Utasema nini kwa Mwislamu?
1 Je, umepata kutoa ushahidi kwa Mwislamu? Ikiwa ndiyo, huenda umetambua kwamba Waislamu wana imani yenye bidii katika Mungu. Walakini, hawajui mengi kuhusu Paradiso inayokuja juu ya dunia kama ilivyotabiriwa na manabii wa Yehova, na tungetaka kushiriki tumaini hilo pamoja nao. (1 Tim. 2:3, 4) Habari ifuatayo ingepaswa kukusaidia utoe ushahidi mzuri.
2 Waislamu huamini Allah, au Mungu, na wanaamini kwamba Muhammad ni nabii wa Mungu. Kitabu chao kitakatifu ni Qurani, na dini yao inaitwa Uislamu, neno linalomaanisha “unyenyekeo.” Qurani inasema kwamba uwongo na ibada ya sanamu ni makosa, kwamba Mungu ni mmoja, na kwamba yeye si sehemu ya Utatu. Pia, inafundisha kutokufa kwa nafsi, moto wa helo, na paradiso ya mbinguni. Waislamu hukubali Biblia kuwa Neno la Mungu lakini wanaamini kwamba hiyo imebadilika, huku Qurani ikiwa imelindwa ikiwa safi kwa kuwa hiyo ingali katika lugha yake ya awali.
3 Uwe mwenye urafiki, mwenye busara, na mwenye utambuzi: Unaposhiriki mazungumzo pamoja na Mwislamu, uwe mwenye urafiki na mwenye busara. (Mez. 25:15) Linda akilini kwamba imani za Kiislamu ni zenye kusitawishwa kwa uthabiti na kwamba nyingi za hizo zimefunzwa kwa ufahamu. Hivyo, kufikiri juu ya mafundisho ya kidini na kujihakikishia wenyewe nini iliyo mapenzi ya Mungu kumekuwa si sehemu ya ukuzi wao wa kiroho. (Rom. 12:2) Ili kusaidia Waislamu, uvumilivu na uelewevu ni vya lazima.—1 Kor. 9:19-23.
4 Epuka kutumia semi ambazo zingefanya Mwislamu aseme akilini mwake kwamba wewe ni mshiriki wa Jumuiya ya Wakristo. Fanya iwe wazi kwamba wewe si sehemu ya dini ya Katoliki wala ya Protestanti, kwamba wewe ni tofauti. Taja Biblia kuwa Kitabu cha Mungu. Kwa kuwa Waislamu huchukia neno “Mwana wa Mungu,” kwa kawaida ni vizuri zaidi kutolitumia au kutozungumzia habari hiyo hadi maendeleo ya kiroho yatakapofanywa. Hata hivyo, unaweza kusema juu ya Yesu, ukimwita nabii au mjumbe. Epuka ubishi. Ikiwa unatambua kwamba hasira inaanza kupanda, ondoka kwa adabu mara moja.
5 Ni vizuri zaidi kusema na mtu moja tu, si na kikundi. Kwa kawaida, inashauriwa kwa wanawake kutoa ushahidi kwa wanawake, na wanaume, kwa wanaume. Bila shaka, wakati mwingine wanawake wanaweza kutoa ushahidi kwa wanaume, na wanaume, kwa wanawake, lakini uamuzi mzuri ungepaswa kutumiwa. Pia, Waislamu wengi hukwazwa kwa urahisi na kile wanachoona kuwa mavazi na kujipamba kusiko na kiasi kwa wanawake. Akina dada wanahitaji kuwa waangalifu kuhusu jambo hilo.—1 Kor. 10:31-33.
6 Mambo ya kuzungumzia: Sema bila kuficha mambo kuhusu ukubwa wa Mungu na upendo wake. Usisite kusema kwamba wewe ni mwamini wa kweli, kwamba Mungu ni mmoja (si Utatu), na kwamba ibada ya sanamu ni kosa. Sema kuhusu uovu katika ulimwengu wa leo—vita, msukusuko wa kiraia, chuki kuelekea rangi ya ngozi, na unafiki ulio wazi kati ya watu wa kidini wengi sana.
7 Broshua La direction venant de Dieu : le chemin qui mène au Paradis itakupa ufahamu wenye kina kuhusu vichwa vya mazungumzo ambavyo vinaweza kutumiwa ili kuanzisha mazungumzo na Waislamu. Hiyo imetayarishwa ili ivutie Waislamu wanaoishi katika mazingira ambamo wanaweza kuwa huru kujifunza Biblia.
8 Kama vile utoaji, unaweza kusema:
◼ “Ninafanya jitihada ya pekee ili kuzungumza na Waislamu. Nimekuwa nikisoma kuhusu dini yenu na ninatumaini kuwa ni sawa ikiwa ninasema kwamba Waislamu huamini Mungu mmoja wa kweli na manabii wote. [Acha mtu ajibu.] Ningependa kuzungumza nawe kuhusu unabii wa kale ambao unatabiri kugeuka kwa dunia kuwa paradiso. Je, ninaweza kukusomea yale ambayo nabii aliandika? [Soma Isaya 11:6-9.] Unabii huu unanifanya nifikiri juu ya mtajo kutoka katika Qurani ambao unapatikana katika broshua hii.” Fungua ukurasa 9 katika broshua Direction venant de Dieu, na usome mtajo wenye miandiko myeusi ambao unasema juu ya kurithi dunia kwa wenye haki. Ikiwa kupendezwa kunaonyeshwa, endelea na mazungumzo kwa kuzungumzia mafungu 7 hadi 9 kwenye ukurasa wenye kufuata. Mtolee mtu broshua, na uchukue mipango kwa ajili ya ziara ya kurudia.—Ili kupata utoaji mwingine, ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998, ukurasa 6, fungu 26.
9 Wakati wa kualika mtu fulani kuchunguza broshua Direction venant de Dieu, ni vizuri zaidi kuita hilo mazungumzo, si funzo la Biblia. Wakati mnapomaliza broshua, mwanafunzi angepaswa kuwa tayari kujifunza broshua Anataka au kitabu Ujuzi. Vichapo vingine vilivyotayarishwa kipekee kwa ajili ya Waislamu ni trakti Le chemin du paradis : Comment le trouver? na kijitabu Le temps de la vraie soumission à Dieu.
10 Tukiwa na ujuzi huu kuhusu imani za Waislamu na mambo yanayowakwaza, tunaweza kuwa wenye utambuzi katika kuchagua vichapo vya kutolea Waislamu na katika namna ya kuwatolea ushahidi. Yehova na aendelee kubariki jitihada zetu za kusaidia watu wa namna zote kuitia jina lake na kuokolewa.—Mdo. 2:21.