Tuhubiri Watu Wa Lugha Zote Na Dini Zote
1 Katika karne ya kwanza, Wakristo walitoa kwa bidii ushahidi kwa watu waliosimulia lugha tofauti na yao na waliokuwa na dini tofauti. Matokeo? “Mnamo mwaka 100, huenda kila jimbo lililopakana na Mediterania lilihesabu jamii ya Kikristo.”—Histoire du Moyen Âge (angl.).
2 Katika maeneo yetu, kwa sababu ya kumiminika kwa wakimbizi na uhamiaji wa watu kutoka maeneo ya mashambani kwenda mijini, miji mingi sasa inakaliwa na jamii kubwa za wageni. Mara nyingi, kwa sababu ya wingi wa lugha na dini, inakuwa vigumu zaidi kujua jinsi gani kuzungumza na watu hao na namna gani kuwatolea ushahidi tunapokutana nao. Kwa kweli, labda kuna eneo la kimishonari katika mtaa wenu kibinafsi. Tunawezaje kufuata amri ya Yesu ‘ya kuhubiri watu kikamili’ na kwa watu wa lugha zote na dini?—Mdo. 10:42.
Tutoe Ushahidi Kwa Watu Wanaozungumza Lugha Nyingine
3 Ingawa ni jambo lisilo la kawaida kukutana na watu wasiozungumza lugha ya mahali, hao wanapatikana katika miji mikuu. Inafaa kwamba tujue namna ya kuwakaribia. Kwa sababu hiyo, tufaidike na mambo yaliyoonwa na ndugu zetu katika nchi nyingine ili tujue jinsi ya kukaribia watu wa aina zote.
4 Tushinde Kizuizi cha Lugha: Bila shaka, watu wengi huelewa haraka na kusikia vizuri zaidi ikiwa wanapata ufundishaji katika lugha yao ya asili. “Kwa ajili ya habari njema” na ili ‘wapate kuwa washiriki wayo pamoja na wengine,’ ndugu na dada wengi wamejifunza lugha ya kigeni. (1 Kor. 9:23) Tangu miaka mingi, dada mmoja mwenye kuzungumza Kiingereza alikuwa akimletea kikawaida magazeti mwanamke mmoja mwenye kuzungumza Kichina, lakini mwanamke huyo alikuwa amekataa kujifunza Biblia, hadi siku ambapo dada mwingine aliyekuwa akijifunza Kichina alipomtolea kitabu katika lugha yake. Alikubali kitabu na funzo la Biblia papo hapo. Jitihada za dada wa pili kwa kusema maneno machache katika lugha ya mwanamke huyo zilifanya tofauti kamili.—Ona Matendo 22:2.
5 Ni kwa sababu nzuri kwamba Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1992 ulitoa maelezo yafuatayo: “Kujifunza lugha, si kwamba tu kunakomaza uwezo wa kiakili wa vijana, lakini tena kunawafanya wawe wenye kufaa zaidi kwa tengenezo la Yehova.” Ndugu fulani washiriki wa familia ya Betheli walijitupa katika kujifunza lugha mpya, jambo linalowawezesha kujifanya wawe wenye mafaa kwa njia ya pekee katika makutaniko ambamo wanahitajiwa katika uongozi. Ikiwa unajua lugha isiyozungumzwa katika mtaa wenu, au ikiwa uko tayari kujifunza moja, unaweza pia kutegemeza kutaniko au sehemu inayozungumza lugha hiyo.—Mat. 9:37, 38.
6 Ikiwa tunajua tu lugha yetu ya asili, je! tungeweza kupanua huduma yetu kwa kujifunza lugha ya Kifaransa ambayo ndiyo lugha ya serikali ya nchi? Hivyo, tutajua kukaribia idadi kubwa zaidi ya watu. Lugha ya Kiingereza huzungumzwa katika nchi nyingi za kiafrika. Inakuwa sehemu ya programu ya ufundishaji wa shule leo. Kwa kadiri wakati mwingine inalazimishwa kwa ajili ya kazi fulani, ndivyo inaweza kutuwezesha kupanua huduma yetu ikiwa tunajifunza yenyewe. Ndivyo ilivyo kuhusu kujifunza lugha nyingine kubwa kubwa za kiafrika, kama vile lingala, Kiswahili au Kirundi.
