Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuhubiri Mutu Mwenye Kuzungumuza Luga Ingine
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Yehova anataka watu wa “kila taifa” wakuwe na hali nzuri ya kiroho. (Mdo. 10:34, 35) Yesu alisema kama habari njema itahubiriwa “katika dunia yote inayokaliwa” na “kwa mataifa yote.” (Mat. 24:14) Nabii Zekaria alisema kama watu ‘kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga’ watakubali ujumbe huo. (Zek. 8:23) Mutume Yohana aliona katika maono, watu ‘kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga’ wakiokoka ziki kubwa. (Ufu. 7:9, 13, 14) Kwa hiyo, wakati tunakutana mutu mwenye kuzungumuza luga ingine, tunapaswa kujikaza kumuhubiria.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Katika Ibada ya Familia ya mangaribi, mufanye mazoezi ya kuhubiri mutu mwenye anazungumuza luga ingine.