Jinsi ya Kutolea Watu Kitabu Biblia Inafundisha
Nyongeza hii inatia ndani mapendekezo mbalimbali ili kutolea watu kitabu Biblia Inafundisha. Ili uwe mwenye matokeo zaidi, yatumie katika maneno yako mwenyewe, patanisha utoaji wako na hali ya watu walio katika eneo lenu, na ujue vizuri mambo kamili yaliyo katika kitabu yanayoweza kutumiwa kama msingi wa mazungumzo ya Kibiblia. Utoaji mwingine mbalimbali wenye matokeo katika eneo lenu unaweza pia kutumiwa.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, uku. 8.
Har-Magedoni
◼ “Watu wanaposikia neno ‘Har-Magedoni,’ wengi wanafikiria uharibifu wa mambo yote kwa jumla. Je, ingekushangaza kusikia kwamba Har-Magedoni ni jambo fulani la kutazamia kwa furaha? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Ufunuo 16:14, 16.] Ona maelezo haya kuhusu jinsi maisha yatakavyokuwa baada ya Har-Magedoni.” Fungua kwenye ukurasa wa 82-84, na soma fungu la 21.
Biblia
◼ “Kwa kawaida watu wanasema kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Je, umepata kujiuliza namna gani kitabu kilichoandikwa na wanadamu kingeweza kuitwa kwa kufaa kuwa ni Neno la Mungu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 2 Petro 1:21 na fungu la 5 kwenye ukurasa wa 19-20.] Kitabu hiki kinatoa majibu ya Biblia kwa maulizo hayo.” Onyesha ulizo kwenye ukurasa wa 6.
◼ “Siku hizi, watu wanapata habari nyingi kuliko wakati wowote wa mbele. Lakini, wewe unafikiri tunaweza kupata wapi mashauri bora yanayoweza kutusaidia kuishi maisha yenye furaha na yenye mafanikio? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:16, 17 na fungu la 12 kwenye ukurasa wa 23.] Kitabu hiki kinaeleza jinsi tunavyoweza kuishi katika njia inayofurahisha Mungu na yenye kutufaidi.” Onyesha kisanduku na picha kwenye ukurasa wa 122-123.
Kifo/Ufufuo
◼ “Watu wengi wanajiuliza ni jambo gani hasa linalotokea mtu anapokufa. Je, unafikiri tunaweza kujua jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mhubiri 9:5 na fungu la 5-6 kwenye ukurasa wa 58-59.] Kitabu hiki kinaeleza pia kile ambacho ahadi ya Biblia kuhusu ufufuo itamaanisha kwa watu waliokuwa wamekufa.” Onyesha picha kwenye ukurasa wa 75.
◼ “Mtu fulani tumpendaye anapokufa, ni jambo la kawaida kutaka kumwona tena mtu huyo. Je, haukubaliani na hilo? [Acha mtu ajibu.] Watu wengi wamepata faraja au kitulizo katika ahadi ya Biblia kuhusu ufufuo. [Soma Yohana 5:28, 29 na fungu la 16-17 kwenye ukurasa wa 71-72.] Sura hii inajibu pia maulizo haya.” Onyesha maulizo ya utangulizi kwenye ukurasa wa 66.
Uzima wa Milele
◼ “Karibu watu wote wanatamani afya njema na maisha marefu. Lakini ikiwa jambo hilo lingewezekana, je, ungetaka kuishi milele? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Ufunuo 21:3, 4 na fungu la 17 kwenye ukurasa wa 54.] Kitabu hiki kinazungumzia jinsi tunavyoweza kupata uzima wa milele na jinsi maisha yatakavyokuwa ahadi hii itakapotimia.”
Familia
◼ “Sisi wote tunafurahia kuwa na maisha ya familia yenye furaha. Je, unakubaliana na jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Biblia inasemea jambo fulani ambalo kila mtu anaweza kufanya katika familia ili kuleta furaha katika familia—kuiga Mungu katika kuonyesha upendo.” Soma Waefeso 5:1, 2 na fungu la 4 kwenye ukurasa wa 135.
Makao
◼ “Mahali pengi, imekuwa vigumu kupata nyumba yenye kufaa iliyo ya bei chini. Je, unafikiri kwamba siku moja kila mtu atakuwa na nyumba yenye kufaa? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Isaya 65:21, 22 na fungu la 20 kwenye ukurasa wa 34.] Kichapo hiki kinaeleza jinsi ahadi hii kutoka kwa Mungu itakavyotimizwa.”
Yehova Mungu
◼ “Watu wengi wenye kuamini Mungu wangependa kujisikia kuwa karibu zaidi naye. Je, unajua kwamba Biblia inatualika tumkaribie Mungu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yakobo 4:8a na fungu la 20 kwenye ukurasa wa 16.] Kitabu hiki kimetayarishwa ili kusaidia watu wajifunze mengi zaidi kuhusu Mungu, kwa kutumia Biblia yao wenyewe.” Onyesha maulizo ya utangulizi kwenye ukurasa wa 8.
◼ “Watu wengi wanasali ili jina la Mungu litakaswe, au litukuzwe. Je, umepata kujiuliza jina hilo ni gani? [Acha mtu ajibu. Kisha soma zaburi 83:18 na fungu la 2-3 kwenye ukurasa wa 195.] Kitabu hiki kinaeleza yale ambayo Biblia inafundisha hasa kuhusu Yehova Mungu na kusudi lake kwa wanadamu.”
Yesu Kristo
◼ “Duniani pote watu wamepata kusikia kuhusu Yesu Kristo. Watu fulani wanasema kwamba Yesu alikuwa tu mtu wa ajabu. Wengine wanamwabudu kama Mungu Mweza Yote. Je, unafikiri kwamba mambo tunayoamini kuhusu Yesu ni ya maana?” [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yohana 17:3 na fungu la 3 kwenye ukurasa wa 37-38.] Vutia uangalifu kwenye maulizo ya utangulizi yaliyo chini ya kichwa cha sura.
Sala
◼ “Je, umepata kujiuliza namna Mungu anavyojibu sala? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 1 Yohana 5:14, 15 na fungu la 16-18 kwenye ukurasa wa 170-172.] Sura hii inaeleza pia kwa nini tunapaswa kusali Mungu na yale tunayopaswa kufanya ili atusikilize.”
Dini
◼ “Watu wengi wanaanza kuona dini za ulimwengu kuwa chanzo cha matatizo ya wanadamu badala ya kuwa suluhisho. Je, unafikiri kwamba dini ni yenye kuongoza watu katika njia iliyo nzuri? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mathayo 7:13, 14 na fungu la 5 kwenye ukurasa wa 145-146.] Sura hii inazungumzia sehemu sita zenye kutambulisha ibada ambayo Mungu anakubali.” Onyesha orodha kwenye ukurasa wa 147.
Misiba/Kuteseka
◼ “Msiba unapotokea, watu wengi wanajiuliza ikiwa Mungu anajali kweli wanadamu na ikiwa anaona kuteseka kwao. Je, umepata kujiuliza kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 1 Petro 5:7 na fungu la 11 kwenye ukurasa wa 11.] Kitabu hiki kinaeleza jinsi Mungu atakavyokomesha kabisa kuteseka kwa wanadamu.” Onyesha maulizo ya utangulizi kwenye ukurasa wa 106.
Vita/Amani
◼ “Kila mahali watu wanatamani sana amani. Je, unafikiri kwamba tumaini la amani duniani ni ndoto tu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 46:8, 9.] Kitabu hiki kinazungumzia jinsi Mungu atakavyotimiza kusudi lake na kuleta amani duniani kote.” Onyesha picha kwenye ukurasa wa 35, na kuzungumzia fungu la 17-21 kwenye ukurasa wa 34.
[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 5]
Namna Mbalimbali za Kuzungumzia Mpango Kuhusu Michango
“Ukipenda kutoa mchango mdogo leo kwa ajili ya kazi yetu ya ulimwenguni pote, nitafurahi kuukubali.”
“Ingawa vichapo vyetu vinatolewa bila malipo, tunakubali michango ya kiasi kwa ajili ya kazi yetu ya ulimwenguni pote.”
“Huenda ukajiuliza jinsi gani tunafikia kutimiza kazi hii. Kazi yetu ya ulimwenguni pote inategemezwa na michango ya kujipendea. Ikiwa unataka kutoa mchango mdogo leo nitafurahi kuukubali.”