Uaminifu Unathawabishwa
1 Katika Waebrania 11:6, tunasoma kwamba Mungu “yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.” Hasa, anathawabisha watumishi wake waliojitoa kwake ‘waliowaaminifu juu ya mambo machache’ kwa ‘kuwaweka rasmi juu ya mambo mengi.’ (Mt. 25:23, TUM) Kwa maneno mengine, ili kuwathawabisha Mashahidi wake waaminifu kwa kazi yao njema, Yehova anawatolea mara nyingi mapendeleo mapya ya utumishi.
2 Kama vile thawabu kwa ajili ya uaminifu wake, mtume Paulo alikabidhiwa huduma iliyomuongoza kuzungukia miji na vijiji vya Ulaya na Asia ya Kati. (1 Tim. 1:12) Hata ikiwa angepaswa kufanya bidii nyingi ili kutimiza kikamilifu huduma hiyo, Paulo alikuwa akithamini sana pendeleo alilopata. (Rom. 11:13; Kol. 1:25) Kwa utendaji wake wenye bidii, alionyesha waziwazi kwamba alikuwa akiishi imani yake. Kielelezo chake kinatutia moyo kuthamini sana mapendeleo yetu ya utumishi.
3 Yehova Alitukabidhi Huduma: Jinsi gani tunaonyesha kwamba tunaona thawabu hiyo, pendeleo hilo, namna ileile kama Paulo? Tunatafuta njia za kuongeza kushiriki kwetu katika huduma hiyo. Tunachukua nafasi zote za kutoa ushuhuda kwa namna ya vivi hivi na nyumba kwa nyumba. Tunarudi kwa watu wote wasiokuwako na tunawatembelea upya wale walioonyesha kupendezwa. Pia, tunaheshimu ahadi ya kukutana tena tunayofanya ili kuongoza mafunzo ya Biblia.
4 Akisema kuhusu huduma, Paulo alitoa kipa moyo kifuatacho: “Sisitiza kuutangaza.” (2 Tim. 4:2, HNWW) Kusisitiza husemekana kuwa tendo la kutia mkazo juu ya jambo fulani. Je! tunatia mkazo juu ya huduma yetu kwa kuitia nafasi ya kwanza katika maisha yetu? Kwa mfano, hatungependa kuacha vidumbuizo na utendaji mwingine mbalimbali wa kibinafsi wa mwisho-juma uchukue nafasi ya wakati ambao tunapaswa kutoa kwa mahubiri. Kwa kuwa tupo hakika kwamba mwisho wa mfumo wa mambo unakaribia haraka, tupo pia hakika kwamba mahubiri ya habari njema ya Ufalme ni kazi ya maana ambayo tunapaswa kushiriki.
5 Uaminifu wetu kwa Mungu unaonekana kwa ukawaida wetu katika kazi ambayo alitukabidhi. Tutimize kiaminifu huduma yetu na Yehova atathawabisha kwa uwingi uaminifu wetu.