Tutoe Habari Njema Kwa Kutazamia Mema
1 Kila mmoja wetu anapenda kupata shangwe na kuridhika katika yale anayofanya, hasa katika kazi inayohusu kufanya wanafunzi. Hisia-moyo hiyo ya kuridhika inatoka wapi? Kwanza kabisa ni kwa vile tunalinda hali ya akili ya kutazamia mema huku tukitumika kwa bidii—na hilo linastahili kufanyiwa bidii—kuwasaidia wengine. (Mit. 11:25) Namna yetu ya kutoa habari njema ingepaswa kuonyesha kwamba tunaamini hakika yale tunayosema. Ikiwa tunasema na moyo wetu, hivyo unyofu wetu na imani yetu wenyewe itaonekana wazi. (Lk. 6:45) Kwa kutayarisha yale tutakayosema, tutajisikia wenye uhakika tunapozungumza na watu wa eneo letu. Hilo litakuwa hasa kweli mnamo mwezi wa Oktoba, tutakapotolea kitabu La vie : comment est-elle apparue ? Évolution ou création ? Madokezo yafuatayo yangeweza kutusaidia kutoa habari njema kwa kutazamia mema.
2 Tunapotolea kitabu “ Création ”, tunaweza kusema wakati wa kupita kwetu kwa mara ya kwanza:
◼ “Kwa kuzungumza na majirani zako, tumeona kwamba wengi wana tumaini katika Mungu, huku wengine wanaona vigumu kuamini katika yeye. Wewe unawaza nini? [Tusikilize jibu.] Angalia namna ya kufikiri ambayo Biblia inatoa kuhusu hilo. [Tusome Warumi 1:20.] Tunaweza kuona shuhuda za ‘nguvu ya milele na Uungu’ wa Mungu kwa kuangalia mambo aliyoumba. Tusome katika kitabu Création fungu la mwisho la ukurasa 48 na tuvutie uangalifu juu ya ugumu wa kutofahamika kwa chembe. Au tutumie fungu 18 kwenye ukurasa 147 ili kuonyesha jinsi mti, kupitia mfumu wake wa ajabu wa kupitishia utomvu, unaonyesha kazi ya Muumba. Tumpendekeze mtu kumwachia kitabu ikiwa anakubali kukisoma. Ikiwa anakichukua, tuonyeshe mchango wa sasa na kwa nini tunauomba.
3 Tunaporudi kuona wale ambao tulizungumza nao juu ya kuwako kwa Muumba, tunaweza kupendelea kusema:
◼ “Wakati wa ziara yangu ya mwisho, tulizungumza juu ya kile kinachoshuhudia kuwako kwa Mungu, ni kusema uumbaji wake wa ajabu. Je! unaona vigumu kuamini kwamba Yule aliyeumba ulimwengu wote anaweza kupendezwa na wakati wetu ujao? [Tuache mtu ajibu.] Unaona, wakati ujao wa mwanadamu umekwisha kujulikana na Muumba.” Tusome Isaya 46:9, 10. Kulingana na kupendezwa ambako msikilizaji wetu anaonyesha, tutumie picha na maneno yanayoandikwa kando-kando ya sura 19, katika kitabu Création, ili kukazia hali nzuri zinazoahidiwa na Mungu. Tusome baadaye fungu la 1 la sura 20 na tutolee funzo la Biblia. Ikiwa mtu anakubali, basi tuanzishe funzo kwa msingi wa kitabu Ujuzi.
4 Tunaweza kujaribu utoaji huu mwingine tunapotolea kitabu “Création”:
◼ “Kwa kuzungumza na watu wa ujirani, nimetambua kwamba wengi wanatamani sana kuishi katika usalama katika ulimwengu wenye amani. Kwa maoni yako, kwa nini wanadamu hawakufaulu kusimamisha hali hizo? [Tusikilize jibu.] Viongozi fulani wa siasa labda ni wanyofu na wanafanya mema, lakini angalia shauri hili lenye hekima la Biblia:” Tusome Zaburi 146:3, 4, kisha tuulize: “Je! kuna mtu fulani anayeweza kutosheleza mahitaji ya mwanadamu?” Tusome mistari 5 na 6. Tuonyeshe picha kwenye ukurasa 251 wa kitabu Création, na tuvutie uangalifu juu ya faida za utawala wa Mungu. Tutolee kitabu na tuonyeshe kiasi cha fedha cha kutoa.
5 Ikiwa tulizungumza mara ya kwanza juu ya utawala wa Mungu, tunaweza kujaribu utoaji huu wakati wa ziara ya kurudia ifuatayo:
◼ “Nilipopita kumepita hivi siku fulani, tulizungumza juu ya mwanadamu kutokuwa na uwezo wa kusimamisha amani ya kweli duniani. Labda unakumbuka kwamba tuliweza kuona sababu ambayo Biblia inatoa kwa kushindwa huko. [Tusome tena Zaburi 146:3.] Je! umeona kwa nini Mungu anatuomba kutotia matumaini yetu katika wanadamu? [Tuache mtu ajibu.] Utakubali kwamba tumaini lolote la suluhisho la mwisho linapaswa kutoka kwa Mungu. Zaburi 146:10 inatufasiria kwa nini tunaweza kuwa wenye kutumainia. [Tusome andiko.] Ikiwa tunataka kuwa raia wa Ufalme wa Mungu, tunapaswa kufanya nini?” Tufungue kitabu Création kwenye ukurasa 250, tusome fungu 13 na tukazie Yohana 17:3. Tupendekeze kwa msikilizaji wetu kumwonyesha jinsi, kwa njia ya funzo la Biblia, mamilioni ya watu walipata ujuzi uongozao kwenye uhai udumuo milele. Ikiwa anaruhusu, tutolee kitabu Ujuzi na tuanzishe funzo.
6 Kwa kuhubiri duka kwa duka, tunaweza kutolea kitabu “Création” kwa msaada wa utangulizi huu mfupi:
◼ “Tunafanya leo utendaji wa pekee kwa wachuuzi. Sisi sote tunahangaishwa na ongezeko kubwa la uhalifu na jeuri katika eneo letu. Je! unafikiri kwamba mtu fulani ana suluhisho kwa tatizo hilo? [Tusikilize jibu.] Mungu ana suluhisho.” Tufungue kitabu Création kwenye ukurasa 196, kisha tusome na kueleza Mithali 2:21, 22 inayotajwa kwenye ukurasa 19. Tuonyeshe kichwa cha sura 16 na tutolee kitabu.
7 Tunaporudi kumwona mchuuzi ambaye tuliachia kitabu “Création”, tunaweza kusema:
◼ “Wakati wa ziara yangu ya mwisho, nilikazia kwamba Mungu ndiye peke yake aliye hakika na suluhisho lenye kudumu kwa tatizo la mauaji na jeuri. Kulingana na ahadi yake, tunaweza kutumaini tukiwa hakika kwamba amani duniani litakuwa jambo hakika. Angalia ni mbele ya uchaguzi gani sisi tunawekwa.” Tusome kwenye ukurasa 250 wa kitabu Création fungu 11, linalotaja Zaburi 37:37, 38. Tueleze picha kwenye ukurasa 251 na tusome sentensi ya kwanza ya fungu 14. Tupendekeze funzo la Biblia kwa msikilizaji wetu, kwenye nafasi yake ya kazi au nyumbani kwake, kulingana na kupenda kwake.
8 Tukiwa “wafanya kazi pamoja na Mungu,” tunazo sababu za kuwa wenye kutazamia mema tunapotoa habari njema. (1 Kor. 3:9) Kulinda hali hiyo ya akili kutatuletea baraka nyingi za Yehova.