7 Katika Kalifornia, dada mmoja painia alikuta watu wengi viziwi. Alikuwa akisali Yehova amuwezeshe kupata mtu ambaye angeweza kumfundisha lugha ya ishara, ili awe na uwezo wa kujulisha ukweli kwa viziwi. Siku moja, alipokuwa akifanya ununuzi katika soko kuu ya mtaa, mwanamke mmoja kijana kiziwi alimkaribia, akimwomba kwa kuandika msaada wake ili kupata bidhaa fulani. Baada ya kupata kile ambacho mwanamke huyo alikuwa akitafuta, dada painia alimwandikia kwamba alitamani kujifunza lugha ya ishara ili aweze kutoa tegemezo kwa watu viziwi wa mtaa. Basi mwanamke huyo akajibu, kwa kuandika tu: “Kwa nini unataka kutegemeza viziwi?” Dada akamjibu: “Mimi ni Shahidi wa Yehova na ninataka kuwasaidia waelewe Biblia. Nitakuwa mwenye furaha kukufundisha Biblia ikiwa unanifundisha lugha yenu.” Dada anaeleza: “Hamuwezi kufikiria furaha yangu mtu huyo aliponiambia: ‘Ninakubali.’” Alikwenda kwa mwanamke huyo kila jioni kwa muda wa majuma sita. Alijifunza lugha ya ishara na akafundisha mwanamke huyo ukweli, ambaye alibatizwa! Hilo lilitukia miaka 30 iliyopita, lakini dada yetu anahubiri sikuzote viziwi na kwa sasa anashirikiana na kutaniko ambamo lugha ya ishara huzungumzwa.
8 Ikiwa unasimulia kwa urahisi lugha yenye kutumiwa katika jimbo lingine au nchi nyingine na kwamba una tamaa na uwezo wa kuhamia mahali ambapo uhitaji ni mwingi katika upande huo, kwa nini usijulishe wazee wa kutaniko jambo hilo? Ikiwa wanafikiri kwamba unatimiza matakwa yanayoombwa kwa jambo hilo, uliza mwangalizi wa mzunguko wenu ikiwa kunalo eneo jirani ambako ungeweza kutumikia. Ikiwa hakuna, unaweza kutuma barua kwenye Sosaiti, ikisindikizwa na barua ya wazee wa kutaniko ambayo ndani yake watatoa maelezo yao juu ya sifa zako na uwezo wako kuhusu lugha.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1988, kurasa 21-3.
9 Tutumie Vyombo Vinavyotolewa Kwetu: Vichapo vyetu hupatikana katika lugha nyingi za kigeni. Ni jambo nzuri kuwa na trakti, au broshua Anataka ikiwa hakuna kutaniko lenye kuzungumza lugha ya kigeni katika mtaa, katika lugha zinazozungumzwa katika eneo letu. Ikiwa ni wazi kwamba Swahili siyo lugha ya asili ya mtu, tumuulize ni lugha gani anazozisoma. Hilo lingepaswa kupanua uchaguzi wa vichapo awezavyo kuvikubali. Kwa mfano, mtu anayezungumza Kirundi anaweza labda kusoma Kiswahili.
10 Hata ingawa hatuzungumze lugha ya mtu tunayemkuta katika mahubiri, labda tuna uwezo hata hivyo wa kumtolea habari njema. Namna gani? Kwa kutumia broshua Une bonne nouvelle pour toutes les nations. Ndani yake ina ujumbe mfupi katika lugha 59. Kama vile maagizo ya ukurasa 2 yanavyoonyesha, baada ya kujua lugha ya msikilizaji wetu, tumsomeshe ushahidi wenye kuchapwa kwenye ukurasa unaofaa wa broshua. Baadaye, tumtolee kichapo katika lugha yake. Ikiwa hatuna nacho, tumwonyeshe kichapo katika Kifaransa. Tumwambie kwamba tutajaribu kurudi tukiwa na kichapo chenye kuandikwa katika lugha yake. Tumuulize jina lake na tuliandike, vilevile na anwani yake. Inawezekana kutoa habari kwa kutaniko au sehemu ya karibu zaidi inayozungumza lugha hiyo, kwa msaada wa fomu “Intérêt à suivre dans une langue étrangère.” (S-70a) Ili kujua mengi zaidi juu ya namna ya kufikisha habari kwa watu wenye kuhusika, angalieni Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1994, ukurasa 2. Ikiwa hakuna mtu anayezungumza lugha hiyo ili kufanya ziara ya kurudia, tunaweza kuchukua daraka hilo, labda hata kwa kujifunza pamoja na mtu na kwa kufuata kichapo cha Kifaransa.—1 Kor. 9:19-23.
Tutoe Ushahidi kwa Watu Walio na Dini Isiyo ya Kikristo
11 Kuwa na ujuzi fulani wa maana ya kidini ya watu kunatuwezesha kuwatolea kwa matokeo ushahidi kuhusu Ufalme wa Mungu. Kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu kinatufanya tupate kujua kwa upana dini zilizo kubwa zaidi za ulimwengu, kikitutolea uelewevu wa kutosha wa imani za watu ili kuwasaidia kujua ukweli.
12 Orodha ya ukurasa wa mwisho wa nyongeza hii inaonyesha orodha ya kisasa ya vichapo ambavyo tengenezo la Yehova linatoa kwa ajili ya mahubiri kwa watu walio na dini isiyo ya Kikristo. Kwa kusoma vichapo hivyo, tutaelewa namna ya kuzungumzia watu habari njema. Tusisahau chombo cha thamani ambacho ni kitabu Kutoa Sababu. Katika kurasa 21-4 za kitabu hicho kunatolewa madokezo yenye kutenda kazi juu ya namna ya kujibu wabudha, wahindu, wayahudi na waislamu.
13 Tuwe Waangalifu kwa Yale Tunayosema: Haifai kutia alama washiriki wa dini fulani kwa kuwazia kwamba imani zao za kibinafsi huwa bila shaka sawasawa na zile za washiriki wengine wa madhehebu hayo. Badala yake, tujitahidi kusikia namna anavyofikiri mtu tunayezungumza naye. (Mdo. 10:24-35) Tangu utoto wake, Salimooni alifundishwa kwamba Kurani ilikuwa Neno la Mungu. Hata hivyo, alikuwa hajapata kufaulu kamwe kukubali fundisho la kiislamu linaloonyesha Mungu kuwa mtu mwenye rehema isiyo na mipaka, lakini anayetesa watu katika helo yenye kuwaka moto. Siku moja, Mashahidi wa Yehova walimwalika kwenye mkutano. Alitambua sauti ya ukweli, na sasa yeye ni mwenye furaha kutumikia daraka la mzee katika kutaniko la Kikristo.
14 Wakati tunapohubiri watu walio na imani zisizo za Kikristo, tunapaswa kuwa wenye busara ili kwamba utangulizi wetu usituzuie kuzungumza nao juu ya habari njema. (Mdo. 24:16) Washiriki wa dini fulani huwa wasiovumilia majaribio yanayolenga kuwageuza kutoka imani yao. Tujitahidi basi kupata mambo ambayo juu yayo tunaweza kupatana ili kuwavuta kuelekea kweli za Biblia. Watu wenye mfano wa kondoo wataitikia utangulizi wenye wema na utoaji ulio wazi wa ukweli.
15 Ni jambo la maana pia kuchagua pia maneno tunayotumia, ili yasije yakawatenga watu isivyofaa mbali na ujumbe wetu. Kwa mfano, ikiwa tunasema waziwazi kwamba sisi ni Wakristo, inawezekana kwamba msikilizaji wetu atushirikishe moja kwa moja na Makanisa ya Jumuiya ya Wakristo, jambo ambalo lingeweza kuwa kizuizi. Ni jambo lenye busara pia kutaja Biblia kwa kusema juu ya “Maandiko” au “maandishi matakatifu.”—Mt. 21:42; 2 Tim. 3:15.
16 Ikiwa tunakutana na mtu wa dini isiyo ya Kikristo na kwamba tunahisi kutokuwa na uwezo wa kutoa ushahidi papo hapo, tuchukue tu nafasi hiyo ili kutafuta habari, tuache trakti, tutoe jina letu na tuandike lile la mtu. Kisha siku moja au mbili baadaye, baada ya kujitayarisha vizuri, tunaweza kufanya ziara ya kurudia ili kutoa ushahidi.—1 Tim. 4:16; 2 Tim. 3:17.
17 Kuhubiri Wabudha: (Ona sura 6 ya kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.) Imani ya wabudha hubadilika kutoka mshiriki mmoja hadi mwingine. Dini ya kibudha haifundishi kuwako kwa Muumba, bali inachukua Boudha Gautama, mhindi aliyeishi katika karne ya sita kabla ya wakati wetu, kama mfano wa ukamilifu wa kidini. Alipoona mara ya kwanza mtu mgonjwa, mtu mzee na mtu aliyekufa, Bouddha aliudhika juu ya maana ya uhai. ‘Je! mtu huzaliwa tu kwa ajili tu ya kuteseka, kuzeeka na kufa?’ akajiuliza. Tunaweza bila shaka kutoa jibu kwa swali hilo kwa wabudha wanyofu wanaotamani hilo.
18 Ikiwa ingefika kwamba tuzungumze na wabudha, tushikamane na ujumbe wenye kutazamia mema na kweli zilizo wazi zinazotolewa katika kitabu kikubwa cha vitabu vitakatifu vyote, Biblia. Kama vile watu wengi, wabudha wanapendezwa sana na amani, adili na maisha ya familia, na wanathamini kwa kawaida kuzungumzia hayo. Hilo linaweza kutuongoza kuonyesha Ufalme kama suluhisho pekee la kweli kwa matatizo ya ulimwengu.
19 Tangu zaidi ya miaka kumi, dada painia wa Nevada katika Shirikisho la Amerika alikuwa akifundisha ukweli kwa wanachuo wachina. Siku moja alipokuwa akihubiri katika jengo lenye makao nane lenye kukaliwa na wanachuo hao, alisali Yehova amsaidie aanzishe funzo la Biblia katika kila makao. Katika majuma mawili, alikuwa akijifunza na angalau mwanachuo mmoja katika kila makao. Dada huyo anapata matokeo mazuri kwa kusema katika utangulizi wake kwamba alitambua kwa wanachuo hangaiko moja: utafutaji wa amani na furaha. Anawauliza ikiwa hilo ni hangaiko lao pia. Jibu lisilobadilika huwa “ndiyo.” Kisha anaongoza uangalifu wao kwenye broshua La paix et le bonheur sans fin : comment les trouver ? (Kiingereza), iliyofanywa kwa ajili ya Wachina. Baada ya kujifunza tu mara tano, mwanachuo mmoja alimwambia kwamba hatimaye alikuwa amepata ukweli aliokuwa akiutafuta kwa muda mrefu.
20 Kuhubiri Wahindu: (Ona sura 5 ya kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.) Hakuna imani ya pekee katika uhindu. Falsafa (filozofia) yake ni yenye mambo mengi sana. Mungu mkuu wa Wahindu, Brahma, ni mungu wa utatu (Brahma Muumbaji, Vishnu mhifadhi wa uhai, Siva kijimungu cha uharibifu). Imani katika kutokufa kwa nafsi ndiyo msingi wa mafundisho kuhusu kuzaliwa upya katika mwili mwingine, inayoelekea kutolea Wahindu maoni ya kwamba mambo yote yamepangwa kimbele juu ya uhai. (Ona kitabu Kutoa Sababu, kurasa 154-8, na Mnara wa Mlinzi wa Mei 15, 1997, kurasa 3-8.) Uhindu hutetea kuvumiliana na hutegemeza kwamba dini zote huishia kwenye kweli moja.
21 Ili kuhubiri mhindu, ni vizuri kumwonyesha tumaini letu la kuishi duniani katika ukamilifu, na pia majibu yenye kutosheleza ambayo Biblia hutoa kwa maswali ya maana ambayo hujitokeza kwa wanadamu.
22 Kuhubiri Wayahudi: (Ona sura 9 ya kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.) Kinyume na dini nyingine zisizo za Kikristo, Uyahudi una mizizi yake katika Historia, na si katika hadithi za kutunga za miungu. Utafutaji wa Mungu wa kweli ambao kwa huo wanadamu hujitoa hupitia kwa vyovyote Maandiko ya kiebrania yaliyoongozwa kwa roho ya Mungu. Hata hivyo, imani hiyo katika kutokufa kwa nafsi ni mafundisho yenye msingi wa Uyahudi wa sasa, jambo linalopingana na Neno la Mungu. Inawezekana kukubaliana kwa kukazia kwamba tunaabudu Mungu wa Abrahamu na kwamba sisi sote tunapata matatizo yale yale katika ulimwengu wa sasa.
23 Ikiwa tunazungumza na Myahudi anayekosa imani katika Mungu, tutajua vizuri zaidi jinsi ya kumgusa moyo kwa kumuuliza ikiwa amekuwa sikuzote katika hali hiyo. Kwa mfano, labda hajapata kamwe kusikia mafasirio yenye kutosheleza juu ya Mungu kuruhusu kuteseka. Tunaweza kualika Wayahudi wanyofu kuchunguza upya yale yanayoonyesha Yesu kuwa Masiya kwa mwangaza wa yale ambayo waandikaji wa Maandiko ya Kigiriki waliyoyasema, na si kupitia sura iliyoharibiwa inayoonyeshwa na Jumuiya ya Wakristo.
24 Kuhubiri Waislamu: (Ona sura 12 ya kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.) Waislamu wanaamini Uislamu (au umuhammadi), yaani imani katika Allah, uungu mmoja wenye kukubaliwa, na katika Muhammad (570-632 W.K.), nabii wa mwisho na wa maana zaidi ya wote. Kwa kutokubali kwamba Mungu ana mwana, Waislamu wanaona Yesu kuwa tu nabii wa pili wa Mungu. Kurani, iliyo na miaka chini ya 1, 400 inanukuu kwa wakati uleule Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki. Kuna ufanani mwingi kati ya Uislamu na Ukatoliki. Dini hizo mbili hufundisha kutokufa kwa nafsi, hali ya mateso ya wakati kidogo na kuwako kwa helo ya moto.
25 Tunaamini Mungu mmoja wa kweli na tunaona Biblia kuwa kitabu kilichopuliziwa na yeye, jambo linalofanya hakika kuwe na makubaliano. Usomaji wenye uangalifu wa Kurani unafunua kwamba Torati, Zaburi na vitabu vya evangeli vinahesabiwa kuwa Neno la Mungu, kwamba inafaa kuvichukua kama vile vilivyo na kuvitumia. Hilo linaweza kutuleta tupendekeze kujifunza sehemu hizo za Biblia na msikilizaji wetu.
26 Utangulizi ufuatao utakuwa labda wenye matokeo kwa mtu anayekiri kuwa mwislamu: “Sikuzungumza mara nyingi na waislamu, lakini nimepata katika kitabu hiki habari fulani juu ya imani zenu. [Tufungue kitabu Kutoa Sababu kwenye ukurasa 24.] Inasemwa kwamba mnaamini kwamba Yesu alikuwa nabii, lakini kwamba Muhammad alikuwa nabii wa mwisho na wa maana zaidi ya wote. Je! unaamini pia kwamba Musa alikuwa nabii wa kweli? [Tuache mtu ajibu.] Je! ninaweza kukuonyesha yale ambayo Mungu alifundisha Musa juu ya jina lake la pekee?” Kisha tusome Kutoka 6:2, 3. Wakati wa ziara ya kurudia, tungeweza kuzungumzia kichwa kidogo “Mungu mmoja tu, dini moja tu” kwenye ukurasa 13 wa broshua Le temps de la vraie soumission à Dieu.
27 Inawezekana kwamba usikute hali hizo zote katika eneo lenu. Hata hivyo, kila mmoja wetu anaweza kupanua huduma yake kwa kujifunza lugha nyingine zaidi ya ile anayoisema kwa ukawaida au kwa kuhamia kwa mtu kujitakia mwenyewe katika eneo lingine. (Isaya 6:8) Leo, wengi hutenda kwa kupatana na yale Isaya 55:6 inayosema, ambapo tunasoma: “Mutafute BWANA [Yehova, NW] angali anaweza kupatikana. Mumwite angali yeye ni karibu.” Hilo linatumika kwa watu wanyofu wote, lugha yao au dini yao iwe ni gani. Tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atabariki jitihada zetu ili kwenda na ‘na kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’—Mat. 28:19.
[Box on page 6]
VICHAPO KWA AJILI YA WATU WASIO WAKRISTO
Wabudha
À la recherche d’un père (Broshua, Kifaransa).
“ Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” (Broshua aina kubwa).
Wachina
La paix et le bonheur sans fin : comment les trouver ? (Broshua aina kubwa).
Wahindu
De Kurukshetra à Harmaguédon et à votre survie (Broshua).
La victoire sur la mort : est-elle à votre portée ? (Broshua).
Le chemin de la liberté : la vérité divine (Broshua).
Nos problèmes — Qui nous aidera à les résoudre ? (Broshua aina kubwa).
Pourquoi adorer Dieu en amour et en vérité ? (Broshua aina kubwa).
Wayahudi
Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? (Broshua aina kubwa).
Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini? (Trakti T-18).
Un monde nouveau de paix : Le verrons-nous un jour ? (Trakti T-17).
Waislamu
Le chemin du Paradis : Comment le trouver ? (Trakti).
Le temps de la vraie soumission à Dieu (Broshua).