Ziara Iwezayo Kuwa Baraka
1 Kwa furaha, Zakayo alimpokea Yesu kuwa mgeni wake. Hata hivyo, ziara hiyo ilionekana kuwa baraka kweli kweli.—Lk. 19:2-9.
2 Leo, Yesu Kristo, Kichwa cha kutaniko, anaomba wazee ‘walichunge kundi la Mungu.’ (1 Pet. 5:2, 3; Yn. 21:15-17) Zaidi ya kufundisha kwenye mikutano na kuonyesha mfano katika kazi ya kuhubiri, wazee hutoa kwa upendo msaada wa kibinafsi kwa washiriki wa kutaniko. Kwa sababu hiyo, unaweza kutazamia kuwaona mara kwa mara wakikushughulikia kipekee nyumbani kwako, kwenye Jumba la Ufalme, unapohubiri pamoja nao, au katika nyakati nyingine. Je! unapaswa kuogopa ziara hizo? Hapana. Jambo la kwamba wazee wanakutembelea halimaanishi kwamba jambo fulani haliendeki. Basi, ni nini kusudi la ziara ya uchungaji.
3 Paulo alisema kwamba alitaka kuzuru akina ndugu ili ‘aone jinsi walivyokuwa.’ (Mdo. 15:36) Wakiwa wachungaji wenye kujaa upendo, wazee wanashughulikia sana kujua namna mlivyo. Wanataka kuwatolea msaada wa kiroho wenye mafaa na wenye kujenga. Yehova, Mchungaji Mkubwa mwenye kujaa upendo, anataka kwamba kila mmoja wetu apewe utunzaji wa namna hiyo.—Ezek. 34:11.
4 Tukubali Ziara ya Wazee: Paulo alipokuwa akiwatembelea ndugu zake, alikuwa na mradi wa ‘kuwapa zawadi ya kiroho kusudi wafanywe imara, na kwamba kupate kuwa na badilishano la kitia-moyo.’ (Rom. 1:11, 12) Tunahitaji sote kitia-moyo cha kiroho katika siku hizi za mwisho zilizo ngumu na tunahitaji sote msaada ili kubaki imara katika imani. Basi, acheni tukubali kwa furaha ziara za uchungaji; zitatokeza bila shaka badilishano lenye kupendeza la kitia-moyo.
5 Tutambue baraka nyingi zinazotokana na kazi ya uchungaji. Ikiwa habari fulani au swali fulani linatusumbua, tukumbuke kwamba wazee wako hapo kwa ajili ya kutusaidia. Tusisite kuwazungumzia chochote kile kiwezacho kuathiri afya yetu ya kiroho. Vilevile, tuwe wenye shukrani kwa Yehova kwa mpango wenye kujaa upendo na tufikirie kwa furaha baraka za kupokea ziara ya uchungaji.