Ujuzi Utokao Kwa Mungu Unajibu Kwa Maulizo Mengi
1 Kabla ya kupata ujuzi sahihi wa ukweli, tulikuwa tukijiuliza bila shaka maulizo mengi juu ya uhai, bila kuwa na uwezo wa kuyajibu. Ni shangwe kama nini, sasa, kupokea majibu yanayotegemea Biblia! Leo, tunao uwezo wa kuwasaidia wengine kupata majibu hayohayo. (Ona 2 Timotheo 2:2.) Tunaweza kushiriki pamoja nao ujuzi wa Mungu uongozao kwenye uhai udumuo milele. (Yn 17:3) Lakini jinsi gani kumsaidia mtu fulani kuona ubora wa thamani ya ujuzi huo? Ni kwa kufikiri tu kwa majibu ambayo sisi wenyewe tulipokea kwa msaada wa ukweli. Tukiwa na wazo hilo kichwani, itakuwa rahisi kwetu kutolea kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Madokezo yanayotolewa hapo chini yataweza kutusaidia kujitayarisha kwa ajili ya mahubiri mnamo Julai.
2 Kwa kuwa watu wengi wanajiuliza kwa nini kuna mateso mengi ulimwenguni, ufundi ufuatao ungeweza kutokeza kuitikia mbalimbali kwenye kupendeza:
◼ “Wakati msiba unapotokea au kwamba matendo ya jeuri na mashambulizi yanapoongezeka, watu wanajiuliza mara nyingi namna gani mambo kama hayo yanaweza kutokea. Ni mafasirio gani ungeweza kutoa?” Tusikilize kwa makini jibu, kisha tufungue kitabu Ujuzi kwenye sura 8 na tuonyeshe yale yanayosemwa kwenye fungu 2. Tukazie kwamba kitabu hicho kinatoa mafasirio ya Biblia kuhusu kuwapo kwa ubaya, na tuongeze: “Ikiwa unaniahidi kukisoma, ningefurahi kukuachia chenyewe.” Ikiwa mtu anaitikia vizuri, tumtolea kitabu kwa mchango (bei) wa sasa.
3 Tunapomtembelea upya mwanamume au mwanamke ambaye tuliachia kitabu “Ujuzi,” tungeweza kusema:
◼ “Ningependezwa kujua ni neno la mwisho gani umefikia juu ya sababu kwa hiyo mateso yanaenea ulimwenguni. Je! unakubaliana na jibu ambalo Biblia inatoa na linaloonyeshwa katika kitabu hiki?” Tuache mtu ajibu. Tusome fungu 17 kwenye ukurasa 77 wa kitabu Ujuzi na tumuombe kusoma Warumi 9:14 katika Biblia yake mwenyewe. Kisha tuseme: “Habari njema, ni kwamba Yehova hatutesi kwa vyovyote kwa udhalimu. Aliahidi kututolea uhai wa milele katika amani na furaha. Sura ya kwanza ya kitabu hiki ni yenye kichwa ‘Unaweza Kuwa na Wakati Ujao Wenye Furaha!’ Ningependa kukufasiria jinsi hilo linawezekana kwako na kwa wale upendao.” Tuchukua sura ya 1 na tuonyeshe ufundi wetu wa funzo. Tumalize mafungo kadha ya sura hiyo kwa kadiri hali zinavyoruhusu.
4 Tutachagua labda kutumia utangulizi unaopatikana kwenye ukurasa 13 wa kitabu “Kutoa Sababu” chini ya kichwa kidogo “Uzee/Kifo”:
◼ “Je! haujawai kujiuliza kamwe kwa nini tunazeeka na tunakufa? [Tuache mtu aseme.] Maandiko yanajibu kwa maulizo yote ambayo tungeweza kujiuliza kuhusu habari hiyo. [Tusome Muhibiri 9:5, 10.] Yanaonyesha pia kwamba kuna tumaini hakika kwa wale wanaojizoeza imani. [Tuchukue fungu 13 la ukurasa 84 wa kitabu Ujuzi; tusome na tufasirie maneno ya Yesu yanayopatikana katika Yohana 11:25.] Sura yote ina kusudi la kujibu kwenye ulizo: ‘Inakuwaje kwa Wapendwa Wetu Waliokufa?’ Ikiwa unapenda kuisoma, ninaweza kukuachia nakala hii.” Tumuonyeshe mtu mchango (bei) wa sasa.
5 Wakati wa ziara ya kurudia, tungeweza kuanzisha upya mazungumzo, kisha kusema:
◼ “Ile siku nyingine, tulizungumza juu ya kile kinachotukia wakati wa kifo. Watu wengi wanaamini kwamba ikiwa kuna uzima baada ya kifo, ni au mbinguni, au katika jehanumu. Lakini je! umekwisha kufikiria uwezekano wa kwamba wafu warudi tena hapa hapa duniani? [Tuache mtu ajibu.] Kulingana na Biblia, wafufuliwa watakuwa sehemu ya wanyenyekevu watakaorithi dunia. [Tusome Zaburi 37:11, 29, kisha tueleze fungu 20 kwenye ukurasa 88 wa kitabu Ujuzi.] Tumaini hilo lilituliza mamilioni ya watu walioishi katika woga wa kifo. Kitabu hiki kitakusaidia kuelewa vizuri zaidi ulizo hilo. Je! unaniruhusu nikuonyesha jinsi gani?”
6 Ikiwa tunapendelea utoaji mwepesi zaidi, tungeweza kujaribu huu:
◼ “Ningependa kukuonyesha picha moja ya kitabu hiki, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Je! hauoni kwamba ni picha nzuri?” Tufungue kitabu ili kwamba mtu aweze kuona kurasa 4 na 5. Tumuache ajibu, kisha tusome kisanduku cha ukurasa wa 5. Tumalizie hivi: “Ninapenda kukuachia kitabu hiki ili kwamba ukisome wewe mwenyewe.” Tuonyeshe mtu mchango wa sasa. Ikiwa mtu alionyesha kupendezwa, tumuulize ni wakati gani tungeweza kumtembelea tena.
7 Tuna ujuzi unaotoka kwa Mungu, ujuzi unaojibu maulizo mengi ya maana yanayogusa maisha yetu. Tujitayarishe kwa makini na Yehova atabariki bidii ambayo tutafanya ili kutangaza ujumbe huu wa lazima kwa watu wanaotafuta ukweli.