Jinsi Washiriki wa Familia Wanavyofanya Kazi Pamoja ili Kushiriki Kikamili—Katika Huduma
1 Ni jambo gani lingekuwa lenye kuchangamsha kuliko kuona waume na wake, wazazi na watoto wakifanya kazi pamoja katika huduma ya Kikristo, wakitukuza jina la Yehova hadharani? (Zab. 148:12, 13) Familia zote zingepaswa kuwa na programu nzuri ya kushiriki kikawaida katika utumishi wa shambani. Je! familia yako inayo siku iliyowekwa kila juma ya kupitisha katika huduma? Ikiwa ndiyo, basi kila mmoja anajua vizuri mambo ya kufanyia mipango na anaweza kushiriki kikamili.—Mez. 21:5a.
2 Kabla ya siku ya familia kwa ajili ya utumishi, kwa nini usifanye mradi wa pamoja ili kutayarisha habari ambayo familia yako itatumia? Vipindi vya mazoezi vyaweza kuwa vyenye kusaidia sana, na hivyo vyaweza kutokeza roho ya kweli ya kushirikiana kifamilia. Ni jambo lenye kudhawabisha kama nini wakati huduma ya shambani ni jambo lenye kuhusisha familia yote na wakati washiriki wote ni wenye kutayarishwa vizuri!
3 Mwangalizi mmoja msafiri alisindikiza familia nzima katika utendaji wa kugawa magazeti. Alipokuwa akifanya kazi ya kutoka nyumba hadi nyumba pamoja na mmoja wa binti, huyo binti aliuliza: “Utafanya kazi pamoja nami kwa muda gani?” Kisha akaeleza kwamba alitaka kufanya kazi pamoja na baba yake baadaye. Ilikuwa wazi kwamba yeye na baba yake kwelikweli walifurahia utumishi wao pamoja. Ni roho nzuri ya familia kama nini!
4 Familia fulani zaweza kuwa na uwezo wa kuwa mapainia wasaidizi pamoja muda wa mwezi mmoja mwakani. Au huenda ikawezekana kwa angalau mshiriki mmoja wa familia kutumikia kwa kuendelea akiwa painia msaidizi au hata kujiandikisha kuwa painia wa kawaida. Kupitia upangaji-mambo na ushirikiano vyenye kufaa, huenda washiriki wote wa familia wakawa na uwezo wa kuzidisha kushiriki kwao binafsi katika utumishi kwa kutegemeza yule anayepainia. Bila shaka, familia yote itabarikiwa na utendaji huo wenye kuzidishwa, na pia mambo mazuri yaliyoonwa ambayo wao hufurahia katika huduma.—Mal. 3:10.
5 Kushiriki kikamili katika kazi ya kueneza evanjeli kutasaidia washiriki wa familia wabaki wenye kushikamanishwa kwa ukaribu, wenye bidii, wenye kuzaa matunda na wenye furaha katika utumishi wa Yehova!—Linganisha Wafilipi 2:1, 2.