Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
ICHUNGWE
Tumia mapendekezo yafuatayo ili yakusaidie kutayarisha utoaji mbalimbali kuhusu toleo la mwezi.
Mkaribie Yehova
“Watu wengi wanaomwamini Mungu watapenda kujisikia kuwa karibu zaidi naye. Je, ulijua kwamba Mungu anatualika tumkaribie? [Soma Yakobo 4:8.] Kichapo hiki kilifanywa ili kusaidia watu watumie Biblia yao wenyewe ili kumkaribia Mungu.” Soma fungu la 1 kwenye ukurasa wa 16.
“Leo ukosefu wa haki ni mwingi. Ni kama tu inavyoelezwa hapa. [Soma Mhubiri 8:9b.] Wengi wanajiuliza hata ikiwa Mungu anajali. [Soma sentensi mbili za kwanza za fungu la 4 kwenye ukurasa wa 119.] Sura hii inaeleza kwa nini Mungu ameruhusu ukosefu wa haki kwa muda.”
Je! Kuna Muumba Anayekujali?
“Tunaweza kupata wapi mashauri yaliyo bora zaidi kuhusu jinsi ya kutatua matatizo yetu makubwa zaidi yanayotusumbua? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mathayo 7:28, 29.] Hilo linaonyesha jinsi watu walivyoitikia Mahubiri ya Mlimani ya Yesu. Angalia yale ambayo wengine wamesema. [Kazia maelezo kwenye ukurasa wa 152.] Sura hii inazungumzia maisha na mafundisho ya Yesu.”
“Je, umekwisha kujiuliza: ‘Ikiwa kuna Mungu, je, atatenda wakati wowote ili kuondoa mateso na ukosefu wa haki katika ulimwengu?’ [Acha mtu ajibu. Kisha soma Ufunuo 21:3, 4.] Kitabu hiki kinaeleza yale Mungu atakayofanya ili kuondoa mateso na chanzo chayo.” Soma sura ya 10.
Endeleeni Kukesha!
“Watu wengi wanahangaishwa na matatizo na pia matukio yenye kushtua yanayoenea leo. [Taja mfano unaojulikana kwenu.] Je, ulijua kwamba mambo kama hayo ni sehemu ya alama ya ujumla inayoonyesha kwamba karibuni serikali ya Mungu itaongoza mambo ya dunia? [Acha mtu ajibu. Kisha soma andiko linalofaa, kama vile Mathayo 24:3, 7, 8; Luka 21:7, 10, 11; au 2 Timotheo 3:1-5.] Broshua hii inazungumzia kwa nini ni jambo la haraka sasa kuwa macho kuhusu maana ya matukio hayo.”
“Watu wengi leo wanataabishwa na matukio yenye kushtua au na kufiwa na mtu katika hali ya kikatili. Wengine wanajiuliza kwa nini Mungu hachukui hatua ili kuzuia mambo kama hayo. Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu atatenda karibuni ili kuondoa mateso ya wanadamu. [Soma Ufunuo 14:6, 7.] Ona lile ambalo hukumu ya Mungu itamaanisha kwa wanadamu. [Soma 2 Petro 3:10, 13.] Broshua hii ina habari zaidi kuhusu habari hii ya maana.”
Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
“Ikiwa ungealikwa kuishi katika mazingira mazuri kama haya, je, ungekubali mwaliko huo? [Onyesha picha kwenye ukurasa wa 4-5, na acha mtu ajibu.] Angalia yale ambayo neno la Mungu linasema kuwa ufunguo wa kufurahia milele aina hiyo ya maisha. [Soma Yohana 17:3.] Kitabu hiki kitakusaidia kupata ujuzi unaoongoza kwenye uzima unaodumu milele.” Chukua mipango ili kuzungumzia mafungu matano ya kwanza ya sura ya 1 kwenye ziara ijayo.
Fungua picha kwenye ukurasa wa 188-189, na ukitumia maneno yenye kueleza picha, uliza mwenye nyumba: “Je, unatumaini kuishi katika Paradiso, wakati ujuzi wa Mungu utakapojaa duniani? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Isaya 11:9.] Kitabu hiki kitakusaidia kujifunza yale ambayo Biblia inasema kuhusu Paradiso na jinsi tunavyoweza kuishiriki.” Chukua mipango ili kuzungumzia fungu la 11-16 ya sura ya 1 kwenye ziara ijayo.
Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
“Je, unafikiri kwamba ulimwengu ungekuwa nafasi bora ikiwa watu wangeishi kulingana na maneno haya? [Soma Mathayo 7:12a. Kisha acha mtu ajibu.] Kitabu hiki kinayo mafundisho mengi kutoka kwa yule mwalimu mkuu aliyepata kuishi.” Onyesha picha na maneno yenye kueleza picha kwenye sura ya 17.
“Wazazi wengi leo wanajaribu kuingiza katika akili ya watoto wao kanuni zinazofaa za maadili. Je, unafikiri kwamba jambo hilo ni la maana? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 22:6.] Angalia kwamba wazazi wanatiwa moyo kuanza kuzoeza watoto wao tangu umri mdogo. Kusudi la kitabu hiki ni kuwasaidia wafanye hivyo.” Onyesha picha na maneno yenye kueleza picha kwenye ukurasa wa 15 au 18.
“Mara nyingi wazazi wanashangazwa na maulizo ya watoto wao. Inaweza kuwa vigumu kujibu maulizo mengine, sivyo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waefeso 6:4.] Kitabu hiki kinaweza kusaidia wazazi wajibu maulizo ya watoto wao leo.” Onyesha picha fulani na maneno yenye kueleza picha kwenye sura ya 11 na 12 au 34 mpaka 36.
La vie — Comment est-elle apparue ? Évolution ou création ?
“Sisi sote tunatiwa wasiwasi na uhalifu na jeuri katika eneo letu. Je, unafikiri kwamba kuna mtu fulani anayeweza kumaliza kweli tatizo hilo? [Acha mtu ajibu.] Mungu anaweza.” Fungua ukurasa wa 196; soma na utoe maelezo kuhusu Methali 2:21, 22 katika fungu la 19. Onyesha kichwa cha sura ya 16, na utolee mtu kitabu.
Fungua kwenye ukurasa wa 6, na useme: “Watu wengi wanafikiri kwamba dunia yetu nzuri na pia uzima ulio katika dunia vimetokea kwa bahati. Unafikiri ni maelezo gani yaliyo sawa kuhusu jinsi mambo yote haya yalivyotokea? [Acha mtu ajibu.] Kuna uhakikisho tele unaothibitisha simulizi la Biblia la Muumba ambaye ni mwenye kujaa nguvu kabisa na ambaye pia anatupenda sana. Yeye ndiye Mungu wa kweli, na jina lake ni Yehova.” Soma Zaburi 83:18, na eleza kwa kifupi jinsi ni kusudi lake kugeuza dunia nzima kuwa paradiso.
Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
“Leo kuna dini nyingi sana: je! umekwisha kujiuliza jinsi gani tunavyoweza kutambua ile ambayo Mungu anakubali?” Baada ya kusikiliza jibu, fungua kitabu kwenye ukurasa wa 377. Onyesha nukta ya 7, na umuulize msikilizaji ikiwa yeye pia anafikiri kwamba dini ya kweli inapaswa kuunganisha wanadamu wote wenye rangi za ngozi tofauti. Tafuta moja ya maandiko yanayotajwa, na ikiwa wakati unaruhusu, zungumzeni kuhusu nukta zingine kwenye orodha hiyo. Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa kwa kweli, mtolee kitabu. Wakati wa kuondoka, unaweza kuuliza, “Dini ya kweli inapaswa kuwa na uvutano gani juu ya mwenendo wa mtu?” Chukua mipango ili kujibu ulizo hilo kwenye ziara ya kurudia.
Ikiwa mtu anajitambulisha kuwa mshiriki wa dini iliyo kubwa, unaweza kusema: “Ni jambo lenye kupendeza kukutana na watu wa dini mbalimbali. Wanadamu wamechukua njia mbalimbali katika kumtafuta Mungu. [Ikiwa inafaa, soma Matendo 17:26, 27.] Mara nyingi watu wanafuata dini ya wazazi wao. [Soma fungu la 12 kwenye ukurasa wa 8.] Kujifunza mengi kuhusu dini nyingine ni jambo lenye kuelimisha na lenye kufundisha. Kitabu hiki kinaeleza asili, matendo, na mafundisho ya dini kubwa ulimwenguni.” Onyesha mfano mmoja kuhusu yale yanayopatikana katika kitabu kuhusiana na dini ya mtu huyo, kama inavyopatikana kwenye kurasa zifuatazo: Wasikh (100-101); Wahindu (116-117); Wabuddha (141); Watao (164-166); Waconfucius (177); Washinto (190-195); Wayahudi (220-221); na Waisilamu (289).
Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
“Huenda ukawa umesikia kuhusu [taja habari hiyo]. Maisha yafupishwapo kwa njia yenye kuhuzunisha, wengi wanajiuliza ni faraja gani inayoweza kutolewa jamaa za waliopatwa na msiba. Unafikiri nini?” Acha mtu ajibu. Kisha fungua ukurasa wa 299 katika kitabu Upeo wa Ufunuo, na uonyeshe picha ya ufufuo. Endelea kwa kusema: “Watu wengi wanashangaa wanaposikia kwamba waadilifu na wasio waadilifu watarudishwa kwenye uzima katika Paradiso duniani. [Soma Matendo 24:15 linalotajwa kwenye fungu la 9 kwenye ukurasa wa 297, kisha utoe maelezo yanayoonyeshwa kwenye fungu la 10.] Kitabu hiki kinazungumzia habari nyingine nyingi zenye kupendeza juu ya kusudi la Mungu kuhusu wakati ujao.”
Biblia—Neno la Mungu au la Mwanadamu?
“Tunaishi wakati ambapo karibu kila mtu anapambana na matatizo mazito. Wengi wanaendea washauri wa aina zote ili kupata mwongozo. Wengine wanaendea watu walio na uwezo wa kufumbua mafumbo ili kupata msaada. Unafikiri tunaweza kupata wapi shauri la maana ambalo litatufaidi kikweli? [Acha mtu ajibu.] Biblia inaonyesha jambo la maana ambalo sisi sote tunahitaji kuelewa.” Soma 2 Timotheo 3:16. Kisha fungua kitabu kwenye ukurasa wa 187, na usome fungu la 9.] Kitabu hiki kitakusaidia uelewe jinsi kutumia mafundisho ya Biblia kila wakati kumeleta matokeo mazuri.
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
“Katika majira ya mapumziko ya Krismasi watu wengi wanafikiri kuhusu Yesu. Hata hivyo, kwa kuwa mambo mengi maovu yanatukia ulimwenguni pote, wamoja wanaweza kujiuliza ikiwa Yesu kweli anatujali. Unafikiri nini kuhusu hilo?” Acha mtu ajibu. Fungua kwenye sura ya 24, na uzungumzie kwa kifupi kwa nini Yesu alikuja duniani. Kisha usome Yohana 15:13, ukitilia mkazo upendo wenye hisia wa Yesu kwa wengine.
“Mtu anapotaja Yesu Kristo, watu wengi wanamfikiria kuwa ama mtoto mchanga ama mwanamume anayeteseka akikaribia kufa. Mawazo yao juu ya Yesu yanatia ndani kuzaliwa na kufa kwake tu. Mambo ya ajabu aliyosema na kufanya wakati wa maisha yake mara nyingi hayaonwi. Yale aliyotimiza yana uvutano juu ya kila mtu aliyepata kuishi katika dunia hii. Ndiyo sababu ni jambo la maana tujifunze mengi tuwezayo juu ya mambo mazuri ajabu aliyofanya kwa ajili yetu.” Soma Yohana 17:3. Fungua kwenye ukurasa wa kwanza wa utangulizi wa kitabu Mtu Mkuu Zaidi, na usome fungu la nne.
Mungu Anataka Nini Kwetu?
“Je! unafikiri kwamba Mungu alikusudia tusumbuliwe na magumu kama yale tunayopata leo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mathayo 6:10.] Je! Umekwisha kufikiria ili kujua ni nini kabisa Ufalme wa Mungu?” Fungua broshua kwenye somo la 6 na usome maulizo yanayoulizwa mwanzoni mwa somo hilo. Anza na kuzungumzia somo hilo, au chukua mipango ili kufanya hivyo kwenye ziara ijayo.
“Ijapokuwa maendeleo ya jamii ya kisasa, ugonjwa na kifo vinaendelea kutokeza mateso mengi na sikitiko kwa wanadamu. Je, unajua lile ambalo Yesu atafanya kwa ajili ya wagonjwa, watu wazee-wazee, na hata wafu?” Acha mtu ajibu. Ikiwa mtu anataka kupata jibu, fungua somo la 5, na usome maulizo ya fungu la 5-6. Zungumzia mafungu hayo au chukua mipango ili kufanya hivyo kwenye ziara ijayo.
Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
“Ni wapi unafikiri tunaweza kupata msaada ili kupambana na mikazo ya maisha? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waroma 15:4.] Ona kwamba Maandiko matakatifu yanatutolea maagizo, faraja, na tumaini, vinavyoweza kututia nguvu ya kuvumilia magumu. Kitabu hiki kinatoa mapendekezo yenye kusaidia kuhusu jinsi tunavyoweza kufaidika zaidi na usomaji wa Biblia.” Kazia mambo manne yanayoonyeshwa kwenye ukurasa wa 30.
“Tangu siku ambazo Yesu alikuwa duniani, watu wengi ni wenye kusali Ufalme wa Mungu uje. Je, umekwisha kujiuliza lile ambalo kuja kwa Ufalme huo kutamaanisha kwa wanadamu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Danieli 2:44.] Kitabu hiki kinaeleza Ufalme wa Mungu ni nini, kile ambacho utatimiza, na jinsi tunavyoweza kufaidika na utawala wake wenye uadilifu.” Onyesha picha kwenye ukurasa wa 92-93.