Umukaribie Mungu
‘Nafsi Yako Itainama juu Yangu’
SIFA ya unyenyekevu inavutia. Kwa kawaida, tunavutiwa na watu wanyenyekevu. Jambo la kuhuzunisha ni hili: Leo ni vigumu kupata watu wanyenyekevu kwelikweli; hasa watu wenye mamlaka ni watu wasio na unyenyekevu. Tuseme nini juu ya Yehova Mungu, Mutu mwenye mamlaka zaidi katika ulimwengu wote? Je, yeye ni munyenyekevu? Ili kujua jambo hilo, tuzungumuzie maneno ya nabii Yeremia katika andiko la Maombolezo 3:20, 21.—Soma.
Yeremia alipoandika kitabu cha Maombolezo, taifa la Israeli lilikuwa katika hali ya magumu. Alitoka tu kujionea jambo fulani ambalo lilimuletea huzuni sana; Wababiloni waliharibu muji wa Yerusalemu ambao alikuwa anapenda sana. Nabii huyo alihuzunika sana ijapokuwa alijua kama kuharibiwa kwa muji wa Yerusalemu ilikuwa hukumu ya haki ya Mungu juu ya Waisraeli kwa sababu ya zambi zao. Lakini, je, Yeremia alikuwa na tumaini lolote? Je, aliwaza kama Yehova alikuwa mbali sana na kwa hiyo hangeweza kuona watu waliotubu na kuwapa tumaini? Sikia maneno ambayo Yeremia alisemea watu wa taifa lake.
Hata ikiwa watu wengi walikuwa na huzuni, Yeremia alikuwa na tumaini kubwa. Alimulilia Yehova hivi: “Hakika nafsi yakoa [Yehova mwenyewe] itakumbuka na kuinama juu yangu.” (Mustari wa 20) Yeremia alikuwa na tumaini kabisa. Alijua kama Yehova hangemusahau yeye na Waisraeli wengine waliotubu. Basi, Mungu mweza-yote angefanya nini kwa ajili yao?—Ufunuo 15:3.
Yeremia alikuwa hakika kama Yehova ‘atainama’ ao kujishusha kuelekea wale waliotubu kwelikweli. Tafsiri nyingine inasema hivi: ‘Kumbuka, na uniinamie.’ Maneno hayo yanatusaidia kuona Yehova kuwa mutu anayetuhangaikia kwa upendo. Yehova, ‘Aliye Juu Zaidi ya dunia yote,’ atainama ao kujishusha ili kuwainua tena waabudu wake watoke katika hali mbaya, na kuwafanya tena wawe na tumaini. (Zaburi 83:18) Ijapokuwa Yeremia alikuwa na huzuni sana, tumaini hilo lilimutegemeza na kumufariji. Kwa hiyo, nabii huyo mwaminifu alikusudia kuvumilia mupaka wakati ambapo Yehova angewakomboa watu Wake waliotubu.—Mustari wa 21.
Maneno hayo yaliyoandikwa na Yeremia yanatufundisha kabisa mambo mawili juu ya Yehova. Jambo la kwanza, Yehova ni munyenyekevu. (Zaburi 18:35) Ijapokuwa Yehova ni mwenye nguvu sana, yeye iko tayari kujishusha sana ili kutusaidia tunapovunjika moyo. (Ayubu 37:23; Zaburi 113:5-7) Hilo ni jambo lenye kutia moyo kabisa, sivyo? Jambo la pili, Yehova ni mwenye rehema; iko “tayari kusamehe” wafanya zambi wanaotubu na kuwakubali tena. (Zaburi 86:5) Sifa ya unyenyekevu na sifa ya rehema zinaenda pamoja; mutu munyenyekevu ni mwenye rehema pia.
Sisi ni wenye shukurani sana kwa sababu Yehova ni tofauti kabisa na viongozi wanadamu, ambao kwa sababu ya kiburi, wana mioyo migumu na hawahangaikie wengine! Je, mambo hayo hayakuchochee kujifunza mengi juu ya Mungu munyenyekevu aliye tayari “kuinama” ao kujishusha ili kuwapatia waabudu wake tumaini?
Tafazali mwezi huu wa 6, soma maandiko haya katika biblia:
◼ Yeremia sura ya 51-52–Ezekieli sura ya 1-5
[Maelezo ya chini]
a Waandishi wa zamani walibadilisha maneno “nafsi yako” katika andiko hilo na kusema “nafsi yangu,” ili kuonyesha kama yanamuhusu Yeremia. Labda waliwaza kama kusema nafsi ya Mungu ni kumukosea heshima, kwa sababu Biblia inatumia neno nafsi kwa ajili ya viumbe vilivyo duniani. Lakini, Biblia inapozungumuza juu ya Mungu, mara nyingi inatumia maneno ambayo watu wanaweza kuelewa. Kwa sababu neno “nafsi” linaweza kumaanisha “uzima tulio nao,” maneno “nafsi yako” yanamaanisha “wewe.”
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 14]
Yehova iko tayari kujishusha sana ili kutusaidia tunapovunjika moyo