Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 2 uku. 10-11
  • Wakati Uko na Ugonjwa Hatari

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Uko na Ugonjwa Hatari
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAMBO YENYE ILISAIDIA WENGINE WAVUMILIE
  • Yehova Mungu Wako Anakuona Kuwa wa Maana!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Namna ya Kusaidia Wale Wenye Wako na Matatizo ya Akili
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • Unafarijiwa ili Uwafariji Wengine
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 2 uku. 10-11

Wakati Uko na Ugonjwa Hatari

“Wakati niliambiwa kama niko na ugonjwa wa kansere kwenye pafu (poumon) na kwenye utumbo-tumbo pana, niliwaza kama nimepewa hukumu ya kifo. Lakini, wakati nilienda ku nyumba kisha kuonana na munganga, niliwaza, ‘Sawa, sikutumainia kama mambo itakuwa vile, lakini ninapaswa kutafuta namna ya kupambana na hii hali.’”​—Linda, iko na miaka 71.

“Niko na ugonjwa wenye kuumiza sana wenye kushambulia mishipa yenye kuwa kwenye upande wa kushoto wa sura yangu. Wakati fulani, maumivu makali ilinifanya nikuwe mwenye kushuka moyo. Mara mingi, nilijisikia peke yangu na niliwaza hata kujiua.”​—Elise, iko na miaka 49.

Mwanaume mumoja mugonjwa mwenye kukaa katika kiti cha magurudumu anazungukwa na watu wenye kumupenda

IKIWA wewe ao mupendwa wako ameambiwa kama iko na ugonjwa wenye unaweza kuleta kifo, unajua namna jambo hilo linaweza kuvunja moyo. Zaidi ya ugonjwa wenyewe, unapaswa kupambana na mahangaiko ya akili kwa sababu ya hali hiyo. Programu ya kuonana na munganga yenye kuhangaisha, magumu ya kupata ao kulipia matunzo, ao matokeo ya mubaya yenye inaweza kuletwa na dawa yenye unatumia, vinaweza kukuongezea woga na wasiwasi. Mahangaiko ya akili yenye kuhusiana na ugonjwa hatari inaweza kuchokesha sana.

Ni wapi tunaweza kupata musaada? Watu wengi wametambua kama wanapata kitulizo kikubwa zaidi kwa kusali kwa Mungu na kusoma maandiko yenye kutuliza yenye kupatikana katika Biblia. Musaada mwingine tunaweza kuupata kupitia watu wa familia na marafiki wenye upendo na wenye wanaweza kututegemeza.

MAMBO YENYE ILISAIDIA WENGINE WAVUMILIE

Robert mwenye kuwa na miaka 58, alishauri hivi: “Ukuwe na imani katika Mungu na atakusaidia kuvumilia ugonjwa wako. Sali kwa Yehova. Umuambie namna unajisikia. Umuombe roho takatifu. Umuombe akusaidie ukuwe na mawazo ya muzuri na ukuwe mwenye kutia moyo watu wa familia na uvumilie ugonjwa wako ukiwa mwenye kutulia.

“Wakati watu wa familia yako wako pale kwa ajili yako na wakati wanakutia moyo, ile inasaidiaka sana. Kila siku, mutu mumoja ao watu wawili wa familia yangu wananiita ku telefone na kuniuliza, ‘Unaendelea je?’ Marafiki wangu wenye kuishi sehemu mbalimbali wananitia moyo. Wananifanya nijisikie muzuri zaidi, na ile inanisaidia nivumilie.”

Ikiwa unatembelea rafiki yako mwenye ni mugonjwa, fikiria jambo lenye Linda anasema: “Bila shaka mugonjwa anapendaka kuishi maisha ya kawaida kadiri inawezekana na hawezi kupenda kila mara kuzungumuzia magonjwa yake. Kwa hiyo, uzungumuzie mambo yenye unazoea kuzungumuzia.”

Kupitia nguvu yenye kutoka kwa Mungu na kitulizo kutoka katika Maandiko, na pia kupitia musaada wenye upendo wa watu wa familia na marafiki, tunaweza kuwa hakika kama maisha ni ya maana, hata wakati tunapambana na ugonjwa hatari.

Maandiko ya Biblia Yenye Inaweza Kusaidia

Umutegemee Mungu.

“Nilimuuliza Yehova, na akanijibu. Aliniokoa katika mambo yote yenye kuniogopesha. Mutu huyu wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia.”​—Zaburi 34:4, 6.

Linda, mwenye tumezungumuzia anasema hivi: “Sikuwake ninasali hivi, ‘Unifanye nijisikie muzuri zaidi.’ Ninazoea kusali, ‘Unisaidie nikuwe nguvu, na unisaidie nivumilie ugonjwa wangu.’”

Usome Neno la Mungu ili kuwa mwenye nguvu.

“Hakuna mukaaji mwenye atasema: ‘Niko mugonjwa.’”​—Isaya 33:24.

Uwaze sana juu ya ahadi za Mungu kuhusu wakati wenye kuja. Ile itakupatia tumaini, jambo lenye linaweza kukupatia nguvu ya kuvumilia.

Uombe watu wa familia na marafiki wakusaidie.

“Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.”​—Mezali 17:17.

Elise mwenye tulizungumuzia, anashauria hivi: “Usijitenge na wengine. Ruhusu marafiki wako wakusaidie. Kunaweza kuwa wakati wenye unaweza kujisikia kuwa peke yako na wakati wenye unaweza hata kuwaza kama Mungu hakusikilize, lakini usijitenge na wengine.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine