Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 1 uku. 5-6
  • Unaweza Kufanya Nini ili Ufurahie Kusoma Biblia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unaweza Kufanya Nini ili Ufurahie Kusoma Biblia?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ni Nani Alitia Sura na Mistari Katika Biblia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Namna ya Kujifunza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Upate Faida Wakati Uko Nasoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Biblia Ni Kitabu Chenye Kinaweza Kueleweka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 1 uku. 5-6
Mwanamuke mumoja anatumia vifaa vya kusaidia kujifunza Biblia wakati anasoma Biblia

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPATA FAIDA WAKATI UNASOMA BIBLIA?

Unaweza Kufanya Nini ili Ufurahie Kusoma Biblia?

Usomaji wako wa Biblia utakuwa wa namna gani? Wa kuchokesha? Ao wa kufurahisha? Jibu linategemea mambo yenye unafanya. Tuone mambo yenye unaweza kufanya ili upendezwe zaidi na usomaji wako na kuufurahia zaidi.

Utumie Biblia yenye kutumainika, na yenye kuwa na maneno yenye kueleweka. Ikiwa unasoma habari yenye kuwa na maneno mengi yenye kuwa nguvu kuelewa ao maneno ya zamani yenye haujue, pengine hautafurahia usomaji wako. Kwa hiyo, tafuta Biblia yenye kutumia maneno mepesi kuelewa yenye yatagusa moyo wako. Lakini, inapaswa pia kuwa yenye kutafsiriwa kwa uangalifu na kwa uaminifu.a

Utumie teknolojia ya sasa. Leo, kuko Biblia zenye kuchapishwa kwenye karatasi (papiers) lakini kuko pia Biblia za kielektroniki. Unaweza kusoma tafsiri fulani kwenye Internete ao kuzichukua na kuziweka kwenye ordinatere, tablete, ao telefone yako kwa ajili ya kusoma. Tafsiri fulani ziko na sehemu zenye kukusaidia kuchunguza bila kukawia maandiko mengine yenye kupatana na andiko lenye unasoma, ao sehemu zenye kukusaidia kulinganisha tafsiri mbalimbali. Ikiwa unapenda kusikiliza kuliko kusoma, kuko pia Biblia yenye kurekodiwa ao ya kusikiliza tu. Watu wengi wanapenda kusikiliza usomaji wa Biblia wakati wako katika chombo fulani cha kusafirisha watu kama vile motokari, wakati wanafua manguo, ao wakati wanafanya mambo mengine yenye yanawaruhusu kusikiliza. Unaweza kuchagua namna moja yenye kukufaa.

Utumie vifaa vya kusaidia kujifunza Biblia. Vifaa vya kusaidia kujifunza Biblia vinaweza kukusaidia upate faida zaidi wakati unasoma. Kuko karte za maeneo yenye kuzungumuziwa katika Biblia. Karte hizo zitakusaidia kujua nafasi kwenye eneo fulani lilipatikana, na utaelewa muzuri habari hiyo. Habari fulani kama vile habari zenye kuwa katika gazeti hili ao katika sehemu “Mafundisho ya Biblia” yenye kuwa kwenye adresi yetu ya Internete jw.org, zinaweza kukusaidia kuelewa maana ya maandiko fulani ya Biblia.

Utumie njia mbalimbali. Ikiwa kusoma Biblia kuanzia mwanzo mupaka mwisho kunaonekana kuwa jambo lenye kuogopesha, jaribu kuchochea hamu yako kwa kuanza na sehemu fulani yenye kukupendeza. Kama unapenda kujifunza juu ya watu wenye kuzungumuziwa katika Biblia, unaweza kujaribu kusoma sehemu za Biblia zenye kuzungumuzia watu hao. Mufano fulani unapatikana katika kisanduku chenye kichwa “Chimba Katika Biblia ili Kujua Watu Wenye Kuzungumuziwa Ndani,” chenye kuwa katika habari hii. Ao pengine unafurahia kusoma Biblia kwa kufuata tungo mbalimbali zenye kuwa ndani ao kwa kufuata mupangilio wa namna mambo yalitokea. Unaweza kujaribu kutumia njia moja kati ya hizo.

a Watu wengi wameona kama Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya imetafsiriwa kwa uaminifu, ni yenye kutegemeka, na ni mwepesi kabisa kuisoma. Biblia hii yenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova inapatikana katika luga zaidi ya 130. Unaweza kuichukua kwenye adresi yetu ya Internete jw.org ao chukua programu ya JW Library. Ao kama unapenda, Mashahidi wa Yehova wanaweza kuja nyumbani kwako ili kukuletea Biblia yenye kuchapishwa.

CHIMBA KATIKA BIBLIA ILI KUJUA WATU WENYE KUZUNGUMUZIWA NDANI

Wanawake fulani waaminifu

Abigaili

1 Samweli sura ya 25

Esta

Esta sura ya 2-5, 7-9

Hana

1 Samweli sura ya 1-2

Maria

(mama ya Yesu) Mathayo sura ya 1-2; Luka sura ya 1-2; soma pia Yohana 2:1-12; Matendo 1:12-14; 2:1-4

Rahabu

Yoshua sura ya 2, 6; soma pia Waebrania 11:30, 31; Yakobo 2:24-26

Rebeka

Mwanzo sura ya 24-27

Sara

Mwanzo sura ya 17-18, 20-21, 23; soma pia Waebrania 11:11; 1 Petro 3:1-6

Wanaume fulani wa pekee

Abrahamu

Mwanzo sura ya 11-24; soma pia 25:1-11

Daudi

1 Samweli sura ya 16-30; 2 Samweli sura ya 1-24; 1 Wafalme sura ya 1-2

Yesu

Injili ya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana

Musa

Kutoka sura ya 2-20, 24, 32-34; Hesabu sura ya 11-17, 20, 21, 27, 31; Kumbukumbu la Torati sura ya 34

Noa

Mwanzo sura ya 5-9

Paulo

Matendo sura ya 7-9, 13-28

Petro

Mathayo sura ya 4, 10, 14, 16-17, 26; Matendo sura ya 1-5, 8-12

VIFAA VYA KUSAIDIA KUJIFUNZA BIBLIA VYENYE KUTOLEWA NA MASHAHIDI WA YEHOVA

  • JW.ORG—Adresi hii ya Internete iko na vifaa vingi vya kusaidia kujifunza Biblia, kama vile sehemu “Majibu ya Maswali ya Biblia.” Iko pia na maagizo juu ya namna ya kuchukua programu ya JW Library

  • “Ona Nchi Nzuri”—Broshua hii iko na karte na picha za maeneo yenye kutajwa katika Biblia

  • Étude Perspicace des Écritures—Ni kitabu chenye buku mbili chenye kuwa na mafasirio juu ya watu, nafasi mbalimbali, na maneno fulani yenye kupatikana katika Biblia

  • “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”—Kitabu hiki cha funzo, kinafasiria ni wakati gani, mahali gani na sababu gani kila kitabu cha Biblia kiliandikwa na kinaonyesha kwa kifupi mambo yenye kuzungumuziwa katika kila kitabu

  • Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?—Kitabu hiki kidogo kinachunguza maandiko kwa uangalifu ili kutoa uhakikisho wenye kuonyesha kama Biblia ni Neno la Mungu lenye kuongozwa na roho yake

  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?—Broshua hii yenye kurasa 32 inaonyesha kwa kifupi tungo kubwa ya Biblia nzima

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine