Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w17 Mwezi wa 11 uku. 18-19
  • Mutu Mwenye Kuonyesha “Ukarimu Atabarikiwa”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mutu Mwenye Kuonyesha “Ukarimu Atabarikiwa”
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Michango Yao ya Zaidi Ilijaza Upungufu wa Wengine
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
w17 Mwezi wa 11 uku. 18-19
Hana anapeleka mutoto Samweli kwenye tabenakulo

Mutu Mwenye Kuonyesha “Ukarimu Atabarikiwa”

TANGU zamani, kutoa zabihu kumekuwa sehemu ya maana sana ya ibada ya kweli. Waisraeli walitoa zabihu za wanyama, na Wakristo wamejulikana siku zote kuwa wenye kutoa ‘zabihu ya sifa.’ Lakini, kuko zabihu zingine zenye kumupendeza Mungu. (Ebr. 13:15, 16) Zabihu hizo zinaleta furaha na baraka, kama vile mifano yenye kufuata inaonyesha.

Hana, mutumishi mwaminifu wa zamani wa Mungu, alipenda sana kuwa na mutoto mwanaume lakini hakukuwa na uwezo wa kuzaa watoto. Katika sala, alifanya naziri kwa Yehova kwamba ikiwa anazaa mutoto mwanaume, ‘atamutoa kwa Yehova siku zote za maisha yake.’ (1 Sam. 1:10, 11) Kisha wakati fulani, Hana akapata mimba, na akazaa mutoto mwanaume na kumupatia jina la Samweli. Kisha Samweli kuachishwa kunyonya, Hana alimupeleka kwenye tabenakulo, kama vile tu alikuwa ametoa naziri. Yehova alimubariki Hana kwa sababu ya roho yake ya kujitoa. Alipata pendeleo la kuzaa watoto wengine tano, na Samweli akakuwa nabii na muandikaji wa Biblia.​—1 Sam. 2:21.

Kama Hana na Samweli, leo Wakristo wako na pendeleo la kutumia maisha yao katika utumishi mutakatifu kwa Muumbaji wao. Yesu aliahidi kuwa tutabarikiwa sana kwa sababu ya kila jambo lenye tunajinyima ili kumuabudu Yehova.​—Mk. 10:28-30.

Wakati wa mitume, mwanamuke mumoja Mukristo mwenye kuitwa Dorkasi alijulikana sana kwa sababu ya “matendo mema na zawadi za rehema,” ni kusema, zabihu zenye alitoa ili kusaidia wengine. Hata hivyo, jambo la kuhuzunisha ni kwamba, “alishikwa na ugonjwa akafa,” hilo lilihuzunisha sana kutaniko. Wakati wanafunzi walisikia kwamba Petro alikuwa katika eneo hilo, walimuomba akuje bila kukawia. Wazia furaha yenye walikuwa nayo wakati Petro alimufufua Dorkasi; huo ndio ulikuwa ufufuo wa kwanza wenye ulifanywa na mutume wenye kuandikwa katika Biblia! (Mdo. 9:36-41) Mungu alikuwa hajasahau zabihu za Dorkasi. (Ebr. 6:10) Habari juu ya ukarimu wake imeandikwa katika Neno la Mungu ili kutuonyesha mufano wa muzuri wenye tunaweza kuiga.

Vilevile mutume Paulo alituachia mufano wa muzuri sana kwa kutumia wakati wake kwa ukarimu na kuhangaikia sana watu. Wakati aliandikia ndugu zake Wakristo katika Korintho, Paulo alisema hivi: “Kwa upande wangu mimi nitatumia kwa furaha zaidi na kutumiwa kabisa kwa ajili ya nafsi zenu.” (2 Kor. 12:15) Mambo yenye Paulo alijionea yalimufundisha kuwa kujitoa kwa ajili ya wengine kunaletea mutu furaha, lakini pia jambo la maana zaidi, kunaleta baraka za Yehova na kukubaliwa naye.​—Mdo. 20:24, 35.

Ni wazi kwamba, Yehova anapendezwa wakati tunatumia wakati na nguvu yetu ili kuendeleza faida za Ufalme na kusaidia Wakristo wenzetu. Lakini kuko njia zingine zenye tunaweza kutumia ili kutegemeza kazi ya kuhubiri Ufalme? Ndiyo! Zaidi ya matendo yetu ya upendo, tunaweza kumuheshimia Mungu kwa kutoa michango ya kujipendea. Michango hiyo inatumiwa ili kuendeleza kazi ya kuhubiri katika dunia yote, kazi hiyo inatia ndani kutegemeza wamisionere na watumishi wengine wa wakati wote. Zaidi ya hilo, kutayarisha na kutafsiri vichapo na video, kutoa misaada wakati wa misiba, na ujenzi wa Majumba ya Ufalme; kazi hizo zote zinategemezwa na michango yetu ya kujipendea. Tunaweza kuwa hakika kuwa mutu mwenye kuonyesha “ukarimu atabarikiwa.” Zaidi ya hilo, wakati tunamutolea Yehova vitu vyetu vya maana, tunamuheshimia.​—Met. 3:9; 22:9.

Njia Mbalimbali za Kutoa Michango

Kama vile Wakristo wa wakati wa mitume, leo ndugu na dada wengi wanaweka pembeni feza za kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote na kuzitia katika visanduku vya michango katika kutaniko lao. (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko yanatuma feza hizo kwenye biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova yenye kusimamia kazi ya kuhubiri katika inchi yao. Unaweza pia kutuma wewe mwenyewe michango yako kwenye shirika lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu. Ili kujua shirika lenye kukubaliwa kisheria lenye Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu, andikia biro ya tawi ya inchi yenu. Unaweza kupata adresi ya biro ya tawi kwenye www.jw.org.

MICHANGO YA KUJIPENDEA

  • Unaweza kutoa muchango kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia karte ya benki. Katika tawi fulani hilo linawezekana pia kwa kutumia adresi yetu ya Internete jw.org ao adresi ingine yenye kuonyeshwa.

  • Michango ya feza za moja kwa moja. Unaweza kutia ndani barua yenye kuonyesha kuwa unatoa muchango wa kujipendea.

MIPANGO KUHUSU MICHANGO

Zaidi ya kutoa zawadi ya feza, kuko njia zingine za kutegemeza kazi ya Ufalme katika dunia yote. Njia hizo linapatikana hapa chini. Mutu mwenye anapenda kutegemeza kazi ya Ufalme kwa kutumia njia fulani, anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria kuhusiana na zawadi yenye anapenda kutolea “Association Les Témoins de Jéhovah.”

Bima ao Asiranse: Unaweza kuandika kwamba “Association Les Témoins de Jéhovah” ndiyo itachukua feza zako za asiranse ao za pansio. Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namna ya kufanya.

Akaunti za Benki: Mutu anaweza kutuma zawadi yake kwa kutia feza katika akaunti ya benki ya “Association Les Témoins de Jéhovah.”Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namba ya akaunti yenye atatumia ili kutuma zawadi yake.

Nyumba ao Parsele: Unaweza kuitoa kuwa zawadi. Unaweza kuendelea kuishi katika nyumba hiyo mupaka utakufa. Mbele ya kutoa zawadi kama hiyo unapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ya inchi yenu.

Wasia ao testama: Shirika la “Association Les Témoins de Jéhovah” linaweza, kupitia testama, kuachiwa uriti wa mali ao feza. Mbele ya kufanya testama hiyo, mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria.

Usemi “mipango kuhusu michango” unaonyesha kwamba ili mutu afanye michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango fulani kamili. Kwa kutumia mipango hiyo watu wengi wamesaidia kutegemeza kazi yetu ya kuhubiri na wanatoa misaada ulimwenguni pote na kupunguziwa kodi wakati wanafanya hivyo.

Ili kupata habari zaidi, fungua adresi yetu ya Internete jw.org, kwenye ukurasa wa kwanza kwenye sehemu ya chini yenye kichwa “Toa Muchango kwa Ajili ya Kazi Yetu ya Kuhubiri Katika Dunia Yote,” ao unaweza kuandikia biro ya tawi kwa kutuma barua kwenye adresi ya B.P. 634, Limete-Kinshasa, ao kuita namba zenye kupatikana hapa chini.

Telefone: 0998189791 ao 0815551000

“Association Les Témoins de Jéhovah” no 75, 13ème Rue, Industriel, Limete-KINSHASA, République Démocratique du Congo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine