Kufaidika Na Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 1996 — Sehemu Ya 1
1 Je! umeyasoma maagizo yanayopatikana katika “programu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1996”? Je! umeyaona mabadiliko fulani? Kutoka Januari hadi Aprili, hotuba Na. 3 itategemea kitabu Kutoa Sababu, na kutoka Mei hadi Desemba, kitabu kipya Ujuzi. Hotuba Na. 4 itazungumzia mtu tofauti wa kibiblia kila juma.
2 Hotuba za Wanafunzi: Hotuba Na. 3 inapewa dada fulani. Inapotegemea kitabu Kutoa Sababu, kikao kinapaswa kuambatana na hali zinazotukia katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba au ushuhuda wa vivi hivi. Wakati habari zinapochukuliwa katika kitabu Ujuzi, hotuba inapaswa kutolewa kana kwamba ni ziara ya kurudia au funzo la Biblia. Jambo hilo lapaswa kuwa lenye mafaa sana, kwa kuwa kitabu Ujuzi kitatumiwa sana katika kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
3 Ikiwa kikao kilichochaguliwa ni funzo la Biblia, akina dada wawili waweza kukaa. Bila kukawia ingia katika habari kisha tu maelezo mafupi ya utangulizi, baadaye uulize maulizo yaliyochapwa katika kitabu. Msikilizaji atapaswa kutimiza sehemu yake kwa kufanya mambo yawe ya kweli. Wakati ukiruhusu maandiko yanayotajwa yaweza kuchukuliwa katika Biblia na kusomwa. Dada anayetoa habari hii anapaswa kuonyesha ufundi wa kufundisha kwa kumvuta msikilizaji wake ili aongee kwa njia ya maulizo na kwa kumfanya apate sababu kwa msingi wa maandiko yanayotumiwa.
4 Ifanyweje ikiwa habari zinayo maandiko mengi yanayotolewa na kwamba isiwezekane kuyachunguza yote kwa dakika tano? Chagua maandiko yanayokazia mambo makuu ya lazima. Ikiwa kuna maandiko machache mambo makuu ya lazima yanaweza kufasiriwa zaidi. Mara kwa mara, unaweza kusoma fungu au sentesi ya kitabu na kuzungumza na msikilizaji wako.
5 Wakati habari unazogawiwa zinatia ndani fungu la mwisho la mojawapo wa sura ya kitabu Ujuzi, unaweza kuchunguza kwa kifupi kisanduku kiitwacho “Tahini Ujuzi Wako” kinachopatikana mwishoni. Visanduku vinavyoongezwa kati ya mafungu yaliyogawiwa vinaweza pia kuchunguzwa ikiwa wakati waruhusu. Ikiwa kisanduku kinapatikana kati ya sehemu mbili zinazochunguzwa na akina dada tofauti, yule anayechunguza sehemu ya kwanza aweza kuongea juu yacho. Picha za kitabu zaweza kufanyiwa maelezo kila mara zinapoambatana na habari zinazochunguzwa.
6 Hotuba Na. 4 yapaswa kutolewa kwa namna yenye kupendeza sana na kuipatanisha na hali za maisha. Kila juma tutazungumzia mtu mmoja wa kibiblia. Tuchunguze kwa uangalifu yale kitabu Auxiliaire kinatufunza juu ya mtu huyo. Hotuba ifasiriwe kulingana na kichwa cha habari, pia tuchague maandiko ya Biblia yatakayosaidia wasikilizaji kukazia fikira zao juu ya mtu huyo wa kibiblia na pia juu ya utu wake, kutia ndani alama za tabia au mielekeo ambayo tungeiga au kutupilia mbali. Tunaweza kutaja maandiko yasiyoambatana moja kwa moja na mtu huyo ikiwa yanakazia wazi namna Yehova anavyoona alama fulani za tabia, nzuri au mbaya, au ikiwa yanapatana na kichwa cha hotuba.
7 Sisi tukifaidika kabisa na mazoezi ambayo tunapata kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, tutazidi kuwa na uwezo wa ‘kuhubiri lile neno’ kwa kufanya yote tuwezayo katika ‘ufundi wa kufundisha.’—2 Tim. 4:2.