Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 2 uku. 4-5
  • Wakati Musiba wa Asili Unatokea

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Musiba wa Asili Unatokea
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUJUA KWELI YA BIBLIA KUNAFANYA MAISHA IKUWE NA MAANA
  • Uko Tayari?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Umutupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Unaweza Kufanya Nini Kama Uko na Mahangaiko?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Saidia Wengine Wavumilie Magumu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 2 uku. 4-5
Wanaume wawili wanakaa katikati ya mabomoko ya jengo fulani lenye limeharibiwa

Wakati Musiba wa Asili Unatokea

“Mwanzoni, tulijisikia wenye kuvunjika moyo sana. Kila kitu chenye tulikuwa nacho kilikuwa kimeharibiwa na matope na maji mingi ya mvua.”​—Andrew, katika Sierra Leone.

“Kisha upepo mukubwa, tulirudia ku nyumba yetu. Tulipoteza kila kitu. Hatukujua tuseme nini. Mutoto wangu mwanamuke, alipiga magoti chini na kulia.”​—David, katika îles Vierges.

IKIWA umekwisha kuokoka musiba fulani wa asili, unaweza kuelewa namna watu wengine wenye waliokoka walijisikia: kuhuzunika sana, kukataa kukubali hali, kuvurugika, kuwa na mahangaiko, na kuota ndoto zenye kuogopesha. Watu wengi wenye wanaokoka wanajisikia wenye kuchoka na wenye kuvunjika moyo sana hivi kwamba hawana hata tamaa ya kuendelea na maisha.

Ikiwa umepoteza kila kitu kwa sababu ya musiba wa asili, wewe pia unaweza kujisikia kama hautaweza tena kuvumilia. Unaweza hata kuwaza kama maisha yako haina tena maana. Lakini, Biblia inafundisha kama maisha yako iko na maana na kama unaweza kuwa na sababu za muzuri za kutumaini kwamba wakati wenye kuja utakuwa muzuri zaidi.

KUJUA KWELI YA BIBLIA KUNAFANYA MAISHA IKUWE NA MAANA

Andiko la Muhubiri 7:8 linasema hivi: “Mwisho wa jambo ni muzuri zaidi kuliko mwanzo wake.” Wakati tu uko unaanza kupona musiba fulani wa asili, unaweza kuona kama maisha yako haitakuwa tena muzuri. Lakini, wakati unatumika kwa uvumilivu ili kutengeneza tena maisha yako, mambo inaweza kuwa tena muzuri zaidi.

Biblia inatabiri wakati wenye “sauti ya kulia wala kilio cha taabu havitasikika tena.” (Isaya 65:19) Jambo hilo litafanyika wakati dunia itageuzwa kuwa paradiso chini ya Ufalme wa Mungu. (Zaburi 37:11, 29) Hakutakuwa tena misiba ya asili. Kumbukumbu yoyote ya mambo yenye kuumiza na maumivu ya kimwili na ya moyoni vitaondolewa milele, kwa sababu Mungu Mweza-Yote anaahidi hivi: “Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayataingia katika moyo.”​—Isaya 65:17.

Waza kidogo: Muumbaji amepanga ‘kukupatia wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini’​—maisha yenye amani chini ya utawala mukamilifu wa Mungu. (Yeremia 29:11) Je, kujua kweli hiyo kunaweza kufanya maisha yako ikuwe na maana? Sally, mwenye tulizungumuzia katika habari ya kwanza anasema hivi: “Kujikumbusha mambo ya muzuri sana yenye Ufalme wa Mungu utatufanyia wakati wenye kuja kunaweza kukusaidia usikazie akili mambo ya zamani na kutakusaidia uvumilie hali yako ya sasa.”

Tunakutia moyo ujifunze mingi zaidi kuhusu mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanyia wanadamu hivi karibuni. Ukifanya vile, unaweza kuwa hakika kuwa hata kama ulipatwa na musiba wa asili, maisha yako iko na maana sasa kadiri unangojea kwa hamu wakati wenye hakutakuwa misiba ya asili. Lakini kwa sasa, Biblia inatoa mashauri yenye kufaa yenye inaweza kukusaidia kuvumilia matokeo ya musiba wa asili. Fikiria mifano fulani.

Maandiko ya Biblia Yenye Inaweza Kusaidia

Ulale vya kutosha.

“Mukono mumoja wa pumuziko ni muzuri zaidi kuliko mikono mbili ya kazi ya nguvu na kufuatilia upepo.”​—Muhubiri 4:6.

Wataalamu wanaripoti kama kisha kupatwa na hali yenye kuogopesha, “kukosa kulala vya kutosha . . . kunaweza kuongeza huzuni na kufanya hisia zako zibadilike-badilike.” Kwa hiyo, ni jambo la hekima kuwa na wakati mingi ya kupumuzika.

Zungumuza na wengine kuhusu namna unajisikia.

“Mahangaiko katika moyo wa mutu yanalemea moyo [ao, “yanamufanya ashuke moyo,” maelezo ya chini], lakini neno la muzuri linauchangamusha.”​—Mezali 12:25.

Zungumuza na mutu mumoja wa familia ao rafiki mwenye unatumainia. Zaidi ya kukusikiliza, watu wa familia ao marafiki wa karibu wanaweza kukuambia maneno yenye kutia moyo na kukutolea musaada wenye kufaa.a

Ufikirie wakati wenye kuja wa muzuri zaidi.

“Kulingana na ahadi [ya Mungu] tunangojea mbingu mupya na dunia mupya, na mule haki itakaa.”​—2 Petro 3:13.

a Mutu mwenye mahangaiko yake inaendelea kwa muda murefu anaweza kuwa na lazima ya kutafuta matunzo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine