Tutolee Watu Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
◼ “Je, unafikiri kwamba ulimwengu ungekuwa nafasi bora ikiwa watu wangeishi kulingana na maneno haya? [Soma Mathayo 7:12a. Kisha acha mtu ajibu.] Kitabu hiki kinayo mafundisho mengi kutoka kwa yule mwalimu mkuu aliyepata kuishi.” Onyesha picha na maelezo ya picha kwenye sura ya 17.
◼ “Wazazi wengi leo wanajaribu kuingiza katika akili za watoto wao kanuni zinazofaa za maadili. Je, unafikiri kwamba jambo hili ni la maana? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 22:6.] Wazazi wanatiwa moyo kuanza kuzoeza watoto wao tangu umri mdogo. Kusudi la kitabu hiki ni kuwasaidia wafanye hivyo.” Onyesha picha na maelezo ya picha kwenye sura ya 15, 18, au 32.
◼ “Mara nyingi wazazi wanashangazwa na maulizo ya watoto wao. Inaweza kuwa vigumu kujibia maulizo mengine, sivyo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:14, 15.] Mama na nyanya wa Timotheo walimfundisha tangu umri mdogo kuhusu yale Maandiko yanasema. Kitabu hiki kinaweza kusaidia wazazi wafanye hivyohivyo kwa ajili ya watoto wao leo.” Onyesha picha fulani na maelezo ya picha kwenye sura ya 11 na 12 au 34 mpaka 36.