Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/97 uku. 1
  • Mikutano Inachochea Kwenye Matendo Mema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano Inachochea Kwenye Matendo Mema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Tunapaswa Kukusanyika Pamoja Ili Kuabudu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Utapata Faida Gani Kama Unaenda ku Mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Kufaidika Kabisa na Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 9/97 uku. 1

Mikutano Inachochea Kwenye Matendo Mema

1 Ibada yetu ina sehemu mbili za lazima: hudhurio kwenye mikutano ya kutaniko na mahubiri. Mambo hayo mawili yanakwenda sambamba na yanatenda moja juu ya lingine. Mikutano inachochea kwenye matendo mema; ingawaje hivyo mojawapo zaidi ya matendo hayo ni lile linalohusu kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Ebr. 10:24) Ikiwa tungeachilia mikutano, tungefikia haraka kuacha kuhubiri, kwani hatungechochewa kuhubiri tena.

2 Wakati wa mikutano ya kila juma, tunapokea elimu ya kiroho iliyotayarishwa ili kutuchochea kuhubiri. Elimu hiyo inatukumbusha kwamba tunaishi kipindi kigumu, na hilo linatuchochea ili kutangaza ujumbe wa uzima uliomo katika Biblia. Tunatiwa moyo na kutiwa nguvu ili kuvumilia katika mahubiri. (Mt. 24:​13, 14) Ni kwa kuchukua nafasi za kutoa maelezo wakati wa mikutano kwamba tunajizoeza kutangaza imani yetu peupe. (Ebr. 10:23) Ni kwa kujiandikisha kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwamba tunajifunza kuwa wahudumu wenye matokeo zaidi na kuboresha uwezo wetu wa akili wa kufundisha.—2 Tim. 4:2.

3 Namna Mikutano ya Utumishi Inavyotuchochea Kuhubiri: Kila mmoja wetu angepaswa kusoma mbele ya wakati habari za Huduma Yetu ya Ufalme. Zitabaki hivyo kikiki katika akili zetu tutakapoziona tena wakati wa mkutano wa utumishi na wakati wa maonyesho yanayotolewa toka jukwani. Katika mahubiri, tutaweza hivyo kufikiria Huduma Yetu ya Ufalme, tukikumbuka maonyesho na, katika njia hiyo, kutoa ushuhuda wenye matokeo zaidi. Ni yale wanayofanya wahubiri wengi.

4 Wakati mkutano wa utumishi unapoendeshwa, wahubiri wengine wanachukua mipango ili kuhubiri pamoja. Wangali bado na madokezo akilini, ni wenye kuchochewa na wanatamani kuyajaribu kwa kuwa mkutano uliwatia moyo kuhubiri kila juma.

5 Hakuna kitu kinachochukua nafasi ya mikutano yetu ya Kikristo. Ni kwenye mikutano ambako washiriki wenzetu na sisi wenyewe tunaweza kuwa pamoja, na ni kwenye mikutano tunachochewa kwenye matendo mema. Je! tunapenda kwamba huduma yetu izae matunda? Kwa hiyo, tuihudhurie, na hilo kwa ukawaida. Tuonyeshe hivyo shukrani yetu kwa Yehova kwa ajili ya mpango huu wa ajabu “si kuachilia mbali kukusanyika pamoja sisi wenyewe.”—Ebr. 10:​25, TUM.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine