Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/99 uku. 1
  • Kuvaa Utu Mpya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuvaa Utu Mpya
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Endelea Kuvaa “Utu Mupya” Kisha Ubatizo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Unaweza ‘Kuvua Utu wa Zamani’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Namna Tunavua na Kuepuka Kabisa Utu wa Zamani
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Namna Tunavaa na Kulinda Utu Mupya
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 2/99 uku. 1

Kuvaa Utu Mpya

1 Wakristo hufurahi kwa kuwa wamejua kweli! Hiyo imetufundisha jinsi ya kuishi ili tuepuke mwendo wa watu wa ulimwengu. Kwa kuwa ‘wamefanywa wageni kwa uhai ambao ni wa Mungu,’ watu hao ‘wamo katika giza kiakili.’ (Efe. 4:​18) Tumekuwa tukifundishwa kufanya upya akili zetu kutoka mafikiri ya ulimwengu kwa kuvua utu wa hapo zamani na kuvaa utu mpya.​—Efe. 4:​22-​24.

2 Utu wa hapo zamani huongoza kwenye mwendo unaozidi wa kuharibika kwa adili ambao hutokeza uchafu na kifo. Kwa hiyo, tunasihi kwa moyo wale watakaosikiliza ujumbe wa Ufalme waweke mbali hasira yenye kisasi, hasira, ubaya, usemi wenye kuudhi, na maongezi yenye aibu. Wale wanaotaka kibali cha Mungu wanapaswa kuweka mbali utu wa hapo zamani kwa uthabiti na kikamili, katika njia ileile wanavyoweza kuvua nguo chafu.​—Kol. 3:​8, 9.

3 Kani Mpya Inayotendesha Akili: Kuvaa utu mpya kwatia ndani kufanywa upya katika kani inayotendesha akili zetu. (Efe. 4:​23) Mtu hufanyaje upya kani hiyo, au mwelekeo wa akili, ili ielekezwe katika njia inayofaa? Hilo hufanywa kwa kujifunza kikawaida na kwa bidii Neno la Mungu na kutafakari maana yake. Ndipo, namna mpya ya kufikiri husitawi, na ndipo mtu huona mambo kama vile Mungu na Kristo wayaonavyo. Maisha ya mtu hubadilika kadiri anavyositawisha sifa nyingi zilizo kama zile za Kristo, kutia ndani shauku nyororo za huruma, fadhili, hali ya akili ya kujishusha, upole, ustahimilivu na upendo.​—Kol. 3:​10, 12-​14.

4 Kwa kuvaa utu mpya, tunawekwa kando kutoka ulimwengu. Namna yetu ya maisha hutufanya tuwe tofauti. Tunasema kweli na tunatumia usemi ulio safi ili kujenga wengine. Tunazuia hasira yetu na tunafanya sifa zenye uadilifu na za kimungu zichukue nafasi ya uchungu, kupiga kelele, matukano na ubaya wote. Kwa kuwa wenye kusamehe, tunafanya zaidi ya yale tunayoombwa. Yote hayo hutayarishwa kutoka moyoni.​—Efe. 4:​25-​32.

5 Usivue kamwe utu mpya. Bila huo, hatuwezi kumtumikia Yehova kwa njia yenye kukubaliwa. Acha huo uvute watu kwenye kweli, na acha huo umtukuze Yehova, Muumba wa utu wetu mpya wa Kikristo ulio wa ajabu.​—Efe. 4:​24.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine