Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w19 Mwezi wa 1 uku. 31
  • Ndugu Mupya wa Baraza Lenye Kuongoza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ndugu Mupya wa Baraza Lenye Kuongoza
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mushiriki Mupya wa Baraza Linaloongoza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Ndugu Wawili Wapya wa Baraza Yenye Kuongoza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova Ni Nini?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Je, Unaweza Kujitoa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
w19 Mwezi wa 1 uku. 31
Kenneth Cook na Jamie

Kenneth Cook, na bibi yake, Jamie

Ndugu Mupya wa Baraza Lenye Kuongoza

ASUBUI ya Siku ya Tatu tarehe 24 Mwezi wa 1, 2018, ndugu na dada wa familia ya Beteli ya inchi ya Amerika na ya Kanada walifurahi kusikia tangazo hili la pekee: Ndugu Kenneth Cook, ameongezwa mu Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova.

Ndugu Cook alizaliwa na kukomalia katika Pennsylvania, Amerika. Alijifunza kweli kupitia mwanafunzi mwenzake mbele tu ya kumaliza masomo ya segondere na alibatizwa tarehe 7 Mwezi wa 6, 1980. Alianza utumishi wa wakati wote wa upainia tarehe 1 Mwezi wa 9, 1982. Kisha kufanya kazi ya upainia kwa miaka mbili, alialikwa ku Beteli, kwa hiyo, alianza kutumikia ku Beteli ya Wallkill, New York, tarehe 12 Mwezi wa 10, 1984.

Kwa miaka 25 yenye ilifuata, Ndugu Cook alitumika katika migao mbalimbali kutia ndani kazi ya uchapishaji na kutumika mu Biro ya Beteli. Alioa bibi yake, Jamie, mu mwaka wa 1996, na Jamie alijiunga naye katika utumishi wa Beteli katika Wallkill. Katika Mwezi wa 12, 2009, Ndugu Cook na bibi yake walitumwa Mahali pa Elimu ya Watchtower katika Patterson, New York, kwenye Ndugu Cook alipewa mugao wa kutumika mu Idara ya Kushugulikia Maulizo ya Wasomaji. Kisha Ndugu Cook na bibi yake kurudia kwa muda mufupi ku Beteli ya Wallkill, walitumwa Brooklyn, New York katika Mwezi wa 4, 2016. Kisha miezi tano, walihamia kwenye makao yetu makubwa katika Warwick, New York. Katika Mwezi wa 1, 2017, Ndugu Cook aliwekwa kuwa musaidizi mu Halmashauri ya Uandikaji ya Baraza Lenye Kuongoza.

Sasa Baraza Lenye Kuongoza Liko na ndugu 8 watiwa-mafuta:

Kenneth Cook; Samuel Frederick Herd; Geoffrey William Jackson; Mark Stephen Lett; Gerrit Lösch; Anthony Morris III; Douglas Mark Sanderson; David Howard Splane

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine