Tufundishe Wengine Yale Mungu Anataka Kwetu
1 Tunaweza bado kupata hesabu ya kutosha ya watu ambao walinyimwa “kuyasikia maneno ya [Yehova].” (Amosi 8:11) Wamoja wanaamini kwamba Mungu yuko, lakini hawajui wala makusudi yake wala matakwa yake. Kwa hiyo, imetupasa kuwafundisha ukweli unaookoa wa Ufalme. Ikiwa sisi ni wenye kuvalia vizuri vifaa vya kazi na tupo tayari kutoa ushuhuda kwa kila nafasi, tutapata watu wenye kutaka kujifunza yale Mungu anataka kwetu.
2 Mnamo Mei na Juni, tutatolea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yatakayokuwa na makala zenye kufaa kabisa. Zaidi ya hilo, tutatolea kwa mara ya kwanza broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Picha zake zenye kuvutia na maulizo yake yanayochochea kufikiri yanaifanya isikilike na watu wengi. Madokezo yafuatayo yanatolewa kwetu ili kutusaidia kutumia vizuri zaidi vichapo hivyo bora.
3 Tuwatafute Watu: Katika maeneo ambako watu hawapatikani nyumbani kwao tunapokwenda nyumba kwa nyumba, inaonekana kuwa jambo la lazima kuwatafuta na kuzungumza nao haidhuru mahali gani wanapopatikana. Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1996 ilitutia moyo kuhubiri habari njema mahali pote: barabarani, katika usafirishaji wa watu wote, katika mabustani, nafasi za kuegeshea magari na katika mitaa ya kibiashara. Ilituhimiza pia kwenye ulazima wa kutokeza nafasi za kuhubiri kwa namna ya vivi hivi. Kwa mfano, painia wa kike alikwenda kwenye nafasi wanapolinda wanyama mwitu akiwa na hesabu fulani ya nakala za Amkeni! ya Agosti 8, 1996 yenye kichwa cha habari “Spishi Zilizo Hatarini mwa Kutoweka—Kwa Nini Tuhangaike?” Kwa muda tu wa saa moja, aliangusha 40 kwa watu wanaopenda sana wanyama! Je! umekwisha kupata matokeo mazuri kwa kuhubiri habari njema mahali pote? Mnara wa Mlinzi, Amkeni! na broshua Anataka ni vichapo vyenye vinavyoambatana vizuri kwa namna zote za kutoa ushuhuda, kwa kuwa mambo yaliyomo yanahusu maisha ya watu na yanachochea kufikiri.
4 Tuanzishe Mazungumzo: Ukurasa wa mwisho wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1996 unatoa madokezo kamili juu ya namna ya kutayarisha utoaji wetu wenyewe wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Madokezo hayo ni yenye kufaa kuhusu kutayarisha utoaji wetu wa broshua Anataka. Maneno yetu yanaweza kuwa mafupi, sentensi chache tu, au ndefu vya kutosha ili kutaja wazo moja linalotokana na andiko la Biblia. Ni jambo la muhimu kuchagua maneno ya kwanza, kwani yatachochea labda mtu ambaye tutakaribia kwa mazungumzo kuendelea kutusikiliza au hapana. Wamoja wanapata matokeo kwa kuanza hivi: “Nilisoma makala moja iliyonitia moyo na ningependa kukuzungumzia yenyewe.” Tunaweza pia kutokeza ulizo lenye kupendeza ili kumshirikisha msikilizaji katika mazungumzo.
5 Katika utoaji wetu mbalimbali katika mwezi huu, ikiwa hilo linafaa katika eneo letu, tunaweza kujaribu kuuliza maulizo kama haya:
◼ “Leo, maandishi ya matusi kwenye vibambazi, uchafu na uchafuzi wa hewa havikosekani. Nini linahitajiwa ili kusafisha dunia na kuifanya kuwa mahali bora kabisa kuishi?” Tuache mtu ajibu na tumfasirie baadaye kwamba tunajua kwa hakika namna na wakati gani dunia nzima itageuka kuwa bustani kubwa. Tumuonyeshe katika moja ya magazeti ya mwisho elezo moja kamili, andiko fupi na picha yenye kuvutia na tumtolee gazeti lenyewe ili alisome. Kabla ya kumaliza mazungumzo, tujaribu kusikilizana ili kurudi tena kumuona msikilizaji wetu.
◼ “Je! unafikiri kwamba Mungu alitaka kutuona tukishambuliwa na magumu kama yale tunayopata leo?” Baada ya mtu kujibu, tungeweza kusema: “Labda unajua sala ambayo Yesu aliwafundisha wanafunzi wake, ndani yake anaomba kwamba Ufalme wa Mungu uje. Je! umefikiria juu ya kile Ufalme wa Mungu unaweza kuwa?” Tufungue broshua Anataka kwenye somo 6 na tusome maulizo yanayoulizwa mwanzoni mwa somo. Kisha, kwa kusoma fungu la 1, tuvutie uangalifu juu ya jibu kwenye ulizo la kwanza. Tuonyeshe kwamba jibu kwa maulizo mengine ni fupi pia. Tutolee broshua na tudokeze kuonana tena ili kuzungumzia kirefu Ufalme.
◼ “Watu wengi wenye akili wanatambua kwamba dini za ulimwengu ndizo chanzo cha matatizo ambayo mwanadamu anakabiliana nayo badala ya kuyatatua. Wewe unafikiri nini kibinafsi?” Baada ya kusikiliza maoni ya msikilizaji wetu, tutoe wazo moja la gazeti la hivi karibuni ambalo linaweza kuamsha kupendezwa kwake juu ya kutofaulu kwa dini au juu ya kuanguka kwayo hivi karibuni. Tumuulize ikiwa angependa kusoma gazeti hilo. Tuseme jina letu na tumuulize lake, tupendekeze kurudi tena kumuona ili kumfasiria kwamba dini ya kweli haiumizi wanadamu.
◼ “Kwa sababu ya magumu mengi ambayo yanazisumbua familia leo, je! haujajiuliza kamwe ni nini siri inayowezesha kupata furaha ya familia?” Tuache mtu ajibu na tumuonyeshe kwamba Mungu anafunua katika Biblia siri ya kweli ya furaha ya familia. Tungeweza labda kusoma Isaya 48:17. Kisha tufungue broshua Anataka kwenye somo 8 na tukazie maandiko fulani ya Biblia yanayotajwa yanayotoa mashauri yanayostahili kufuatwa na kila mshiriki wa familia. Tusome mfululizo wa maulizo yanayoulizwa mwanzoni mwa somo. Tumuulize mtu ikiwa angependa kusoma majibu hayo. Ikiwa ndivyo, tumtolee broshua tukimuonyesha wakati huohuo bei ya sasa. Tupendekeze kumtembelea tena ili kuzungumzia zaidi mashauri yenye kutenda kazi ya Biblia kwa ajili ya maisha ya familia yenye furaha.
6 Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1997 ilitutia moyo kujipa ujasiri (uhodari) ili kufanya ziara za kurudia. Ilidokeza kutumia broshua Anataka ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ikiwezekana wakati wa kuonana kwa mara ya kwanza, ikiwa sivyo wakati wa ziara ya kurudia. Uhitaji mkubwa zaidi wa wanadamu ni kujifunza yale Mungu anataka kwetu na, kisha, kuyatumikisha. (Kol. 1:9, 10) Tutafaidi sana jirani yetu muda wa miezi ya Mei na Juni ikiwa tunaweza kuanza kumfundisha yale tunayojua kuhusu matakwa ya Yehova kwa ajili ya uhai.—1 Kor. 9:23.