Tutumie Broshua Ili Kugusa Akili Na Moyo
1 Kweli ya Biblia ingepaswa kutolewa kwa jinsi ya kugusa akili na moyo pia. Alipokuwa akifasiria kweli kwa wasikilizaji wake, Yesu alichagua habari zilizowapendeza na kuwachochea. (Lk. 24:17, 27, 32, 45) Matokeo mema ya huduma yetu hutegemea kwa kiwango kikubwa jitihada tunazofanya ili kutambua mahitaji ya kiroho ya wasikilizaji wetu.
2 Broshua zaweza kuwa vifaa vyenye matokeo katika kufikia akili na moyo wa watu tunaokutana nao hudumani. Tufikirie kimbele nani awezaye kuitikia ujumbe wa kila moja ya broshua zinazotolewa mnamo Septemba:
—Je! Kweli Mungu Anatujali? Watu wanaoteseka kiuchumi au walio na matatizo makubwa watathamini ujumbe wenye kufariji kuhusu wakati ujao usio na mateso.
—Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? Vijana wanaofikiria kwa uzito wakati ujao wao watafaidika kutokana na majibu ya Biblia yanayopatikana katika broshua hiyo.
—Kuishi Milele Duniani Katika Furaha! Kupitia zile picha nyingi na maandiko ya Biblia yaliyotajwa, watoto wadogo na wale walio na matatizo ya kusoma wataelewa makusudi ya Mungu.
—Serikali Itakayoleta Paradiso. Mtu yeyote ambaye kazi zake mbalimbali huhusiana na serikali au maisha ya kijamii aweza kuvutwa na ujumbe huu unaosema kwamba Ufalme wa Mungu utatatua matatizo ya ainabinadamu.
—Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Wafanyakazi wanaoandaa mambo ya mazishi huthamini kuwa na nakala za broshua hii kwa ajili ya familia zilizofiwa. Wahubiri wanaotoa ushahidi katika mashamba ya wafu hutumia broshua hii ili kufariji wenye kulia wapendwa wao. Dada wawili waliongea na familia ya watu saba waliokuwa wakisali mbele ya kaburi. Waliwajulisha ujumbe wenye kufariji wa broshua, na funzo la Biblia pamoja na mama lilianzishwa siku iliyofuata!
—Doit-on croire à la Trinité? Mtu mwenye kupenda dini sana aweza kuitikia kweli inayopatikana katika mfichuo huo wenye kutegemezwa vizuri na hati nyingi wa mafundisho ya msingi ya Jumuiya ya Wakristo.
3 Tufahamiane na kila moja ya broshua hizo na tufikirie njia bora ya kuzitumia katika eneo. Turudilie matangulizi yaliyopendekezwa kwenye ukurasa wa mwisho wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 1998. Yehova na abariki jitihada zetu za kugusa akili na moyo wa watu!—Mk. 6:34.