Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 2 uku. 3
  • Wakati Inaonekana Kama Maisha Inakuwa Nguvu Kuvumilia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Inaonekana Kama Maisha Inakuwa Nguvu Kuvumilia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wakati Maisha Inakuwa Nguvu Sana Kuvumilia
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Wakati Mutu Mwenye Unapenda Anakufa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Wakati Musiba wa Asili Unatokea
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Wakati Musiba Unatokea
    Amuka!—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 2 uku. 3
Kijana mumoja mwanamuke iko analia wakati iko ku kazi

Wakati Inaonekana Kama Maisha Inakuwa Nguvu Kuvumilia

MAISHA inaweza kuwa muzuri sana wakati mambo yote inaenda muzuri. Lakini itakuwa namna gani kama hali mbalimbali zinafanya maisha yako ionekane kuwa nguvu kuvumilia?

Kwa mufano, Sally,a wa États-Unis, mwenye alipoteza sehemu kubwa ya vitu vyake wakati wa upepo mukubwa, anasema hivi: “Nilijisikia kama singeweza tena kuvumilia. Siku mingi nilijisikia kuwa nimefika ku mwisho.”

Ao, itakuwa namna gani ikiwa mupendwa wako anakufa? Janice, katika Australia, anasema hivi: “Wakati watoto wangu wawili wanaume walikufa, ilikuwa kama vile maisha yangu imevunjika vipande-vipande. Nilipaswa kufanya yote yenye ningeweza ili kuviunganisha tena. Nilimuomba Mungu hivi: ‘Tafazali, moyo wangu hauwezi tena kuvumilia! Uniache tu nilale. Sipendi tena kuamuka.’”

Daniel naye, alihuzunika sana wakati bibi yake alifanya uzinifu. Anaeleza hivi: “Wakati bibi yangu aliniambia kama amefanya uzinifu, nilijisikia kama vile kisu kimeingizwa ndani ya moyo wangu. Ile maumivu ya mwili ilinichoma tena na tena​—na ilifanya miezi mingi.”

Gazeti hili la Munara wa Mulinzi litazungumuzia namna maisha inaweza kuwa na maana hata wakati

  • Musiba wa asili unatokea

  • Mutu mwenye unapenda anakufa

  • Bibi ao bwana anakosa uaminifu

  • Uko unapambana na ugonjwa hatari

  • Maisha inakuwa nguvu kuvumilia

Kwa hiyo, tuone kwanza kile tunaweza kufanya wakati musiba wa asili unatokea.

a Majina fulani katika habari hizi zenye kufuatana imebadilishwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine