(1) Kutumia Maulizo, (2) Andiko, na (3) Sura Ili Kuanzisha Funzo
Njia rahisi ya kutolea watu kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? ni (1) kutokeza ulizo la maoni, (2) kusoma andiko moja lenye kufaa, na (3) kutaja sura moja katika kitabu, ambayo inazungumzia habari hiyo kwa kusoma maulizo ya utangulizi chini ya kichwa cha sura. Ikiwa mwenye nyumba anaonyesha kupendezwa, unaweza kumwonyesha namna ya kujifunza Biblia ukitumia mafungu ya kwanza ya sura hiyo. Njia hii inaweza kutumiwa ili kuanzisha funzo tunapofanya ziara ya kwanza au ziara ya kurudia.
◼ “Je, unafikiri kwamba inawezekana kwa wanadamu wafikie kumjua Muumba wetu mweza yote, kama inavyosemwa hapa katika Biblia?” Soma Matendo 17:26, 27, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 1.
◼ “Kulingana na matatizo tunayopambana nayo leo, je, unafikiri kwamba inawezekana kupata kitulizo na tumaini kama inavyoelezwa hapa?” Soma Waroma 15:4, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 2.
◼ “Je, ungeleta mabadiliko yanayozungumziwa hapa ikiwa wewe ulikuwa na uwezo wa kufanya hivyo?” Soma Ufunuo 21:4, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 3.
◼ “Je, unafikiri kwamba watoto wetu wataweza kufurahia wakati wowote hali zilizoelezwa katika wimbo huu wa zamani?” Soma Zaburi 37:10, 11, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 3.
◼ “Je, unafikiri kwamba kutakuwa na siku ambapo maneno haya yatapata kutimizwa?” Soma Isaya 33:24, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 3.
◼ “Je, umepata kujiuliza wakati wowote ikiwa wafu wanajua mambo ambayo walio hai wanafanya?” Acha mtu ajibu. Kisha soma Mhubiri 9:5, na kazia sura ya 6.
◼ “Je, unafikiri kwamba itawezekana siku moja tuone tena wapendwa wetu waliokufa, kama Yesu alivyosema katika maandiko haya?” Soma Yohana 5:28, 29, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 7.
◼ “Kwa maoni yako, itawezekanaje mapenzi ya Mungu yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni, kama inavyoonyeshwa katika sala hii yenye kujulikana sana?” Soma Mathayo 6:9, 10, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 8.
◼ “Je, unafikiri kwamba tunaishi katika kipindi cha wakati chenye kuelezwa katika unabii huu?” Soma 2 Timotheo 3:1-4, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 9.
◼ “Watu wengi wanajiuliza kwa nini matatizo ya wanadamu yanazidi kuongezeka. Je, umepata kufikiria maelezo yenye kutolewa katika andiko hili kuwa ndio sababu?” Soma Ufunuo 12:9, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 10.
◼ “Je, umewahi kutaka kujua jibu kwa ulizo kama hili?” Soma Ayubu 21:7, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 11.
◼ “Je, unafikiri kwamba kutumia shauri hili la Biblia maishani kunaweza kusaidia watu wawe na maisha ya familia yenye furaha?” Soma Waefeso 5:33, na acha mtu ajibu. Kisha kazia sura ya 14.
[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 6]
Funzo la Biblia linaweza kuripotiwa ikiwa limeongonzwa mara mbili baada ya kumwonyesha mtu namna ya kujifunza na ikiwa kuna sababu ya kuamini kwamba funzo litaendelea.