Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/12 uku. 4-5
  • Biblia Ni Kitabu Chenye Kinaweza Kueleweka

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Ni Kitabu Chenye Kinaweza Kueleweka
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ILIANDIKWA KWA NAMNA YENYE KUELEWEKA
  • WATU WOTE WANAWEZA KUIPATA
  • Sababu Gani Unapaswa Kupendezwa na Biblia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Biblia Ni Neno ya Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Yehova Mungu, Anazungumuza na Watu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Unaweza Kufanya Nini ili Ufurahie Kusoma Biblia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/12 uku. 4-5
Kusoma Biblia yenye kuchapishwa na kwenye telefone

HABARI KUBWA | Unaweza Kuelewa Biblia

Biblia Ni Kitabu Chenye Kinaweza Kueleweka

Kwa kweli, Biblia ni kitabu cha zamani sana. Kiliandikwa wakati gani? Tangu Biblia ilianza kuandikwa, kumekwisha kumepita miaka 3 500 hivi. Kwa kulinganisha, huo ulikuwa wakati wa utawala wenye nguvu wa kizazi cha Shang katika China, na karibu miaka 1 000 hivi mbele dini ya Buda ianze katika India.​—⁠Soma kisanduku “Maelezo Mafupi Juu ya Biblia.”

Biblia inatoa majibu yenye kufurahisha kwa maulizo ya maana sana katika maisha

Ili kitabu kisaidie watu na kiwapatie muongozo wenye kuwaletea faida, wanapaswa kukielewa na kukiona kuwa cha maana. Biblia ni kitabu cha namna hiyo. Inatoa majibu yenye kufurahisha kwa maulizo ya maana sana katika maisha.

Kwa mufano, umekwisha kujiuliza, ‘Sababu gani tuko hapa?’ Ulizo hilo limehangaisha watu kwa miaka mingi, na limeendelea kuhangaisha watu mupaka leo. Lakini, jibu linaweza kupatikana katika sura mbili za kwanza za kitabu cha kwanza cha Biblia, ni kusema, kitabu cha Mwanzo. Katika sura hizo, habari ya Biblia inaanza kwa kuzungumuzia “mwanzo,” ni kusema, mamiliare ya miaka iliyopita, wakati ulimwengu wetu wenye kuwa na vitu kama vile vikundi vya nyota, nyota, na dunia, viliumbwa. (Mwanzo 1:1) Kisha inaeleza hatua kwa hatua namna dunia ilifikia kuwa mahali viumbe vinaweza kuishi, namna viumbe mbalimbali viliumbwa, na namna wanadamu waliumbwa. Inaeleza pia kusudi la mambo hayo yote.

ILIANDIKWA KWA NAMNA YENYE KUELEWEKA

Biblia inatupatia mashauri mazuri ya kutusaidia kupambana na magumu ya kila siku. Mashauri hayo ni mepesi kueleweka. Yanaeleweka kwa sababu mbili.

Kwanza, habari ya Biblia iko wazi, ya moja kwa moja, na yenye kuvutia. Kuliko kutumia maneno mengi yenye hayaeleweke ao ya mafumbo, inatumia maneno yenye kuwa wazi ao yenye tunaweza kuelewa. Mambo magumu yanaelezwa kwa maneno yenye tunatumia katika maisha ya kila siku.

Kwa mufano, Yesu alitumia mifano mingi myepesi yenye kuhusu maisha ya watu ya kila siku ili kuwafundisha mambo yenye yaligusa mioyo yao. Mifano mingi kati ya hiyo, inapatikana katika mahubiri yenye watu wengi wanaita Mahubiri ya Mulimani. Mahubiri hayo yanapatikana katikasura ya 5 mupaka 7 ya kitabu cha Biblia cha Mathayo. Mutu mumoja mwenye kutoa maelezo juu ya Biblia aliita mahubiri hayo “hotuba yenye faida.” Anasema kama kusudi la mahubiri hayo, “haiko kujaza mawazo katika akili zetu, lakini ni kuongoza na kunyoosha matendo yetu.” Pengine unaweza kusoma sura hizo katika dakika 15 mupaka 20, na utashangazwa kuona namna maneno ya Yesu ni mepesi lakini yenye nguvu.

Pili, habari zenye Biblia inazungumuzia zinaifanya pia ikuwe mwepesi kueleweka. Biblia haiko kitabu cha hadisi za kuwazia ao za kutungwa. Lakini, kama vile kitabu kimoja kinaonyesha, sehemu kubwa ya Biblia inazungumuzia “watu wakubwa na wa kawaida” na “magumu yao, matumaini yao, makosa yao, na ushindi wao.” (The World Book Encyclopedia) Ni vyepesi kwetu kuelewa habari hizo zenye kuzungumuzia watu wa kweli na matukio ya kweli na kuelewa mambo yenye habari hizo zinatufundisha.—Waroma 15:4.

WATU WOTE WANAWEZA KUIPATA

Ili uelewe kitabu fulani, kinapaswa kuwa katika luga yenye unajua. Leo, pengine Biblia inapatikana katika luga yenye unaweza kuelewa, hata iwe unaishi wapi ao uko wa inchi gani. Fikiria mambo fulani yenye kufanya jambo hilo kubwa lenye kushangaza liwezekane.

Kazi ya kutafsiri. Biblia iliandikwa kwanza katika luga ya Kiebrania, ya Kiaramu, na ya Kigiriki. Hilo lilifanya watu wengi wasiweze kuisoma. Ili Biblia ikuwe katika luga zingine, bidii nyingi zimefanywa na watafsiri wenye moyo muzuri. Kwa sababu ya bidii yao, leo Biblia imetafsiriwa yote nzima ao sehemu katika luga karibu 2 700. Hilo linamaanisha kama watu zaidi ya 90 juu ya 100 wanaweza kusoma sehemu fulani ya Biblia katika luga yao ya kizalikio.

Kazi ya kuchapisha. Maandishi ya kwanza kwanza ya Biblia yaliandikwa kwenye vitu vyenye vinaweza kuharibika, kama vile kwenye ngozi za wanyama na kwenye makaratasi ya mafunjo (papyrus). Ili kuchunga habari, maandishi hayo yalipaswa kuandikwa kwa uangalifu tena na tena kwa mukono. Kopi za maandishi hayo zilikuwa bei, na watu wachache tu ndio wangeweza kuziuza. Lakini, kupitia mashini ya kuchapisha yenye Gutenberg alitengeneza kumepita miaka zaidi ya 550, Biblia ilianza kupatikana kwa watu wengi sana. Kulingana na uchunguzi mumoja, zaidi ya Biblia miliare tano, zenye kuwa nzima ao sehemu, zimegawanywa.

Katika mambo hayo, hakuna kitabu kingine cha dini chenye kinaweza kulinganishwa na Biblia. Kwa kweli, Biblia ni kitabu chenye kinaweza kueleweka. Lakini inaweza kuwa vigumu kuielewa. Hata hivyo, kuko musaada. Unaweza kuupata wapi? Na unaweza kupata faida gani? Utapata majibu ya maulizo hayo katika habari yenye kufuata.

Maelezo Mafupi Juu ya Biblia

  • Biblia inafanyizwa na vitabu vitakatifu 66.

  • Kati ya mambo yenye kuwa katika Biblia kuko historia, sheria, unabii, mashairi ao maandishi yaliyopangwa kwa utaratibu fulani, mezali, nyimbo, na barua.

  • lianza kuandikwa katika mwaka wa 1513 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu na ikamalizika katika mwaka wa 98 kisha kuzaliwa kwa Yesu, kipindi cha miaka zaidi ya 1 600

  • Wanaume 40 hivi waliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika Biblia.

Uhai—Ulitokana na Muumba?

Ili kupata habari zingine juu ya namna uzima ulianza, soma broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza pia kupata broshua hiyo kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/sw.

Biblia—Ina Ujumbe Gani?

Ili kupata habari zingine juu ya Biblia, soma broshua Biblia​—⁠Ina Ujumbe Gani? yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza pia kupata broshua hiyo kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/sw.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine