Michango Kwa Ajili Ya Kazi Ya Ulimwenguni Pote Ya Sosaiti Inategemeza Mpanuko
Kama ilivyotabiriwa na Isaya 54:2, 3, ibada safi ya Yehova inaendelea kupanuka kokote duniani. Ndivyo ilivyo hasa katika nchi mbalimbali za bara la Afrika, na pia katika visiwa fulani kando-kando. Mnamo miaka kumi ya nyuma, vizuizi vilivyokuwa vimewekewa utendaji wa Ufalme viliondolewa katika nchi kama vile Angola, Kameruni, Ithiopia, Gini ya Ekwatori, Madagaska, Malawi, Musumbiji na Togo. Katika nchi hizo na pia katika nyingine ambako mashamba ni meupe kwa ajili ya mavuno, kulitumwa wamishonari wa Gileadi, wahitimu wa Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, wanamemba wa Betheli na wahubiri wengine.—Mt. 9:37, 38.
Ni wazi kwamba ongezeko la hesabu ya watendaji wa ibada ya kweli katika tengenezo la Yehova linaomba ujenzi wa mamia ya Majumba ya Ufalme. Linakuwa pia jambo la lazima kujenga Majumba ya makusanyiko na kujenga au kupanua matawi. Sehemu kubwa ya michango inayotolewa kwa Sosaiti kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote inatumiwa kwa ajili ya kulipia miradi hiyo, na pia kwa ajili ya kuendeleza kazi ya Ufalme si tu katika Afrika, lakini pia katika sehemu nyingine za ulimwengu.
Picha na michoro inayopatikana kwenye kurasa mbili za nyongeza hii inatutolea wazo la yale Sosaiti inajikaza kufanya kwa ajili ya Afrika. Kuna hapa majengo fulani fulani yanayoendelea na miradi fulani ambayo itaanzishwa hivi karibuni.
Kwa kuchunguza ripoti ya ulimwengu katika Kitabu-Mwaka 1996, utapata wazo kamili zaidi la huduma ambayo wahubiri wanatimiza katika nchi hizo. Nchi nyingi zinapata ongezeko la ajabu, na hudhurio kubwa kwenye Ukumbusho linaonyesha matarajio mazuri ya ongezeko. Tunapofikiria yale ambayo kazi ya kuhubiri na utendaji unaohusu kufanya wanafunzi unawezesha kutimiza katika mabara mengine, tunaelewa ni pendeleo kama nini tulilo nalo la kutegemeza sababu ya ibada ya kweli kwa upande wa kimwili.—Lk. 16:9; 1 Tim. 6:18.
[Captions on page 3]
Jumba la Ufalme lililojengwa muda wa siku 9 katika KwaZulu-Natal, Afrika ya Kusini.
Jumba la Ufalme la bei ya chini, Nigeria.
Katika Musumbiji, Jumba la Makusanyiko lenye nafasi za kukaa 1,500, karibu na kumalizika mwishoni mwa 1996.
Majengo ya tawi la Musumbiji ambayo yatatumiwa kuanzia masika ya 1996.
Tawi la Sierra Leone, ambalo linapaswa kumalizwa katika kiangazi hiki.
[Captions on page 4]
Morisho: Jumba la Makusanyiko lililomalizwa, lenye kufunguliwa ubavuni, na majengo ya tawi yatakayomalizika katika majira ya chipukizi 1997.
Tawi la Zimbabwe, katika ujenzi.
Jumba la makusanyiko lenye kufunguliwa ubavuni
na tawi lenye kujengwa katika Senegali.
Tawi jipya katika Kenya pa Nairobi, mji mkuu.
Tawi la Madagaska, karibuni kumalizika.
Mradi wa tawi kwa ajili ya Malawi.