Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/11 uku. 8-9
  • Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Michango Yao ya Zaidi Ilijaza Upungufu wa Wengine
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mutu Mwenye Kuonyesha “Ukarimu Atabarikiwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/11 uku. 8-9
[Picha katika ukurasa wa 8]

Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji

NDUGU François, muzee wa kutaniko katika inchi moja inayoendelea, anaeleza hivi: “Matokeo ya uchaguzi yalipingwa, hilo likatokeza machafuko yenye jeuri, na kulazimisha maelfu ya Mashahidi wa Yehova kukimbia na kuacha nyumba zao. Haikuwa rahisi kupata chakula na dawa, na bei ya vitu hivyo ilipanda sana. Benki zilifungwa, mashine za kusaidia kuchukua feza hazikufanya kazi tena.”

Ndugu wa biro ya tawi walifanya haraka ili kutuma feza na mahitaji ya lazima kwa Mashahidi waliokimbilia katika Majumba ya Ufalme. Vikundi vya wapiganaji vilifunga barabara ili motokari zisipite, lakini kwa kuwa wote walijua kwamba Mashahidi wa Yehova hawajiingize katika siasa, motokari za biro ya tawi ziliruhusiwa kupita.

Ndugu François anaendelea kusema hivi: “Katika barabara inayoongoza kwenye Jumba moja la Ufalme, askari fulani wenye kujificha walipiga motokari masasi. Lakini, masasi ilipita katikati yetu. Tulipoona askari moja, aliyekuwa na silaha katika mikono yake, akija haraka karibu nasi, tuligeuza motokari, na kurudi haraka kwenye biro ya tawi. Tulimushukuru Yehova kwa kuwa sisi wote tulifika salama. Siku iliyofuata, ndugu 130 waliokuwa katika Jumba la Ufalme walifika mahali palipokuwa na usalama. Wengine walikuja kwenye biro ya tawi na tukawatolea mahitaji yao ya kiroho na kimwili mupaka wakati fujo ilimalizika.”

Ndugu François anasema hivi: “Baadaye, biro ya tawi ilipokea barua nyingi kutoka sehemu mbalimbali za inchi hiyo ambazo ndugu na dada waliandika ili kuonyesha shukrani yao ya kutoka moyoni. Kujionea namna ndugu zao kutoka mahali pengine walivyowasaidia, kuliwafanya waendelee kumutegemea Yehova zaidi.”

Wakati wa misiba ya asili ao misiba inayoletwa na wanadamu, hatuwaambie ndugu na dada zetu ‘wajipashe [waote] moto na kula vizuri.’ (Yak. 2:15, 16) Tofauti na hilo, tunajikaza kuwatolea mahitaji yao ya kimwili. Vivyo hivyo, katika siku za mitume, kisha kujulishwa kwamba njaa ingetokea, ‘wanafunzi waliamua, kila mumoja kwa kadiri ambayo yeyote angeweza kutoa, wafanye huduma ya kupeleka misaada kwa akina ndugu waliokuwa wakikaa Yudea.’​—Mdo. 11:28-30.

Sisi watumishi wa Yehova, tuko tayari kusaidia wale walio katika uhitaji wa kimwili. Lakini watu wana lazima ya kuhangaikiwa kiroho. (Mt. 5:3) Ili kuwasaidia watambue uhitaji wao wa kiroho na namna ya kuutosheleza, Yesu aliamuru wafuasi wake wafanye watu kuwa wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Kila Shahidi wa Yehova anatoa wakati, nguvu, na mali yake ili kutegemeza kazi ya kufanya wanafunzi. Tengenezo la Yehova linatumia michango ili kutoa misaada ya kimwili, lakini michango hiyo inatumiwa zaidi sana ili kutegemeza faida za Ufalme na kueneza habari njema duniani pote. Tunapohubiri na kutoa michango, hilo linaonyesha kwamba tunapenda Mungu na majirani zetu.​—Mt. 22:37-39.

Wote wanaotoa michango ili kutegemeza kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri inayofanywa duniani pote wanapaswa kuwa hakika kwamba michango yao inatumiwa kwa njia nzuri sana. Je, uko tayari kusaidia ndugu zako walio katika uhitaji? Je, una nia ya kutegemeza kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi? Ikiwa ndiyo, ‘usiwanyime watu mema wanayostahili, mukono wako ukiwa na uwezo wa kuyafanya.’​—Met. 3:27.

NJIA MBALIMBALI ZA KUTOA MICHANGO

Kama ilivyokuwa katika siku za Paulo, leo wengi ‘wanaweka kando kitu fulani,’ ao kiasi fulani cha feza ambazo watatia katika kisanduku chenye maneno “Kazi ya Ulimwenguni Pote.” (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko yanatuma feza hizo kwenye biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi ya kuhubiri katika inchi yao. Unaweza pia kutuma wewe mwenyewe michango yako kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika inchi yenu. Ukitaka kujua shirika linalokubaliwa kisheria ambalo Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu, andikia biro ya tawi ya inchi yenu. Unaweza kupata adresi ya biro ya tawi kwenye www.jw.org.

  • KUKOPESHA BIRO YA TAWI FEZA

    Unaweza kukopesha “Association Les Témoins de Jéhovah” feza kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Wakati utahitaji feza zako, biro ya tawi itakurudishia feza hizo bila kukuongezea faida yoyote. Ili kupata habari zaidi unaweza kutumia namba hii ya telefone: 099818 9791 ao 0815551000.

  • MIPANGO MINGINE INAYOHUSU MICHANGO

    Kuna njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Njia hizo zinatia ndani:

    Bima ao Asiranse: Unaweza kuandika kwamba “Association Les Témoins de Jéhovah” ndiyo itachukua feza zako za asiranse ao za pansio. Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili ajue jinsi ya kufanya.

    Akaunti za Benki: Mutu anaweza kutuma zawadi yake kwa kutia feza katika akaunti ya benki ya “Association Les Témoins de Jéhovah.” Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili ajue namba ya akaunti ambayo kupitia hiyo atatuma zawadi yake.

    Nyumba ao Parsele: Unaweza kuitoa kuwa zawadi. Unaweza kuendelea kuishi katika nyumba hiyo mupaka utakapokufa. Mbele ya kutoa zawadi kama hiyo unapaswa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ya inchi yenu.

    Zawadi: Ni mupango wa kutoa feza ao vitu vingine ili viwe mali ya shirika fulani linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova. Yule anayependa kutoa zawadi ili kutegemeza kazi ya Ufalme, anapaswa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria kuhusiana na zawadi ambayo anapenda kutolea “Association Les Témoins de Jéhovah.”

    Wasia ao testama: Shirika la “Association Les Témoins de Jéhovah” linaweza, kupitia testama, kuachiwa uriti wa mali ao feza. Mbele ya kufanya testama hiyo mutu anapaswa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria.

Usemi “mipango mingine inayohusu michango” unaonyesha kwamba ili mutu afanye michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango fulani kamili. Broshua Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide katika Kihispania na Kiingereza imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotamani kutoa michango ili kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri ulimwengu pote iendelee. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa ao kama uriti mutu anapokufa. Kisha kusoma broshua hiyo na kushauriana na washauri wao wa mambo ya kisheria ao kodi, watu wengi wamesaidia kutegemeza kazi yetu ya kuhubiri na wanatoa misaada ulimwenguni pote na kupunguziwa kodi wanapofanya hivyo. Ikiwa unapenda kupata broshua hiyo unaweza kuiomba kwenye biro ya tawi.

Ili kupata habari zaidi, unaweza kuzungumuza na biro ya tawi. Unaweza pia kutuma barua kwenye adresi ya B.P. 634, Limete-Kinshasa, ao kuita namba zilizo hapa chini.

“Association Les Témoins de Jéhovah” no 75, 13ème Rue, Industriel, Limete-KINSHASA, République Démocratique du Congo.

Telefone: 099 818 9791 ao 0815551000

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine