Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/96 uku. 6
  • “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ujuzi Utokao Kwa Mungu Unajibu Kwa Maulizo Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Tuingize Katika Wengine Tumaini La Uhai Wa Milele
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 12/96 uku. 6

“Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”

1 Maneno ya Yesu yanayoripotiwa katika Yohana 17:3 ni ya kuchukua kwa uzito. Yanasema vizuri yale yanayotaka kusema: kutwaa ujuzi juu ya Mungu na Kristo kunamaanisha uhai udumuo milele! Lakini je! inatosha tu kuwajua Yehova na Yesu ili kupokea zawadi kama hiyo? Hapana. Waisraeli walijua kwamba Yehova alikuwa Mungu wao, lakini namna yao ya kuishi ilikuwa ikikanusha imani yao. Hivyo, wakapoteza upendeleo wa kimungu. (Hosea 4:​1, 2, 6) Leo, mamilioni ya watu labda wana “bidii kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi.” (Rom. 10:​2, TUM) Inafaa wafikie kumjua Yehova, yule “Mungu pekee wa kweli,” na kujua jinsi ya kumtumikia ifaavyo. Katika kusudi hilo, tutatolea mnamo Desemba kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Tutafanya hivyo namna gani? Madokezo fulani yafuatayo yataweza kuwa ya lazima kwetu.

2 Kwa kuwa wazo la kuishi milele duniani halizoelewi na watu wengi, utangulizi huu ungeweza kuvutia uangalifu wao:

◼ “Tunauliza ulizo moja tu kwa majirani zetu. Ikiwa wangekualika kuishi milele katika ulimwengu kama huu, je! ungekubali mwaliko? [Tuonyeshe picha ya kurasa 4-5 ya kitabu Ujuzi. Tusikilize jibu.] Maisha haya yenye furaha yanatolewa kwako. Lakini kwa maoni yako, nini ungeweza kufanya ili kufaidika nayo? [Tuache mtu ajibu.] Angalia yale tunayoombwa katika Yohana 17:3. [Tusome andiko hilo.] Kitabu hiki kinasaidia watu wengi kutwaa ujuzi huo wa pekee. Je! ungependa kupata nakala moja yacho? [Tusikilize jibu.] Wakati wa ziara yangu ijayo, nitakuonyesha kwa nini ni jambo la akili kuamini kwamba tunaweza kuishi milele hapa hapa duniani.”

 3 Tunaporudi kuwaona wale ambao tulizungumza nao Yohana 17:​3, tunaweza kuanza hivi:

◼ “Mara ya mwisho, nilikusomea maneno yanayoonekana kuwa ya ajabu ya Yesu yanayopatikana katika Yohana 17:​3, ambako anatuhakikishia kwamba kujifunza kuwajua, yeye na Baba yake, kunamaanisha uhai udumuo milele. Lakini watu wengi wanaamini kwamba ni mbinguni tu ambako maisha mazuri yanatungoja. Wewe unawaza nini? [Tusikilize jibu.] Ikiwa una kitabu ambacho nilikuachia karibu nawe, ningependa kukuonyesha maandiko fulani ya Biblia yanayoonyesha kwamba Paradiso itarudishwa duniani. [Tuzungumzie mafungu 11-16 ya kitabu Ujuzi.] Kwa wakati mwingine, ningependa kukuonyesha kwa nini unaweza kutumainia hakika katika ahadi za Biblia. Kwa kungoja wakati huo, labda ungependa kusoma sura ya 2 katika kitabu chako?”

 4 Tazama utoaji ambao ungeweza kuwa wenye kufaa ikiwa tunakutana na mtu anayeamini:

◼ “Tunazungumza na majirani zetu juu ya sababu zinazofanya kuwe na dini nyingi tofauti ulimwenguni. Katika Shirikisho ya Amerika yenyewe, kuna vikundi vya kidini yapata 1,200 na kuna zaidi ya dini 10,000 katika nchi zote za dunia. Ijapokuwa hivyo, kuna Biblia moja tu. Namna gani wewe unafasiria uwingi huo wa dini? [Tungoje jibu. Tufungue kitabu Ujuzi kwenye sura ya 5 na tusome fungu 1.] Utapata majibu yenye kuridhisha kwa maulizo hayo kwa kusoma sura hiyo. Ningefurahi kukuachia kitabu hiki ikiwa unapendezwa kukichunguza.” Ikiwa msikilizaji wetu anakubali, tupange siku kamili ya kukutana na tumalize kwa kusema: “Mara ijayo, tutaweza kwa mfano kuona ikiwa dini zote ni njia tu mbalimbali zinazoongoza mahali pamoja.”

 5 Tunaporudi kuendeleza mazungumzo juu ya sababu zinazofanya kuwe na dini nyingi, tunaweza kusema:

◼ “Mara ya mwisho tulipoonana, nilitokeza ulizo la kujua ikiwa dini zote hazikuwa hatimaye njia mbalimbali zinazoongoza kwenye kusudi moja. Wewe unafikiri nini? [Tusikilize jibu.] Ningependa kukuonyesha katika kitabu nilichokuachia yale Yesu alisema kuhusu ulizo hilo. [Tufungue kitabu Ujuzi kwenye sura 5 na tusome mafungu 6-7 mahali ambapo Mathayo 7:​21-23 inanukuliwa.] Unajiuliza labda kwa nini ni jambo la lazima kujua kwa usahihi mapenzi ya Mungu. Utaona kwamba mafungu yafuatayo ni yenye kuelimisha. Soma sehemu inayobaki ya sura hiyo, ikiwa unapenda; na wakati wa ziara yangu ijayo, ningefurahi kukuonyesha thamani yote ya ujuzi sahihi wa Biblia.”

 6 Utangulizi wa moja kwa moja mara nyingi ni wenye matokeo ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Utangulizi unaofuata umechukuliwa kwenye ukurasa wa 10 wa kitabu “Kutoa Sababu”:

◼ “Ninakuzuru [kutembelea] ili nikutolee mtaala wa Biblia nyumbani bila malipo. Ukitaka, ningependa kuchukua dakika chache tu nionyeshe jinsi watu katika nchi kama 200 wanavyozungumza Biblia nyumbani wakiwa vikundi vya jamaa. Tunaweza kutumia vichwa vyo vyote kati ya hivi viwe msingi wa mazungumzo yetu. (Onyesha mambo yaliyomo katika kitabu cha funzo.) Ni kichwa kipi hasa kinachokupendeza?” Tuache mtu afanye uchaguzi wake. Tufungue kitabu kwenye sura inayompendeza na tuanzishe funzo kwa kuanzia fungu la kwanza.

 7  Tazama ufundi mwingine wa moja kwa moja ambao tungeweza kujaribu ili kuanzisha mafunzo:

◼ “Ninatoa mafunzo ya Kibiblia kwa bure na bado ningali nafasi katika matumizi yangu ya wakati kwa ajili ya wanafunzi wa ziada. Ninatumia kitabu hiki. [Tuonyeshe kitabu Ujuzi.] Masomo yanadumu miezi fulani tu na yanatoa majibu kwa maulizo kama vile: Sababu gani Mungu huruhusu kuteseka? Sababu gani tunazeeka na kufa? Inakuwaje kwa wapendwa wetu waliokufa? Au tena: Jinsi gani unavyoweza kumkaribia Mungu?” Tuulize baadaye: “Je! ninaweza kukufanyia onyesho la namna inavyofanyika?” Ikiwa mtu hapendezwi na funzo, tumuulize ikiwa angependa kuwa na kitabu Ujuzi ili kukisoma peke yake. Ikiwa anasema kwamba atakisoma, tumtolee nakala moja na tumuonyeshe bei yacho kwa sasa.

 8 Ni hazina kama nini aliyo nayo yule aliye na ujuzi sahihi wa Mungu na Kristo! Kujifunza kuwajua kunamaanisha hakika uhai udumuo milele katika hali kamilifu. Mnamo mwezi wa Desemba, tuchukue nafasi zote za kutangazia wengine ujuzi uongozao kwenye uhai huo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine