Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/1 uku. 16
  • Uzima Ulianza Namna Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uzima Ulianza Namna Gani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tulitokana na wanyama?
  • Wanyama
    Amuka!—2015
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/1 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Ni nini inayochochea watu wengi wafikirie ikiwa kuna Muumbaji?

Mama anamuangalia mutoto wake kwa furaha

Uzima ni jambo la ajabu, sivyo?

Miaka 3000 hivi iliyopita, muandikaji wa mashairi ao maandishi yaliyopangwa kwa utaratibu fulani aliandika hivi: “Nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.” (Zaburi 139:14) Unapofikiria namna mutoto anakomaa kutokana na chembe moja, hilo halikushangaze sana? Watu wengi wanaamini kuwa vitu vilivyo na uzima viliumbwa na Muumbaji.—Soma Zaburi 139:13-17; Waebrania 3:4.

Yule aliyeumba ulimwengu na kufanya dunia iikaliwe ndiye aliumba pia uzima. (Zaburi 36:9) Amezungumuza na watu na ametuambia juu yake mwenyewe.—Soma Isaya 45:18.

Tulitokana na wanyama?

Katika mambo mengi, miili yetu inafanana na miili ya wanyama. Lakini hilo ni kwa sababu watu na wanyama waliumbwa na Muumbaji ili waishi kwenye dunia. Aliumba mutu wa kwanza kutokana na mavumbi, lakini haiko kutokana na munyama.—Soma Mwanzo 1:24; 2:7.

Watu wako tofauti na wanyama katika mambo mbili ya maana. Jambo la kwanza, watu wana uwezo wa kujua Muumbaji, kumupenda, na kumuheshimu. Jambo la pili, watu waliumbwa ili waishi milele lakini hapana wanyama. Hata hivyo leo, watu wote wanariti kifo kwa sababu mutu wa kwanza alikataa kuongozwa na Muumbaji.—Soma Mwanzo 1:27; 2:15-17.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 1 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine