Internete
Onyesha video Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli? na utolee musikilizaji broshua Habari Njema, kisha umuonyeshe somo la 3