Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/2 uku. 4
  • Musa​—Mwanaume Aliyeonyesha Imani Yenye Nguvu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Musa​—Mwanaume Aliyeonyesha Imani Yenye Nguvu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuige Imani ya Musa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Unamuona “Yeye Asiyeonekana”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Musa​—Mwanaume Aliyeonyesha Upendo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Muti Mudogo Unawaka Moto
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/2 uku. 4

Musa​—Mwanaume Aliyeonyesha Imani Yenye Nguvu

IMANI NI NINI? Neno “imani” kama linavyotumiwa katika Biblia, linamaanisha kusadiki kabisa jambo fulani kwa kutegemea mambo yaliyo hakika. Mutu anayemuamini Mungu ana uhakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake zote.

[Picha katika ukurasa wa 4]

MUSA ALIONYESHA IMANI NAMNA GANI? Musa alifanya maamuzi ambayo yalionyesha kwamba aliamini ahadi za Mungu. (Mwanzo 22:15-18) Alikuwa na nafasi ya kuishi maisha ya raha katika utajiri wa Misri, lakini aliachana na mambo hayo, ‘akachagua kutendewa vibaya pamoja na watu wa Mungu badala ya kufurahia zambi kwa muda.’ (Waebrania 11:25) Je, alifanya uamuzi huo bila kufikiri, na hivyo akasikitika baadaye kwa sababu ya uamuzi ambao alifanya? Hapana, kwa sababu Biblia inasema kwamba Musa ‘aliendelea kuwa imara kama mutu anayemuona Yeye asiyeonekana.’ (Waebrania 11:27) Musa hakusikitika hata kidogo kwa sababu ya maamuzi aliyofanya kwa imani.

Musa alitafuta kusaidia wengine wawe na imani yenye nguvu katika Mungu. Kwa mufano, fikiria yale yaliyotokea wakati Waisraeli walionekana kuwa wamenaswa kati ya majeshi ya Farao na Bahari Nyekundu. Wakiwa wenye kuogopeshwa sana na ule ulioonekana kuwa musiba uliokaribia kutokea, Waisraeli walimulilia Yehova na Musa. Musa angefanya nini?

Labda Musa hakujua kama Mungu alikuwa karibu kugawanya mara mbili Bahari Nyekundu, na hivyo kuwafungulia Waisraeli njia ili waponyoke. Na alitaka Waisraeli wenzake wawe na uhakika huohuo. Tunasoma hivi: ‘Musa akawaambia watu: Musiogope. Simameni imara muuone wokovu wa Yehova, atakaowafanyia ninyi leo.’ (Kutoka 14:13) Je, Musa aliweza kuwasaidia Waisraeli wenzake wawe na imani yenye nguvu? Ndiyo, kwa sababu Biblia inasema juu ya Musa na Waisraeli hivi: ‘Kwa imani walipita katikati ya Bahari Nyekundu kana kwamba ni juu ya inchi kavu.’ (Waebrania 11:29) Imani ya Musa ilimufaidi yeye na pia kila mutu aliyefuata mufano wa imani yake.

TUNAWEZA KUJIFUNZA NINI JUU YA IMANI YA MUSA? Tunaweza kumuiga Musa kwa kufanya maamuzi ambayo yanaonyesha kwamba tunaamini ahadi za Mungu. Kwa mufano, Mungu anaahidi kwamba atashugulikia mahitaji yetu ya kimwili ikiwa tunatia ibada yake pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu. (Mathayo 6:33) Kwa sababu watu wengi wanatia vitu vya kimwili pa nafasi ya kwanza leo, inaweza kuwa vigumu kwetu kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza. Lakini tunaweza kuwa na uhakika kwamba wakati tunafanya yote tunayoweza ili kufanya maisha yetu yawe mepesi na kutia ibada yake pa nafasi ya kwanza, Yehova atatutolea vitu vyote tunavyohitaji. Anatuhakikishia hivi: “Sitakuacha wala kukutupa hata kidogo.”​—Waebrania 13:5.

[Picha katika ukurasa wa 4]

Tunajikaza pia kusaidia wengine wawe na imani yenye nguvu. Kwa mufano, wazazi wenye hekima wanatambua kwamba wana nafasi kubwa ya kuwasaidia watoto wao wajue kabisa kwamba kuna Mungu na kwamba ametupatia kanuni juu ya mambo yaliyo mema na mambo yaliyo mabaya. Zaidi ya hilo, watoto wanahitaji kusadikishwa kabisa kama kufuata kanuni za Mungu ndiyo njia nzuri zaidi ya maisha. (Isaya 48:17, 18) Wazazi wanawapatia watoto wao zawadi nzuri sana wanapowasaidia kuamini kwamba Mungu “yuko, naye anawapa zawabu wale wanaomutafuta.”​—Waebrania 11:6, La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine