Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w16 Mwezi wa 11 uku. 19-20
  • “Kazi Ni Kubwa”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Kazi Ni Kubwa”
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Michango Yao ya Zaidi Ilijaza Upungufu wa Wengine
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mutu Mwenye Kuonyesha “Ukarimu Atabarikiwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
w16 Mwezi wa 11 uku. 19-20
Mufalme Daudi anaonyesha mwanaume fulani plan za majengo ya hekalu; ndugu mumoja anaangalia plan za nyumba yenye atajenga

“Kazi Ni Kubwa”

NI WAKATI wa mukutano wa maana sana katika Yerusalemu. Mufalme Daudi ameita wakubwa, maofisa, na wanaume wenye nguvu. Wanafurahi kusikia tangazo la pekee. Yehova amechagua Sulemani, mutoto wa Daudi, ili ajenge jengo la pekee kwa ajili ya ibada ya Mungu wa kweli. Mufalme Daudi mwenye kuzeeka, amepewa plan ya jengo hilo kupitia roho ya Mungu na ameipatia Sulemani. Daudi anasema hivi: “Kazi ni kubwa; kwa kuwa jumba hilo la kifalme si la mwanadamu, bali ni la Yehova Mungu.”—1 Nya. 28:1, 2, 6, 11, 12; 29:1.

Kisha Daudi anauliza hivi: ‘Na ni nani anayejitolea kuujaza mukono wake leo kwa zawadi kwa ajili ya Yehova?’ (1 Nya. 29:5) Ikiwa ulikuwa hapo, ungetenda namna gani? Moyo wako ungekuchochea kutegemeza kazi hiyo kubwa? Waisraeli walitenda bila kukawia. Kwa kweli, ‘walishangilia kutokana na matoleo yao ya hiari [ya kujipendea] waliyotoa, kwa maana walimutolea Yehova matoleo ya hiari kwa moyo kamili.’—1 Nya. 29:9.

Mamia ya miaka kisha hapo, Yehova alianzisha jambo kubwa zaidi kuliko hekalu hilo. Alianzisha hekalu kubwa la kiroho, ni kusema, mupango ili wanadamu wamukaribie katika ibada kwa musingi wa zabihu ya Yesu. (Ebr. 9:11, 12) Namna gani Yehova anasaidia watu wamukaribie leo? Ni kupitia kazi yetu ya kufanya wanafunzi. (Mt. 28: 19, 20) Kupitia kazi hiyo, kila mwaka tunaongoza mamilioni ya mafunzo ya Biblia, maelfu ya wanafunzi wanabatizwa, na mamia ya makutaniko yanaanzishwa.

Kwa sababu ya ongezeko hilo, inaomba kuchapisha vichapo vingi zaidi vyenye kutegemea Biblia, kujenga na kutunza Majumba ya Ufalme, na kupata Majumba kwa ajili mikusanyiko. Kwa kweli, kazi yetu ya kutangaza habari njema ni kazi kubwa na yenye kuleta baraka!—Mt. 24:14.

Upendo kwa Mungu na jirani, na kujua kama kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme ni ya haraka, vinachochea watu wa Mungu ‘kuujaza mukono wao . . . kwa zawadi kwa ajili ya Yehova’ kwa kutoa michango ya kujipendea. Ni jambo lenye kufurahisha sana ‘kumuheshimu Yehova kwa vitu [vyetu] vyenye samani’ na kuona namna michango hiyo inatumiwa kwa uaminifu na kwa busara ili kufanya kazi kubwa zaidi katika historia ya wanadamu!—Met. 3:9.

Njia Mbalimbali Za Kutoa Michango

Kama vile Wakristo wa wakati wa mitume, leo ndugu na dada wengi wanaweka pembeni feza za kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote na kuzitia katika visanduku vya michango katika kutaniko lao. (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko yanatuma feza hizo kwenye biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova yenye kusimamia kazi ya kuhubiri katika inchi yao. Unaweza pia kutuma wewe mwenyewe michango yako kwenye shirika lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu. Ili kujua shirika lenye kukubaliwa kisheria lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu, andikia biro ya tawi ya inchi yenu. Unaweza kupata adresi ya biro ya tawi kwenye www.jw.org.

KUKOPESHA BIRO YA TAWI FEZA

  • Unaweza kukopesha “Association Les Témoins de Jéhovah” feza kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Wakati utakuwa na lazima ya feza zako, biro ya tawi itakurudishia feza hizo bila kukuongezea faida yoyote.

  • Ili kupata habari zaidi unaweza kutumia namba hii ya telefone: 0998189791 ao 0815551100

MIPANGO MINGINE YENYE KUHUSU MICHANGO

  • Kuko njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote.

  • Njia hizo ni:

Bima ao Asiranse:

Unaweza kuandika kwamba “Association Les Témoins de Jéhovah” ndiyo itachukua feza zako za asiranse ao za pansio. Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namna ya kufanya.

Akaunti za Benki: Mutu anaweza kutuma zawadi yake kwa kutia feza katika akaunti ya benki ya “Association Les Témoins de Jéhovah.” Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namba ya akaunti yenye atatumia ili kutuma zawadi yake.

Nyumba ao Parsele: Unaweza kuitoa kuwa zawadi. Unaweza kuendelea kuishi katika nyumba hiyo mupaka utakufa. Mbele ya kutoa zawadi kama hiyo unapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ya inchi yenu.

Zawadi: Ni mupango wa kutoa feza ao vitu vingine ili vikuwe mali ya shirika fulani lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia. Ule mwenye anapenda kutoa zawadi ili kutegemeza kazi ya Ufalme, anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria kuhusiana na zawadi yenye anapenda kutolea “Association Les Témoins de Jéhovah.”

Wasia ao testama: Shirika la “Association Les Témoins de Jéhovah” linaweza, kupitia testama, kuachiwa uriti wa mali ao feza. Mbele ya kufanya testama hiyo, mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria.

Usemi “mipango mingine inayohusu michango” unaonyesha kwamba ili mutu afanye michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango fulani kamili. Broshua Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide katika Kihispania na Kiingereza, imetayarishwa ili kuwasaidia watu wenye wanapenda kutoa michango ili kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri ulimwenguni pote iendelee. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa, ao kama uriti wakati mutu anakufa. Kisha kusoma broshua hiyo na kupata mashauri ya washauri wao wa mambo ya kisheria ao kodi, watu wengi wamesaidia kutegemeza kazi yetu ya kuhubiri na wanatoa misaada ulimwenguni pote na kupunguziwa kodi wakati wanafanya hivyo. Ikiwa unapenda kupata broshua hiyo unaweza kuiomba kwenye biro ya tawi.

Ili kupata habari zaidi, fungua adresi yetu ya Internete jw.org, kwenye ukurasa wa kwanza kwenye sehemu ya chini yenye kichwa “Toa Muchango kwa Ajili ya Kazi Yetu ya Kuhubiri Katika Dunia Yote,” ao unaweza kuandikia biro ya tawi kwa kutuma barua kwenye adresi ya B.P. 634, Limete-Kinshasa, ao kuita namba zenye kupatikana hapa chini.

“Association Les Témoins de Jéhovah” no 75, 13ème Rue, Industriel, Limete-KINSHASA, République Démocratique du Congo.

Telefone: 0998189791 ao 0815551100

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine