Mikutano Inachochea Kwenye Matendo Mema
1 Ibada yetu ina sehemu mbili za lazima: hudhurio kwenye mikutano ya kutaniko na mahubiri. Mambo hayo mawili yanakwenda sambamba na yanatenda moja juu ya lingine. Mikutano inachochea kwenye matendo mema; ingawaje hivyo mojawapo zaidi ya matendo hayo ni lile linalohusu kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Ebr. 10:24) Ikiwa tungeachilia mikutano, tungefikia haraka kuacha kuhubiri, kwani hatungechochewa kuhubiri tena.
2 Wakati wa mikutano ya kila juma, tunapokea elimu ya kiroho iliyotayarishwa ili kutuchochea kuhubiri. Elimu hiyo inatukumbusha kwamba tunaishi kipindi kigumu, na hilo linatuchochea ili kutangaza ujumbe wa uzima uliomo katika Biblia. Tunatiwa moyo na kutiwa nguvu ili kuvumilia katika mahubiri. (Mt. 24:13, 14) Ni kwa kuchukua nafasi za kutoa maelezo wakati wa mikutano kwamba tunajizoeza kutangaza imani yetu peupe. (Ebr. 10:23) Ni kwa kujiandikisha kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwamba tunajifunza kuwa wahudumu wenye matokeo zaidi na kuboresha uwezo wetu wa akili wa kufundisha.—2 Tim. 4:2.
3 Namna Mikutano ya Utumishi Inavyotuchochea Kuhubiri: Kila mmoja wetu angepaswa kusoma mbele ya wakati habari za Huduma Yetu ya Ufalme. Zitabaki hivyo kikiki katika akili zetu tutakapoziona tena wakati wa mkutano wa utumishi na wakati wa maonyesho yanayotolewa toka jukwani. Katika mahubiri, tutaweza hivyo kufikiria Huduma Yetu ya Ufalme, tukikumbuka maonyesho na, katika njia hiyo, kutoa ushuhuda wenye matokeo zaidi. Ni yale wanayofanya wahubiri wengi.
4 Wakati mkutano wa utumishi unapoendeshwa, wahubiri wengine wanachukua mipango ili kuhubiri pamoja. Wangali bado na madokezo akilini, ni wenye kuchochewa na wanatamani kuyajaribu kwa kuwa mkutano uliwatia moyo kuhubiri kila juma.
5 Hakuna kitu kinachochukua nafasi ya mikutano yetu ya Kikristo. Ni kwenye mikutano ambako washiriki wenzetu na sisi wenyewe tunaweza kuwa pamoja, na ni kwenye mikutano tunachochewa kwenye matendo mema. Je! tunapenda kwamba huduma yetu izae matunda? Kwa hiyo, tuihudhurie, na hilo kwa ukawaida. Tuonyeshe hivyo shukrani yetu kwa Yehova kwa ajili ya mpango huu wa ajabu “si kuachilia mbali kukusanyika pamoja sisi wenyewe.”—Ebr. 10:25, TUM.